Kwa mujibu wa ripoti na vyombo vya habari vya kimataifa, Rais wa Marekani Donald Trump amejibu kwa ukali taarifa zilizoibuliwa kuhusu vipengele vinavyodaiwa kuvuja vya makubaliano yanayoweza kufikiwa kati ya Marekani na Iran, akisisitiza kuwa madai hayo hayana uhusiano na makubaliano yoyote rasmi yaliyoandikwa katika mazungumzo ya kidiplomasia.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa vikosi vya nchi hiyo vinafanya operesheni za kujihami kwa mujibu wa sheria za kimataifa na kwamba malengo yaliyoshindikana kufikiwa kwa vikwazo na vita hayawezi kupatikana kwa kuongeza mashinikizo ya kijeshi.
Iran haitakoma kurutubisha urani; ni haki yake kama taifa huru, shughuli zote zikiwa salama na zikifuatiliwa na IAEA, na mazungumzo na Marekani yanaendelea bila kujadiliwa kwenye vyombo vya habari.