19 Februari 2026 - 23:24
Jarida la The Economist; limetumia kichwa cha Habari Kikisema: “Hatima ya Kennedy inamsubiri Trump!"

Jarida la The Economist limetoa onyo la kisiasa likirejelea hatima ya John F. Kennedy, likidokeza kuwa mazingira ya mvutano na migawanyiko mikali yanaweza kuongeza hatari za kiusalama kwa Donald Trump.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Jarida la The Economist limetoa tafadhali kwa kutumia kichwa cha Habari kikisema: “Hatima ya Kennedy inamsubiri Trump!” - kauli inayorejelea tukio la kuuawa kwa John F. Kennedy mwaka 1963 huko Dallas.

Kwa kutumia kauli hii, jarida hilo linaashiria mazingira ya mvutano mkubwa wa kisiasa na hatari za usalama zinazoweza kumkabili Donald Trump, hasa katika kipindi cha kampeni na migawanyiko mikali ya kisiasa nchini Marekani na migogoro yake anayoiibua nje ya Marekani.

Hata hivyo, usemi huo mara nyingi hutumika kama lugha ya kisiasa au tahadhari ya kiishara (metaphor), si utabiri wa tukio mahsusi, bali kuonyesha kiwango cha hatari au mivutano inayomzunguka mwanasiasa huyo.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha