mauaji
-
Javier Bardem na Wasanii wa Hollywood Walaani Mauaji ya Kimbari ya Israel Katika ukanda wa Gaza - Wakiwa katika Hafla ya Tuzo za Emmy 2025
Javier Bardem, mwigizaji mashuhuri kutoka Hispania, katika hafla ya Tuzo za Emmy 2025 huko Los Angeles, alivutia hisia za hadhira kwa kuvaa kofia ya Kipalestina (kufiya) na kutamka kwa uwazi: "Nipo hapa kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza. Uhuru kwa Palestina!" Alieleza msimamo wake wa wazi na wa moja kwa moja dhidi ya ukatili wa Israel, na aliungwa mkono na wengi waliokuwepo ukumbini. Aidha, Bardem alitangaza kuwa anaunga mkono kampeni ya kususia kampuni na taasisi zinazoshirikiana na utawala wa Kizayuni (Israel), na akasambaza ujumbe wake wa mshikamano na Palestina kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Maana ya hatua yake: Kauli na kitendo cha Javier Bardem kinaashiria mshikamano wa wasanii kimataifa na watu wa Palestina, hasa katika nyakati ambapo jukwaa la burudani linaangaliwa na watu wengi duniani. Uvaaji wa chafia na kauli ya wazi ni ishara ya kuhamasisha umma wa kimataifa kushiriki katika harakati za kuunga mkono Palestina.
-
Mkusanyiko wa watu wa Venezuela katika kuunga mkono malengo ya Palestina na kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza
Katika jimbo la Vargas, Venezuela, vikundi na mashirika ya kijamii, kwa msaada wa "Jukwaa la Mshikamano na Malengo ya Palestina", siku ya Jumamosi tarehe 13 Septemba 2025, walikusanyika pamoja ili: Kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza, Kuonesha upinzani wao dhidi ya sera na vitisho vya serikali ya Marekani dhidi ya nchi yao, Na kusisitiza juu ya haki ya Venezuela ya kujitawala kama taifa.
-
Idadi ya Mashahidi wa Gaza yafikia 64,803
Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa jumla ya mashahidi katika eneo hilo imefikia watu 64,803.
-
Rais wa Dar al-Iftaa ya Iraq asema:
“Ndio kwa Umoja wa Waislamu, ‘Hapana’ kwa Ubeberu wa Dunia”
Sheikh al-Sumayda‘i katika ufunguzi wa Mkutano wa Umoja alisema: "Lazima tuseme 'Ndio' kwa umoja wa Waislamu na, kwa kukataa ubeberu wa kimataifa, tuseme 'Hapana' kwa Magharibi na mabeberu."
-
Chama cha Kimataifa cha Utafiti wa Mauaji ya Kimbari: Israel Imetekeleza Mauaji ya Kimbari Gaza
Rais wa chama kikubwa zaidi duniani cha wataalamu wa masuala ya mauaji ya kimbari (IAGS) ametangaza kuwa taasisi hiyo imepitisha azimio linalothibitisha kuwa vitendo vya Israel katika Ukanda wa Gaza vinaendana na vigezo vya kisheria vya mauaji ya kimbari.
-
Jumuiya ya Al-Wefaq: Mkutano wa Waziri Mkuu wa Bahrain na Balozi wa Israeli ni “Dhalili ya Kuanguka kwa Diplomasia”
Jumuiya ya Al-Wefaq imeelezea mkutano wa Waziri Mkuu wa Bahrain na balozi wa utawala wa Kizayuni kama ishara ya kushindwa kwa diplomasia na kuendelea kwa sera ya kawaida za kawaida bila kuzingatia vipengele vya kibinadamu na kidini, na kuwatuhumu viongozi wa Bahrain kushiriki kwa kimyakimya katika “uchumi wa mauaji ya kimbari.”
-
Chanzo: Tovuti Rasmi ya Ofisi ya Ayatollah Makarim Shirazi | Je, Sheria ya Mtume (s.a.w.w) Inaruhusu Kuuawa kwa Imam Hussein (a.s)?
Kwa mujibu wa Aya ya "Tathira" (Qur’an, Ahzab: 33), Ahlul-Bayt (a.s), akiwemo Imam Hussein(as), wamesafishwa (wametakaswa) na Mwenyezi Mungu dhidi ya dhambi. Hivyo, haiwezekani Imam kuwa chanzo cha fitina au kuvunja umoja.
-
Wananchi wa Yemen wanalenga (wanashambulia) maeneo mbalimbali ya Wazayuni kujibu jinai zinazoendelea kufanywa na Israel
Vikosi vya jeshi la Yemen vimeanzisha operesheni mpya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya utawala wa Israel, hatua ambayo kwa mujibu wa duru za Yemen, ilifanyika kujibu mauaji ya raia huko Gaza.
-
A'shura-Tanzania | Kuelimika Juu ya Tukio la A'shura na Tukio lolote la Historia ya Kiislam ni kusimamia Ukweli Halisi na Haki ilivyo Katika Historia
Tunasoma Matukio ya Historia ya Kiislamu ili Kuelimika na baada ya Kuelimika Tunasimama katika Msingi wa Haki na kusema ukweli Halisi wa Kihistoria ulivyo andikwa katika Vyanzo Sahihi vya Shia na Sunni.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ulimwengu ya Ukaribu baina ya Madhehebu za Kiislamu: "Uhalifu wa Israel ni Jeraha kwenye Mwili wa Umma wa Kiislamu"
Hojjatul Islam Wal-Muslimeen Dakta Hamid Shahriari, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ulimwengu ya Ukaribu baina ya Madhehebu za Kiislamu ameandika katika ujumbe wake kwenye Twitter yake kuwa: "Uhalifu wa Israel sio tu kuishambulia Iran, bali pia ni jeraha kwenye mwili wa Umma wa Kiislamu."
-
Mauaji ya Mwanazuoni wa Kishia katika jimbo la Badakhshan nchini Afghanistan
Hojjat al-Islam wal- Muslimin, Sayyid Kazem Amiri, Profesa wa Seminari ya Imam Sadiq (AS) ameuawa katika mji wa Kashem, Mkoa wa Badakhshan, Afghanistan.
-
Tamko la Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) kuhusu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) imesisitiza katika tamko lake kwamba: kuanzisha vita dhidi ya Iran ya Kiislamu ni sawa na kuvamia harem (makao matakatifu) ya Ahlul-Bayt (a.s). Katika hali hii, wanaharakati wote wa haki duniani, hasa mashirika na jumuiya zilizo chini ya mwavuli wa Ahlul-Bayt na wale wanaohusishwa na Jumuiya hii, wanaweza sasa kwa sauti kubwa kuliko wakati wowote kusema wazi kuwa utawala wa Kizayuni ni wa kigaidi na mvamizi. Aidha, taifa la Iran, likiwa limeungana zaidi na thabiti kuliko wakati wowote, litatoa jibu kali na la wazi kwa utawala huu wa kihalifu na muuaji wa watoto.
-
Idadi ya waliouawa Gaza imefikia watu 54,880 | Hali ni mbaya sana na watu wengi wanahitaji msaada wa kibinadamu
Hali ya Gaza inaendelea kuwa mbaya kutokana na mashambulizi ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni. Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa ndani ya saa 24 zilizopita watu 108 wamepoteza maisha na wengine 393 wamejeruhiwa. Jumla ya waliofariki tangu kuanza kwa mashambulizi haya imezidi kufikia watu 54,000. Hali hii inahitaji mshikamano wa kimataifa ili kusitisha ukatili huu na kuanzisha mazungumzo ya amani.
-
Ayatollah Ramezani: "Viongozi wa Dini wanapaswa kuwa waongozaji katika kufanikisha amani yenye haki"
Mkutano wa kihistoria wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ahlul Bayt (a.s) na Askofu Mkuu wa Kanisa la Ivory Coast
Katika ziara ya Ayatollah Reza Ramezani, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ahlul Bayt (a.s) nchini Ivory Coast, alikutana kwa kifamilia na Kardinali Ignace Dogbo Assi, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini humo na mwakilishi wa Vatican. Katika mazungumzo hayo, pande zote mbili zilisisitiza umuhimu wa mazungumzo ya kidini, kuunga mkono heshima ya utu wa binadamu, na juhudi za kufanikisha amani ya kudumu duniani.
-
Mwakilishi wa Palestina katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa: "Fanikisha kuwasukuma Waisraeli kusitisha mauaji ya kimbari yanayoendelea"
Mwakilishi wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa amemshitaki utawala wa Kizayuni wa Israel kwa ukiukaji wa sheria za kimataifa na hukumu za Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICC), na kuhimiza hatua madhubuti kutoka kwa nchi za dunia ili kuzuia uhalifu unaoendelea wa utawala huo katika Ukanda wa Gaza. Ametoa msisitizo kuwa mashambulizi yanayofanywa mara kwa mara na Israel dhidi ya raia wasio na hatia na kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia, ni hali inayotakiwa kupokelewa kwa uzito mkubwa na jamii ya kimataifa.
-
Huthi: Ziara ya Donald Trump katika Nchi za Kiarabu Ilikuwa kwa Ajili ya Kudai Hongo
Mwanachama wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Mohammed Ali al-Houthi, amesema kuwa baadhi ya nchi za Kiarabu zimeathiriwa na udhaifu wa kisaikolojia na shida ya kushindwa. Aliongeza kuwa nchi hizi haziwezi hata kukata uhusiano wa kidiplomasia na Israeli, jambo ambalo linaonyesha upungufu wa msimamo na ushupavu katika kushikilia mikao ya kisiasa.
-
Jeshi la Israel linapanga njama ya kuteka 50% ya Ukanda wa Gaza
Jeshi la Israel linapanga kudhibiti asilimia 50 ya Ukanda wa Gaza ikiwa kutakuwa hakuna maendeleo katika mazungumzo ya pande mbili.
-
Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria yalaani Serikali kwa mauaji ya Waandamanaji 26 wanaounga mkono Palestina, na kuwaweka kizuizini 274
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, matukio kadhaa ya amani ya kidini yaliyoandaliwa na Harakati ya Kiislamu ya Nigeria chini ya uongozi wa Sheikh Zakzaky, likiwemo Kongamano la Mwaka la Mauaji ya Zaria ya mwaka 2015 na programu ya Nisfu / Nusu Sha’ban kwa ajili ya kuadhimisha Maulid ya Imam Mahdi (a.t.f.s), yaliripotiwa kuvurugwa na vikosi vya usalama.
-
Hatua mpya katika kuhalalisha uhusiano wa kawaida; Mkutano kati ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati (UAE ) na utawala haram wa Kizayuni
Waziri wa Mambo ya Nje wa UAE Abdullah Bin Zayed amejadili uhusiano wa pande mbili katika mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kizayuni Gideon Sa'er huko Abu Dhabi. Katika kikao hicho amesisitiza juhudi za kidiplomasia za kufikia usitishaji vita huko Ghaza, lakini mkutano huu ulifanyika katika hali ambayo utawala wa Kizayuni unaendelea kuua na kufanya mauaji ya kimbari huko Ghaza.
-
Kuuawa Shahidi na Kujeruhiwa kwa Wapalestina 373 ndani ya masaa 24
Wizara ya Afya ya Gaza imetangaza kuuawa Shahidi na kujeruhiwa Wapalestina 373 katika muda wa saa 24 zilizopita na kuongezeka kwa idadi ya Mashahidi wa mauaji ya kimbari na kufikia zaidi ya watu 50,600.
-
Shambulio baya la jeshi la Kizayuni kwenye Kliniki (Zahanati) ya Umoja wa Mataifa Kaskazini mwa Gaza
Shambulio la Wazayuni katika Zahanati moja katika Ukanda wa Gaza limepelekea kuuawa Shahidi watu kadhaa wakiwemo watoto.
-
Ilitajwa katika Salamu ya Eid al-Fitr:
Kiongozi wa Ansarullah: Watu wa Yemen wanashikamana na kadhia ya Palestina
Akitoa salamu za pongezi za Eid al-Fitr, Sayyid Abdul Malik al-Houthi alisema: "Watu wa Gaza hawakufunga tu Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, bali pia walipata heshima ya Jihadi na Upinzani (Muqawamah) dhidi ya wavamizi."
-
Kulaani Ukandamizaji na Mauaji ya watu wa Nigeria Katika Siku ya Al-Quds | Moto wa Mwamko wa Kiislamu Hautazimika
Baraza la Uratibu wa Tabligh za Kiislamu, limelaani ukandamizaji wa Maandamano ya Siku ya Quds Duniani nchini Nigeria, na limetangaza kuwa: Jinai hizo za kipofu zitazidisha azma ya Mataifa ya Kiislamu kukabiliana ipasavyo na mfumo wa ukoloni na uistikbari.
-
Mashambulizi ya anga ya Marekani nchini Yemen yameingia wiki ya pili / Mashambulio makubwa ya mabomu katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hodeidah
Mji wa Hodeidah ulioko Magharibi mwa Yemen umelengwa na mashambulizi makubwa ya mabomu ya jeshi la Marekani.
-
Wapalestina 130 Wameuawa Shahidi Katika Saa 48 Zilizopita
Katika saa 48 zilizopita, Mashahidi 130 na Majeruhi 263 wamehamishiwa katika Hospitali za Ukanda wa Gaza.
-
Wakimbizi wapya 13,000 wa Syria wamekimbilia Lebanon / wakikimbia uhalifu wa Al-Julani kwenye Pwani ya Syria
Takriban wakimbizi wapya elfu 13 wa Syria wameingia katika vijiji na miji 23 Kaskazini mwa Lebanon.
-
Vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza vimeanza tena| Wapalestina 131 wameuawa Shahidi katika mashambulizi ya mabomu ya ndege za Israel
Utawala wa Kizayuni umeshambulia kwa mabomu maeneo mbalimbali ya makazi ya watu katika Ukanda wa Ghaza
-
Radiamali ya Seneta RajA Nasser kwa mauaji ya Mwanazuoni wa Pakistan
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan amelaani mauaji ya Mufti Munir Shakir, Mwanazuoni wa Kisunni wa Pakistan, na kuyataja kuwa ni hasara isiyoweza kufidiwa.