Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Leo, wabunge wote wa Iran walivaa sare za kijeshi za Jeshi la Ulinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ndani ya Bunge, na kutangaza azimio rasmi la kuijibu Ulaya kwa kuyachukulia majeshi ya nchi za Ulaya kama makundi ya kigaidi.
Hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya nchi za Ulaya kuchukua hatua ya kulitangaza Jeshi la Ulinzi wa Mapinduzi la Iran kuwa kundi la kigaidi. Jambo hilo limeifanya Iran kujibu kwa msimamo sawa, kwa kuyaweka majeshi ya Ulaya katika orodha ya makundi ya kigaidi kimtazamo wa Tehran.
Wachambuzi wanaona kuwa hatua hii ni sehemu ya vita vya kisiasa na kisaikolojia kati ya Iran na Ulaya, na inaashiria kuongezeka kwa mvutano katika uhusiano wa pande hizo mbili.
Your Comment