20 Novemba 2025 - 20:40
Jeshi la Israel wafanya mashambulizi mapya Gaza baada ya siku ya mauaji makubwa

Jeshi la Israel limefanya mashambulizi ya anga mashariki mwa Khan Yunis na kuua na kuwajeruhi makumi ya raia. Vikosi vya uokoaji viliopoa miili ya mashahidi na kuwahamisha waliojeruhiwa, huku hospitali zikithibitisha vifo 28, wakiwemo watoto 17.

Shirika Ia Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Asubuhi ya Alhamisi, jeshi la uvamizi la Israel lilifanya mashambulizi kadhaa ya anga mashariki mwa Khan Yunis katika eneo la kusini mwa Gaza. Vikosi vya ulinzi wa raia vilipata miili ya mashahidi watatu na kuwaokoa watu 15 waliojeruhiwa kutoka eneo hilo, kufuatia siku ya maafa ambayo watu 28 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Kwa mujibu wa mwandishi wa Kituo cha Taarifa cha Palestina (PIC), jeshi la Israel lilizindua mashambulizi kadhaa ya anga mapema asubuhi mashariki mwa Khan Yunis, yakifuatana na mashambulizi makali ya mizinga.

Wakati huohuo, mamlaka za ulinzi wa raia zilikithibitisha kuwa vikosi vyao viliopoa miili ya mashahidi watatu na kuwahamisha watu 15 wa familia za Abu Sabt na Sahmoud baada ya shambulio la Israel kulenga nyumba katika eneo la Bani Suheila mashariki mwa Khan Yunis.

Ulinzi wa raia pia ulisema kuwa timu zake ziliweza kumuokoa raia aliyejeruhiwa katika eneo la Johor ad-Dik, kusini mashariki mwa Jiji la Gaza, baada ya uratibu na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA).

Mnamo Jumatano, vyanzo vya kitabibu katika hospitali za Gaza viliripoti kuwa raia 28, wakiwemo watoto 17 na mwanamke mmoja, waliuawa huku wengine 77 wakijeruhiwa katika mashambulizi ya Israel dhidi ya Jiji la Gaza na Khan Yunis, jambo ambalo ni ukiukaji wa wazi wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyopaswa kuanza tarehe 10 Oktoba.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha