Wabunge wa Iran wamevaa sare za IRGC na kutangaza azimio la kuyachukulia majeshi ya Ulaya kama makundi ya kigaidi, ikiwa ni jibu la hatua ya Ulaya kulitaja Jeshi la Ulinzi wa Mapinduzi la Iran kuwa kundi la kigaidi.
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (SEPAH) wa Eneo Kuu la RASHT, Kanali Hassan Amini, ametangaza kuhusu kuanzishwa kwa mahema ya wananchi katika barabara ya watembea kwa miguu ya kiutamaduni ya Manispaa ya Rasht kwa mwaka wa nne mfululizo, na kusema kuwa mahema haya, yenye programu za kitamaduni, huduma na kidini, yatapokea wageni na wapenzi wa Sayyid al-Shuhadaa (a.s.) hadi mwisho wa mwezi wa Safar.