Taarifa
-
Walinzi wa Mapinduzi wa Iran Wawashukuru Wananchi wa Jordan na Kutangaza Kulenga Ndege za Marekani Katika Uwanja wa Ndege wa Aqaba
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran wamewashukuru wananchi na wanajeshi wa Jordan kwa taarifa walizodai zilisaidia katika mashambulizi dhidi ya vituo vya Marekani, huku wakitangaza kulenga ndege za kijeshi za Marekani katika Uwanja wa Ndege wa Aqaba.
-
IRGC Yathibitisha kushambulia kwa kushtukiza kituo cha uongozi wa operesheni za Marekani eneo la Al-Tanf nchini Syria
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limefanya shambulio la kushtukiza dhidi ya kituo cha uongozi wa operesheni maalumu kinachodaiwa kutumiwa na majeshi ya Marekani katika eneo la Al-Tanf nchini Syria, likisema hatua hiyo ni majibu ya mashambulizi yaliyosababisha vifo vya wanajeshi wa Iran.
-
IRGC Yatoa Taarifa ya Kuharibu Rada za Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain katika Operesheni "Nasr 2 | Ushindi 2"
limedai kuharibu rada za ulinzi wa anga, mfumo wa onyo la mapema na kituo cha udhibiti wa boti zisizo na rubani za Kikosi cha Tano cha Wanamaji wa Marekani nchini Bahrain.
-
Wizara ya Usalama ya Iran Yapongeza Mahudhurio Makubwa ya Umma wa Kiislamu Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi
Wizara ya Usalama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ya kupongeza ushiriki mkubwa wa wananchi, Marjaa wa dini, serikali na wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ikieleza kuwa tukio hilo limeonyesha umoja, uaminifu na mshikamano wa Umma wa Kiislamu.
-
Iran Yalaani Katika Baraza la IMO Mashambulizi ya Marekani Dhidi ya Miundombinu ya Bahari ya Nchi Hiyo
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani katika mkutano wa Baraza la Shirika la Kimataifa la Bahari (IMO) mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya bandari, maeneo ya pwani na miundombinu ya bahari ya Iran, ikiyataja kuwa ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na tishio kwa usalama wa raia na usafiri wa baharini.
-
Iran yasema vikwazo vya baharini vya Marekani vimeondolewa katika bandari zake
Iran yatangaza kuondolewa kwa vikwazo vya baharini vya Marekani katika bandari zake, hatua inayoweza kufungua ukurasa mpya wa usafirishaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.
-
Mbunge wa Hizbullah: Israel Itaondoka Kusini mwa Lebanon kwa Mujibu wa Makubaliano kati ya Marekani na Iran
Mbunge wa Hizbullah amesema Lebanon itakuwa sehemu ya makubaliano yoyote ya usitishaji vita, akisisitiza kuwa kuondoka kwa majeshi ya Israel kusini mwa Lebanon na dhamana za Marekani ni masharti muhimu ya utekelezaji wake.
-
Gharibabadi: Umoja wa Ardhi na Usalama wa Taifa la Iran Si Sehemu ya Propaganda za Kisiasa
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amesema Iran haitaruhusu mamlaka yake, umoja wa ardhi wala usalama wa taifa kuwa sehemu ya propaganda au mashinikizo ya kisiasa kutoka kwa Marekani na washirika wake.
-
Iran, China na Urusi katika Baraza la Magavana la IAEA: Rasimu ya Azimio dhidi ya Iran ni ya Kisiasa na Haina Tija
Iran, China na Urusi zimekosoa rasimu ya azimio dhidi ya Iran katika Baraza la Magavana la IAEA, zikisema ni ya kisiasa na inalenga kuongeza shinikizo badala ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, huku zikisisitiza kuwa hatua hizo zinaweza kuhatarisha diplomasia na utulivu wa nyuklia.
-
Mjadala Mkubwa Wazuka Mitandaoni Kuhusu Taarifa Zinazokinzana za Uwezo wa Kijeshi wa Iran
Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamehoji taarifa zinazokinzana kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran, baada ya baadhi ya vyombo vya habari kudai kuwa umedhoofika pakubwa huku matukio ya baadaye yakionyesha Iran ikiendelea na operesheni za kijeshi, hali iliyozua mjadala kuhusu ukweli wa taarifa hizo.
-
Iran Yaukosoa Mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Yasema Azimio 2231 Lilikoma Mwaka Jana
Ujumbe wa Iran katika Umoja wa Mataifa umeelezea kikao cha Baraza la Usalama kuhusu Iran kuwa ni “onyesho jingine la unafiki na viwango viwili,” ukisisitiza kuwa Azimio Na. 2231 la Baraza la Usalama lilimalizika rasmi Oktoba 18, 2025 na kwamba hakuna tena msingi wa kisheria wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran.
-
Iran Yaongeza Ulinzi wa Mlango wa Hormuz, Vikosi vya Makombora Vapewa Mamlaka ya Kujibu Vitisho Moja kwa Moja
Chanzo chenye taarifa za ndani kimesema Iran imeimarisha kwa kiwango kikubwa uwepo wa kijeshi katika Mlango wa Hormuz, ikirejesha shughuli katika vituo vyote vya makombora vya eneo hilo na kupeleka vifaa vipya vya ulinzi vilivyofanikiwa kudungua makumi ya droni.
-
Iran Yadungua Ndege ya Marekani Isiyo na Rubani Baada ya Kukiuka Anga ya Nchi Hiyo
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeripotiwa kudungua ndege ya Marekani isiyo na rubani aina ya MQ-1 Predator baada ya kuingia katika anga ya Iran, tukio lililotajwa kuwa ukiukaji wa makubaliano ya usitishaji mapigano.
-
Burkina Faso Yakanusha Taarifa za Machafuko; Serikali Yatetea Muswada wa Kudhibiti Maeneo ya Ibada
Serikali ya Burkina Faso imetetea hatua ya kumkamata mwanazuoni wa Kiislamu Dk. Mohamed Kindou kufuatia hotuba yake kuhusu muswada wa maeneo ya ibada, huku ikisisitiza kuwa hakuna uasi dhidi ya Rais Ibrahim Traoré na kwamba wananchi bado wanaunga mkono uongozi wake.
-
Kundi la udukuzi “Handala”: Taarifa nyeti za jeshi la Israel ziko mikononi mwetu
Kundi la udukuzi Hanzala limedai kuwa limepata taarifa nyeti za jeshi la Israel, likionya kuwa linafuatilia harakati zote na huenda likachapisha taarifa zaidi hivi karibuni.
-
Mwendesha Mashtaka wa Tehran afungua mashtaka dhidi ya wanasiasa wanaounga mkono mikondo hasimu
Mwendesha Mashtaka wa Tehran ametangaza mashtaka dhidi ya baadhi ya wanasiasa kwa tuhuma za kushirikiana na Marekani na utawala wa Kizayuni, ambapo watu 4 wamekamatwa kwa madai ya kuchochea vurugu na kudhoofisha usalama wa ndani.
-
Jumuiya ya Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s) Uturuki Yaionya Marekani: Imam Khamenei ni Mstari wetu Mwekundu
Jumuiya ya Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s) nchini Uturuki, katika tamko lake, imetangaza kuwa jaribio lolote la kumvunjia heshima au kumdhuru Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ni mstari mwekundu wa ulimwengu wa Kiislamu.
-
Mkuu wa Polisi wa Iran Awaarifu Bunge Kuhusu Juhudi za Kudumisha Amani na Utulivu Nchini
Katika taarifa yake amewaeleza wabunge hatua na juhudi zinazochukuliwa na vyombo vya usalama na utekelezaji wa sheria ili kuhakikisha amani, utulivu na usalama vinaendelea kudumishwa nchini.
-
Trump Atapanga Hatua Kuhusu Mafuta ya Venezuela Ijumaa
Trump Atatoa Uamuzi Kuhusu Mafuta ya Venezuela Ijumaa Akihudhuria Wakurugenzi wa Makampuni Makuu ya Mafuta. Taarifa zinaonyesha kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, atakutana Ijumaa na wakurugenzi wa makampuni makuu ya mafuta ili kufanya maamuzi kuhusu sekta ya mafuta ya Venezuela.
-
Habari za Hivi Punde | Iran Yakamata Meli Iliyokuwa Inasafirisha Lita Milioni 4 za Mafuta ya Magendo katika Ghuba ya Uajemi
Maafisa wa Iran wamesisitiza kuwa operesheni hiyo ni sehemu ya juhudi endelevu za kupambana na magendo ya rasilimali za taifa, kulinda uchumi wa nchi, na kudumisha usalama wa majini katika eneo la Ghuba ya Uajemi.
-
Mchambuzi wa Zamani wa CIA: Uwezo wa Kijeshi wa Iran Sasa Ni Imara Zaidi na Marekani Haiwezi Kamwe Kuilazimisha Iran Ijisalimishe
Johnson anaamini kuwa Iran sasa si tu haiko dhaifu, bali imejizatiti kama mchezaji mkuu katika masuala ya kieneo, na ina uwezo wa kushughulikia changamoto na shinikizo kutoka nje.
-
Jeshi la Israel wafanya mashambulizi mapya Gaza baada ya siku ya mauaji makubwa
Jeshi la Israel limefanya mashambulizi ya anga mashariki mwa Khan Yunis na kuua na kuwajeruhi makumi ya raia. Vikosi vya uokoaji viliopoa miili ya mashahidi na kuwahamisha waliojeruhiwa, huku hospitali zikithibitisha vifo 28, wakiwemo watoto 17.
-
Hizbullah: Ulegevu wa serikali ya Lebanon unaongeza ukatili wa Wazayuni
Hizbullah imesisitiza katika taarifa yake kwamba serikali ya Lebanon inapaswa kufahamu kuwa kila aina ya ulegevu, udhaifu au kujisalimisha mbele ya utawala wa Kizayuni kutawafanya waongeze ukatili na tamaa zao za kupindukia.
-
Irani Dhidi ya Magharibi: Kutoka Uzoefu wa Kihistoria Hadi Mapambano ya Kistaarabu ya Leo
Mkutano “Sisi na Magharibi katika Mitazamo na Fikra za Ayatullah Al-Udhma Sayyid Ali Khamenei” wafanyika Tehran.
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina: Mashambulizi ya wakazi wa maboma ni sehemu ya mpango wa mauaji ya kimbari na kuhamishwa kwa nguvu
Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina, kupitia taarifa yake, imelaani vikali mashambulizi ya walowezi wa Kizayuni dhidi ya raia wa Kipalestina na wanaharakati wa kigeni katika msimu wa kitaifa wa uvunaji wa zeituni katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.
-
Iran yashuku ujumbe wa Netanyahu kuhusu kutoshambulia tena
"Vikosi vya ulinzi vya Iran vipo katika hali ya tahadhari ya juu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa hila kutoka Israel, na hatuamini nia hizi".
-
Lebanon imekamata watu 32 kwa tuhuma za kushirikiana na Israel kama majaribio ya kijasusi
Maafisa wa Lebanon wameripoti kwamba angalau watu 32 wamekamatwa kwa tuhuma za kushirikiana na Mossad na kupeleka taarifa za kina kuhusu nafasi na harakati za Hezbollah kwenda Israel wakati wa vita vya hivi karibuni.
-
Magaidi 10, Wakiwemo Wanawake Wawili, Watekwa na Shirika la Taarifa za Kijajusi la Kijeshi la Iraq
Shirika la Taarifa za Kijeshi la Iraq leo limetangaza kuwa katika operesheni mbalimbali za kiusalama, limefanikiwa kuchukua watu 10 wa kigaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi, wakiwemo wanawake 2.
-
Ismail Baghaei – Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran:
Amesema kuwa taarifa ya Kundi la G7 kuhusu kurejesha vikwazo vya Baraza la Usalama dhidi ya Iran ni ya kinafiki na yenye upotoshaji.
Ismail Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amelaani na kulikemea tamko la Kundi la G7 kuhusu suala la nyuklia la Iran, akilitaja kuwa ni la kinafiki na kupotosha ukweli.
-
Wizara ya Ulinzi ya Iran: Hakuna Nguvu Yenye Haki ya Kuingilia Uwezo wa Makombora ya Iran
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Ulinzi, Brigedia Talaeinik alibainisha kuwa Marekani na washirika wake wanasisitiza mazungumzo kuhusu programu ya makombora na wanataka kupunguza umbali wa makombora ya Iran. Hata hivyo, alisema kuwa msingi wa uwezo wa makombora ya Iran ni kulinda usalama na maslahi ya kitaifa ya wananchi wake.