moyo
-
Adabu Muhimu Miongoni mwa Adabu za Kusoma Qur’an Tukufu
Qur’ani si kitabu cha kusomwa kwa macho na kufahamika kwa fikra pekee. Qur’ani ni minong’ono ya Mola kwa nyoyo zilizo na masikio ya roho. Adabu ya tilawa si sura za nje tu; adabu ya kusoma Qur’ani ni kutambua kuwa umeingia katika uwepo wa Allah, na kwamba kila aya ni pumzi kutoka kwa Mola wa walimwengu, na wewe ndiye unayeambiwa.
-
Wanafunzi wa Chuo cha Kimataifa cha Al-Mustafa (s) Foundation wakihuisha Usomaji wa Dua ya Nudba Leo hii Mbezi Beach, Jijini Dar-es-Salaam
Matukio kama haya ya Usomaji wa Dua mbalimbali yanaongeza moyo wa ibada miongoni mwa wanafunzi na hutoa nafasi ya kuungana kiroho katika jamii ya hawza hiyo, huku yakihimiza umuhimu wa dua kama silaha ya waumini katika maisha ya kila siku.
-
Sheikh Dkt. Reihan Yasin: "Nafasi ya Vijana Katika Mapinduzi ya Imam Hussein(as) Katika Ardhi ya Karbala"
Vijana Waumini wa Kiislamu walicheza nafasi muhimu, yenye ufanisi mkubwa na athari chanya katika Vita vya Karbala. Karbala ilikuwa imejaa vijana, na mmoja wao alikuwa ni "Qasim bin Hassan". Alikuwa kijana na shujaa, na pia alikuwa anayo maanadalizi ya kutosha, kwa sababu alikuwa na moyo safi na wenye utimamu.
-
"Kuna Wivu wa Husuda na Wivu Ghibta | Je, Tuwe na Wivu wa Aina ya Ghibta au Tusiwe nao?"
Husuda ni kutamani neema ya mtu mwingine itoweke, iwe neema hiyo itamfikia mwenye husuda au la. Kinyume cha husuda ni 'Ghibta', ambapo mtu hatamani neema ya mwingine ipotee, bali anatamani kuwa na neema kama hiyo bila kumtakia mwingine mabaya.