Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Baada ya Programu ya kusoma Qur’an, ambapo waumini wakiongozwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, ilifuatia neno la shukrani kutoka Kwa Kiongozi Muadhamu kwa wasomaji wa Qur’an ambapo aliwatakia kila mema, Baraka na neema tele katika Usomaji wa Qur'an Tukufu, na alisema:
"Ilifanyika vizuri sana, tulifaidika sana. Insha’Allah kila wakati wawe na Qur’ani karibu na mioyo yao, na kwamba kila siku msitu mdogo wa Qur’ani ukuwe zaidi na zaidi."
Kiongozi Mkuu aliendelea kusisitiza umuhimu wa Qur’ani katika maisha ya kila siku ya Waislamu, akihimiza kwamba usomaji na tafsiri yake iwe sehemu ya maisha ya kiroho, ikisaidia kuimarisha uhusiano na Mwenyezi Mungu na kuendeleza thawabu za kiroho.
Ramadhan, mwezi wa Qur’ani Tukufu, unatoa fursa ya pekee kwa Waislamu kusoma, kuelewa, na kutekeleza mafundisho yake, huku kila sala, doa, na usomaji ukipandisha thawabu na kumkaribia Mtukufu.
Your Comment