azimio
-
Barua ya Iran, Urusi na China kwa Grossi: Wajibu wa Kuripoti wa IAEA Umefikia Mwisho
Wawakilishi wa kudumu wa Iran, Urusi na China katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) wamemwandikia barua rasmi Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa wakala huo, wakisisitiza kuwa kwa kumalizika kwa muda wa utekelezaji wa Azimio la 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jukumu la IAEA la kuwasilisha ripoti chini ya azimio hilo limefikia mwisho, na kwamba hatua yoyote mpya katika mwelekeo huo haina uhalali wa kisheria.
-
Katika mazungumzo ya simu kati ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Pakistan:
Araghchi alisema: “Azimio namba 2231 la Baraza la Usalama linapaswa kuchukuliwa kuwa limekamilika na kuhitimishwa kwa wakati uliopangwa.”
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, huku akishukuru msimamo wa uwajibikaji wa Pakistan katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kupinga matumizi mabaya ya nchi tatu za Ulaya, alisisitiza kwamba Azimio namba 2231 lazima, kwa mujibu wa masharti yake na maandiko ya makubaliano ya nyuklia (JCPOA), lichukuliwe kuwa limekamilika katika muda uliopangwa, yaani tarehe 26 Mehr 1404 (18 Oktoba 2025).
-
Hamas: Kuweka veto kwa Azimio la Gaza kunaonesha ushirikiano wa Marekani katika uhalifu wa Israel
Harakati ya Kiislamu ya Mapambano ya Palestina, Hamas, siku ya Ijumaa ilitangaza kuwa kura ya turufu (veto) ya Marekani dhidi ya azimio kuhusu Gaza ni uthibitisho wa wazi na kamili wa ushirikiano wake katika uhalifu wa Israel dhidi ya watu wa Palestina walioko Ukanda wa Gaza. Hamas imesema kuwa hatua hiyo inaonesha kuwa Marekani inasaidia moja kwa moja mashambulizi, mauaji na uharibifu unaofanywa na Israel dhidi ya raia wasio na hatia, na siyo tena mpatanishi wa haki katika mgogoro huo. Vilevile, harakati hiyo imeitaka jumuiya ya kimataifa kusimama imara dhidi ya upendeleo huu na kuchukua hatua za dharura kuwalinda Wapalestina na kukomesha uvamizi wa Israel.
-
Upigaji kura wa leo katika Baraza la Usalama kuhusu kurejesha vikwazo dhidi ya Iran
Uanzishaji wa ‘mfumo wa kichocheo’ (Snapback mechanism / Triger Machanism) na Ulaya umeiweka Baraza la Usalama katika hali nyeti; ambapo kupinga azimio jipya kunamaanisha kurejea kwa vikwazo vyote dhidi ya Iran.
-
Chuo Kikuu cha Campinas, Brazil, Chataka Kukomeshwa kwa “Mauaji ya Kimbari Gaza”
Baraza Kuu la Chuo Kikuu cha Jimbo la Campinas (Consu – Unicamp) katika kikao chake cha Jumanne, Agosti 5, 2025, limepitisha azimio linalotaka kukomeshwa kwa kile walichokiita “mauaji ya kimbari Gaza” na kulitaka Serikali ya Brazil kusitisha uhusiano wake wa kibiashara na kijeshi na Israel.
-
Msimamo Mkali wa Hizbullah Dhidi ya Jaribio la Kuvunjwa kwa Silaha za Muqawama: Azimio Jipya la Serikali ya Nawaf Salam ni Tishio kwa Uhuru wa Lebanon
Chama cha Hizbullah kimetoa tamko kali kupinga uamuzi mpya wa serikali inayoongozwa na Nawaf Salam, ambao wanauona kama hatua ya hatari ya kudhoofisha muqawama (mapambano ya ukombozi) na kukabidhi usalama wa Lebanon kwa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel. Katika taarifa hiyo, Hizbullah imesisitiza kuwa itakabiliana na uamuzi huu kwa msimamo thabiti kama hatua isiyokubalika kabisa, huku ikisisitiza umuhimu wa kulinda silaha za kujihami na kuimarisha jeshi la taifa kwa ajili ya kutetea ardhi na uhuru wa Lebanon. Lebanon Bado Chini ya Vitisho vya Israel na Marekani
-
Radiamali ya Wapalestina kuhusu Kura ya Veto juu ya Azimio la Baraza la Usalama: Hatua ya Marekani ni Kutoa Uhalali wa Mauaji ya Kimbari huko Gaza
Ofisi ya Habari ya Serikali ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imelaani vikali kura ya veto iliyowekwa na Marekani dhidi ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kuitaja kama ishara ya wazi ya uungaji mkono wa Washington kwa uhalifu unaotekelezwa na utawala wa Kizayuni. Taasisi hiyo imesisitiza kuwa hatua hiyo itaongeza mgogoro wa kibinadamu huko Gaza na kusababisha kuongezeka kwa mauaji ya raia wasio na hatia. Imeyataka jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za haraka na madhubuti ili kuokoa maisha ya watu wasiokuwa na hatia katika eneo hilo.