palestina
-
Taarifa kutoka Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kuhusu Wimbi la 17 la Mashambulizi Mchanganyiko dhidi ya Utawala wa Kizayuni
Vituo hivi vimekuwa kitovu cha uovu dhidi ya wadhulumiwa wa Gaza, Lebanon, Yemen, na pia katika vita vilivyowekwa kwa uchokozi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran tangu Kimbunga cha Al-Aqsa kilipoanza.
-
Kiongozi cha Ansarullah Yemen:
"Jinai dhidi ya Iran hata bada ya kusisitiza kuwa haina haja ya silaha za Nyuklia ni kwa sababu ya misimamo imara Iran juu ya kadhia ya Palestina"
Wamagharibi hatwaki kuona Iran ikiwa ni nchi huru, na hii ni kutokana na msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kuwatetea wananchi wa Palestina na kukataa udhalimu wa uvamizi wa Kizayuni kwa ardhi za Taifa la Palestina.
-
Waisraeli 24 wauawa na 592 kujeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya Iran katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu
Ofisi ya habari ya Israel imeripoti kuwa, tangu kuanza mashambulizi ya makombora mazito ya Jamhuri ya Kiislamu ndani ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu, Wazayuni 24 wameuawa na wengine 592 wamejeruhiwa.
-
Wimbi kali la Mashambulizi ya Makombora ya Iran linaendelea katika awamu ya 3 ya Ahadi ya Kweli 3 /Makazi ya Netanyahu na maeneo kadhaa ya kistratijia
Ikinukuu vyanzo vyake vya kijeshi, Redio ya Jeshi la Israel ilithibitisha kurushwa zaidi ya Makombora 50 ya Balistiki kutoka ardhi ya Iran, na ving'ora vya kengele ya hali ya hatari vilisikika katika maeneo yote yanayokaliwa kwa mabavu ya Palestina.
-
Hamas: Dhana ya Netanyahu ya "ushindi kamili" ni ndoto tu
Harakati ya Hamas imesisitiza kuwa upinzani dhidi ya mauaji ya kimbari dhidi ya raia umeanzisha vita vya kuvunja nguvu za adui, ambapo kila siku wanatumia mbinu mpya za uwanjani kumshangaza adui.
-
Idadi ya waliouawa Gaza imefikia watu 54,880 | Hali ni mbaya sana na watu wengi wanahitaji msaada wa kibinadamu
Hali ya Gaza inaendelea kuwa mbaya kutokana na mashambulizi ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni. Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa ndani ya saa 24 zilizopita watu 108 wamepoteza maisha na wengine 393 wamejeruhiwa. Jumla ya waliofariki tangu kuanza kwa mashambulizi haya imezidi kufikia watu 54,000. Hali hii inahitaji mshikamano wa kimataifa ili kusitisha ukatili huu na kuanzisha mazungumzo ya amani.
-
Mwakilishi wa Palestina katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa: "Fanikisha kuwasukuma Waisraeli kusitisha mauaji ya kimbari yanayoendelea"
Mwakilishi wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa amemshitaki utawala wa Kizayuni wa Israel kwa ukiukaji wa sheria za kimataifa na hukumu za Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICC), na kuhimiza hatua madhubuti kutoka kwa nchi za dunia ili kuzuia uhalifu unaoendelea wa utawala huo katika Ukanda wa Gaza. Ametoa msisitizo kuwa mashambulizi yanayofanywa mara kwa mara na Israel dhidi ya raia wasio na hatia na kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia, ni hali inayotakiwa kupokelewa kwa uzito mkubwa na jamii ya kimataifa.
-
Upanuzi wa kampeni ya kususia bidhaa za Israel: Kutoka New Delhi hadi maeneo mbalimbali ya India
Waandaji wa kampeni hii wamesema kuwa lengo ni kuonyesha upinzani wao dhidi ya uhalifu unaoendelea wa utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina na kushinikiza kwamba baadhi ya chapa za kimataifa zinashiriki kifedha kwa ajili ya kuunga mkono utawala huu.
-
Ansarullah: Operesheni za Kijeshi za Yemen Zitaendelea Kuongezeka Taratibu
Mwanachama wa Ofisi ya Kisiasa ya Ansarullah Yemen amesisitiza kuwa ikiwa uvamizi wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza utaendelea, basi operesheni za kijeshi za Yemen zitaendelea kuongezeka taratibu.
-
"Vita vya Gaza vimesababisha Wapalestina 1,500 kupoteza uwezo wa kuona"
Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza leo Jumapili kuwa, kutokana na vita na kuzidi kwa mzingiro unaoendelea wa jeshi la utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza, Wapalestina 1,500 wamepoteza uwezo wao wa kuona.
-
Katika mkutano na maelfu ya wafanyakazi kutoka kote nchini:
Kiongozi wa Mapinduzi ametoa uungaji mkono kamili kwa jamii ya wafanyakazi / Fikira zisikengeushwe kutoka kwenye suala la Palestina
Ayatollah Khamenei pia alisisitiza kuwa, pamoja na kuendelea kwa jinai na mauaji ya kikatili dhidi ya watu wa Gaza na Palestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni kwa msaada wa Marekani na Uingereza, mataifa yanapaswa kusimama dhidi ya utawala wa Kizayuni na wafuasi wake, na wasiruhusu masuala yanayohusu Palestina kusahaulika.
-
Hasira za Wafuasi wa Uzayuni Kufuatia Matokeo ya Uchaguzi wa Canada / Mark Carney na Msimamo Wake wa Kizayuni Dhidi ya Palestina
Matokeo ya uchaguzi wa karibuni nchini Canada yamezua ghadhabu miongoni mwa wafuasi wa utawala wa Kizayuni, hasa baada ya ushindi wa Mark Carney, mwanasiasa ambaye anajulikana kwa msimamo wake wa kihafidhina zaidi kuhusu suala la Palestina. Mabadiliko haya katika mwelekeo wa siasa za Canada yamewafanya baadhi ya wafuasi mashuhuri wa Kizayuni kuonesha hali ya kukata tamaa, huku wakitoa ukosoaji mkali dhidi ya mazingira mapya ya kisiasa yanayoweza kuathiri uhusiano wa karibu wa Canada na Israel.Hofu kuu ya makundi hayo ni kwamba sera mpya zinaweza kupunguza uungaji mkono wa wazi kwa Israel, na kufungua nafasi kwa mijadala mikali zaidi kuhusu haki za Wapalestina katika siasa za ndani na nje ya Canada.
-
Onyo Kuhusu Mradi wa "Kuisahau Palestina" – Njama ya Kimataifa kwa Ushirikiano wa Viongozi wa Kiarabu
Kiongozi wa Harakati ya Kuamsha Ummah wa al-Mustafa: Kusahau Kadhia ya Palestina ni Njama Hatari na Usaliti Usiosameheka. Kiongozi wa Harakati ya Kuamsha Ummah wa Mustafa, katika hotuba yake ya hivi karibuni mjini Lahore, amekosoa vikali ukimya wa ulimwengu wa Kiislamu mbele ya uhalifu wa utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Palestina. Amesema kuwa kusahaulika kwa suala la Palestina ni njama hatari na usaliti usiosameheka, na akasisitiza kwamba ukimya huu – kuanzia vyombo vya habari hadi baadhi ya Serikali za Kiarabu – ni sehemu ya mradi wa kufuta kwa taratibu Palestina kutoka kwenye kumbukumbu ya Ummah wa Kiislamu.
-
Uturuki imefunga anga lake kwa ndege za Israel, ikiwa ni pamoja na ndege ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu
Uturuki imetangaza rasmi kuwa imefungia anga lake kwa ndege za Israel, ikiwa ni pamoja na ndege ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, na haitatoa ruhusa yoyote kwa safari yake kwenda Azerbaijan. Hatua hii imechukuliwa kutokana na sera za utawala wa Israel kuhusu Gaza, na Uturuki inaendelea kuunga mkono haki za watu wa Palestina.
-
Je, jinai ya Palestina ni kweli kuwa inaungwa mkono na Iran ya Kishia?!
Wakati picha za kutisha za mauaji ya halaiki huko Gaza zimeamsha dhamiri za wanadamu kote ulimwenguni, ukimya mzito katika baadhi ya jamii za Kiislamu, haswa kati ya duru za kidini, unatia shaka. Kwa nini baadhi ya watu wanauita Upinzani (Muqawamah) huu "wa Kidini" au "Kisiasa" na kuondoa uungaji mkono wao wakati Hamas, Hezbollah, au Iran inaposimama dhidi ya Israel?!, Je, (kupinga) dhulma na ukandamizaji kwa Wapalestina unahitaji idhini ya Madhehebu?
-
Usitishaji vita wa siku 70 huko Gaza; Je, Tel Aviv itakubali na kutii makubaliano hayo?
Mazungumzo kati ya Hamas na Mamlaka ya Misri Mjini Cairo yanaendelea kufanikisha usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza. Makubaliano hayo yanajumuisha kuachiliwa kwa idadi kadhaa ya wafungwa wa Israel na Palestina na iwapo yatakubaliwa, yanaweza kusaidia kuboresha hali ya kibinadamu katika eneo hilo. Walakini, Tel Aviv bado haijajibu vyema kwa makubaliano ya mwisho.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Ulamaa wa Pakistan: Mahali pa mwisho pa mradi wa "Israeli Kubwa" ni Makka na Madina
Mkuu wa Baraza la Ulamaa wa Pakistan alionya kwamba mradi wa "Israeli Kubwa" unatafuta udhibiti wa mwisho juu ya Madina na Makka.
-
Jeshi la Israel linapanga njama ya kuteka 50% ya Ukanda wa Gaza
Jeshi la Israel linapanga kudhibiti asilimia 50 ya Ukanda wa Gaza ikiwa kutakuwa hakuna maendeleo katika mazungumzo ya pande mbili.
-
Wito wa Maandamano kufuatia Mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni
Kufuatia mashambulio hayo ya kinyama ya utawala wa Kizayuni, Baraza la Uratibu wa Tabligh za Kiislamu limetoa taarifa likiwaalika Wananchi Watukufu wa Tehran kushiriki katika maandamano yatakayofanyika kesho katika Medani ya Palestina.
-
Katuni | Hakuna njia ya kutokea na kukimbia huko Gaza
Watoto wa Kipalestina wanatamani sana Msaada kutoka kwa Mashirika ya Kimataifa.
-
Mwenyekiti wa Bunge la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
Kila siku huko Gaza ni Apocalypse (Zama za Mwisho / Mwsiho wa Dunia) / Ukimya wa watawala wa Kiarabu unatia uchungu zaidi kuliko uhalifu (jinai)
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan amesema: "Tukio chungu zaidi si tukio la uhalifu unaofanyika dhidi ya Gaza, bali ni kile kimya kinachojiri katika Kasri za watawala wa Kiislamu na Kiarabu." Lugha zilizokuwa zikizungumza kutetea Uislamu sasa hivi zinalamba nyayo za madola ya kibeberu.
-
UNICEF: Maisha ya watoto milioni moja huko Gaza yako hatarini
Wakati huo huo hujuma zikiendelea na ugavi wa misaada kwa Gaza ukikatizwa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto lilionya kuhusu hali mbaya ya kibinadamu katika eneo hili na kutangaza kwamba maisha ya watoto wapatao milioni moja katika ukanda huu yako chini ya hatari na tishio kubwa.
-
Kuuawa Shahidi na Kujeruhiwa kwa Wapalestina 373 ndani ya masaa 24
Wizara ya Afya ya Gaza imetangaza kuuawa Shahidi na kujeruhiwa Wapalestina 373 katika muda wa saa 24 zilizopita na kuongezeka kwa idadi ya Mashahidi wa mauaji ya kimbari na kufikia zaidi ya watu 50,600.
-
Hassan Badir, Afisa wa Dawati la Palestina la Hezbollah ya Lebanon auawa Shahidi
Utawala wa Kizayuni ulilenga nyumba ya makazi na baadhi ya watu wa familia ya Hassan Badir pia walikuwa ndani ya nyumba hiyo wakati wa jinai hiyo ya Wazayuni.
-
Mmoja wa Maafisa wa Dawati la Palestina la Hezbollah ya Lebanon ameuawa Shahidi
Jana usiku utawala wa Kizayuni ulishambulia jengo la makazi kwa mashambulizi ya anga bila ya kutoa tahadhari ya awali.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Ikiwa Amerika itafanya jambo lolote ovu, litajibiwa vikali
Ayatollah Khamenei amesema kuhusu misimamo ya vitisho ya hivi karibuni ya Marekani: Kwanza, iwapo uovu utafanywa kutoka nje, jambo ambalo bila shaka halina uwezekano mkubwa, kwa hakika watajibiwa kwa kupigwa kwa pigo kali , na pili, ikiwa adui anafikiria kuzusha mpasuko (fitna) kwa ndani, kama ilivyokuwa katika baadhi ya miaka ya nyuma, Taifa litatoa jibu kali kwa waasi (wapenzi wa fitna) kama ilivyokuwa kwa miaka hiyo.
-
Ilitajwa katika Salamu ya Eid al-Fitr:
Kiongozi wa Ansarullah: Watu wa Yemen wanashikamana na kadhia ya Palestina
Akitoa salamu za pongezi za Eid al-Fitr, Sayyid Abdul Malik al-Houthi alisema: "Watu wa Gaza hawakufunga tu Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, bali pia walipata heshima ya Jihadi na Upinzani (Muqawamah) dhidi ya wavamizi."
-
Siku ya Quds Duniani:
Mojawapo ya sehemu ya malengo ya Siku ya Quds Duniani, ni kuienzi Amani ya Dunia nzima
Mojawapo ya sehemu ya malengo ya Siku ya Quds Duniani, ni kuienzi na kuidumisha Amani ya Dunia nzima. Waislamu waishi kwa Amani, Wakristo waishi kwa Amani, na hata Mayahudi waishi kwa Amani, na mtu yeyote asionewe na kudhulumiwa popote pale alipo Duniani.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Maandamano ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Maandamano yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Mwenyezi Mungu akipenda (Insha Allah), Matembezi (Maandamano) ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Matembezi bora zaidi, Matukufu na yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds.
-
Hazrat Ayatollah Javadi Amoli:
Siku ya Quds ni sehemu ya "Siku ya Kimataifa ya Uislamu"
Ayatollah Javadi Amoli, akiwaalika watu kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alisema: Ni wajibu wetu sote kushiriki katika Maandamano haya, kwanza, Na kila mmoja wetu kwa mujibu wa elimu tuliyo nayo, awe na nia ya Tawalli na Tabarri ya Kimungu, pili, na kujaribu kufayanya kuwa maandamano mapana zaidi, tatu, yaani tuyafanye maandamano haya kwa nia ya kuwa karibu na kuwaheshimu na kuwathamini Mashahidi wa njia hii, ili hatua hizi zote zithibitishwe na Dhati Takatifu ya Mwenyezi Mungu.