Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limedai kuharibu rada za Marekani za udhibiti wa baharini katika Miamba ya Salamah na rada ya udhibiti wa anga katika eneo la Ghanam nchini Oman, katika mwendelezo wa operesheni iliyopewa jina la "Nasr 2 / Ushindi 2".
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limedai kuwa limeharibu miundombinu ya kijeshi ya Marekani nchini Bahrain pamoja na mifumo ya rada nchini Oman, likisema operesheni hiyo ni sehemu ya awamu ya tano ya mashambulizi ya kulipiza kisasi.
Rada ya Iran aina ya "Kavosh" pamoja na mizinga ya HM-40 vimeonekana katika gwaride la kijeshi nchini Armenia, jambo linaloashiria kuendelea kwa ushirikiano wa kijeshi kati ya Tehran na Yerevan.