Jeshi la Israel limefanya mashambulizi ya anga mashariki mwa Khan Yunis na kuua na kuwajeruhi makumi ya raia. Vikosi vya uokoaji viliopoa miili ya mashahidi na kuwahamisha waliojeruhiwa, huku hospitali zikithibitisha vifo 28, wakiwemo watoto 17.
Baraza la Mkoa wa Najaf Al-Ashraf limetangaza likizo ya wiki moja kwa ofisi zote za serikali katika mkoa huo, ili kuwezesha ushiriki wa wananchi katika maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s) na kutoa huduma bora kwa maelfu ya mahujaji wanaoelekea Najaf Ashraf.