21 Juni 2025 - 13:05
Source: IQNA
Qari maarufu wa Misri, Sheikh Taruti, afungamana na Iran katika kukabiliana na Israel

Qari mashuhuri wa Misri, Sheikh Abdul Fattah Taruti, ametangaza kufungamana na watu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel.

Katika ujumbe alioutuma kwa Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa (IQNA), Sheikh Abdul Fattah Taruti amebainisha mshikamano wake na taifa adhimu la Iran wakati huu wa kukabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel ambao unaendeleza mashambulizi ya kichokozi dhidi ya Iran.

Sheikh Taruti katika ujumbe wake ameomba dua ya ushindi kutoka kwa Allah kwa taifa la Iran kupitia Baraka za Qur’ani Tukufu. Akilihutubu taifa la Iran amesema: “Wamisri pamoja na viongozi wao wako pamoja nanyi, wanawaunga mkono yote ambayo mnafanya dhidi ya adui Mzayuni aliyeanzisha hujuma.”

Sheikh Taruti aidha ametangaza mshikamano na  watu wa Iran katika mapambano yao dhidi ya utawala ghasibu wa Israel kwa kusoma aya za Sura an-Nasr kama ilivyo katika klipu hii hapa chini.

342/

Your Comment

You are replying to: .
captcha