Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Ibn Tv Africa katika ripoti yake juu ya tukio muhimu la Shirika la Habari Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- lililojiri huko Accra, Ghana imesema: Katika hafla maalumu iliyojaa hadhira ya watu kutoka nyanja mbalimbali za kitamaduni, kidini na waandishi wa habari, ofisi ya kanda ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- kwa ajili ya Afrika Magharibi imezinduliwa rasmi mjini Accra, Mji Mkuu wa Ghana.
Ofisi hiyo mpya inatarajiwa kuwa kituo muhimu cha usambazaji wa habari kwa mataifa ya Afrika Magharibi, ikilenga kuimarisha upashanaji wa taarifa na maadili ya kiroho, utu, na haki kupitia mtazamo wa Kiislamu unaotegemea mafundisho ya AhlulBayt (as).
Shirika la Habari la ABNA, ambalo kwa sasa linafanya kazi katika lugha 27, linajihusisha na kusambaza habari za kitamaduni na kidini kwa kiwango cha kimataifa. Miongoni mwa lugha zinazotumika ni pamoja na Kiingereza, Kifaransa, Kihausa, Kiswahili, Kiarabu, Kihispania, na Kireno.
Akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi, Ayatollah Reza Ramazani, Katibu Mkuu wa Baraza la Dunia la AhlulBayt (as), alieleza umuhimu wa maadili ya juu katika uandishi wa habari. Alisema:
"Mtazamo wa kimantiki, wa kiroho, wa utu, na unaozingatia haki lazima utawale utangazaji wa habari wa ABNA."
Hafla hiyo imepokelewa kwa furaha na matumaini makubwa na viongozi wa jamii, wanahabari, na waumini, kama hatua chanya kuelekea kuimarisha mawasiliano ya kiutamaduni na kidini katika bara la Afrika.
Your Comment