mambo ya nje
-
Araghchi: Hatua Yoyote ya Uhasama Dhidi ya Iran Itajibiwa kwa Haraka na kwa Nguvu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa Iran itatoa jibu la haraka na la maamuzi kwa hatua yoyote ya uhasama, akisisitiza kuwa malengo yaliyoshindikana kufikiwa kwa vikwazo na vita hayawezi kupatikana kwa vita zaidi.
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Kulaani Haki ya Iran ya Kujilinda ni Unafiki wa Wazi
Ismail Baqaei amesema taarifa ya Umoja wa Ulaya ya kulaani hatua za Iran za kujibu mashambulizi ya Marekani inaonyesha unafiki na viwango viwili, akisisitiza kuwa Iran ilitumia haki yake halali ya kujilinda kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
-
Mkutano wa Balozi wa China mjini Kabul na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban kuhusu vifo vya raia wa China mpakani mwa Afghanistan na Tajikistan
“Balozi wa China mjini Kabul, katika mkutano na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban, alitaja mashambulio ya hivi karibuni dhidi ya wafanyakazi wa China katika eneo la mpakani kati ya Tajikistan na Afghanistan — ambayo yamesababisha vifo vya watu 5 na kuwajeruhi wengine kadhaa — kuwa ‘kitendo cha maadui kwa ajili ya kuleta kutokuaminiana’. Pia aliishukuru Taliban kwa kuanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran | Atoa Onyo kwa Marekani : "Hatutavumilia ukiukwaji wa sitisho la mapigano, Sisi sio kama Lebanon"
Kauli hii ni onyo kali kwa Marekani na washirika wake dhidi ya uvunjaji wowote wa makubaliano ya amani au usitishaji wa mapigano katika muktadha wa mvutano wa kijeshi unaoendelea katika eneo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran:
"Kila afisa wa Kijeshi au Mwanasayansi wa Nyuklia wa Iran anayeuliwa Kigaidi, kuna wengine mia moja nyuma yake walioko tayari kuchukua nafasi yake"
Abbas Araqchi alisema: "Tofauti na utawala wa Kizayuni, Iran haitaficha kamwe hasara zake na inajivunia Mashahidi wake kama vielelezo vya ujasiri. Taifa la Iran litasimama kidete dhidi ya yeyote anayejaribu kuliamulia mustakabali wake hadi tone la mwisho la damu".
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Haki za Nyuklia za Iran Lazima Ziheshimiwe Katika Mazungumzo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Uhuru wa Kisiasa ni Asili ya Sera ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu – Haki za Nyuklia Lazima Zihifadhiwe Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mazungumzo maalum amesisitiza kuwa uhuru wa kisiasa ni nguzo kuu ya sera ya kigeni ya Iran, akieleza kuwa taifa hilo limekuwa likijitahidi daima kujiepusha na utegemezi au kuingiliwa na madola ya kigeni.