14 Septemba 2025 - 19:15
Uhamaji wa Waisraeli 11,000 Baada ya Vita na Iran | Walihama ili kukimbia Makombora ya Iran

Kwa Mujibu wa Taarifa, kurejea kikamilifu kwa wakimbizi hawa majumbani mwao kutachukua miaka kadhaa.

Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Shirika la Kitaifa la Hali za Dharura la utawala wa Kizayuni limetangaza kuwa zaidi ya wananchi 11,000 wa Israel wamelazimika kuyahama makazi yao kufuatia makombora ya Iran.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, sehemu kubwa ya waliokimbia bado wako chini ya mshtuko wa kisaikolojia uliosababishwa na mashambulizi hayo. Aidha, kupanda kwa bei ya upangishaji nyumba na malalamiko makubwa dhidi ya utendaji wa serikali ni miongoni mwa changamoto kuu zinazowakabili.

Shirika hilo limekadiria kuwa kurejea kikamilifu kwa wakimbizi hawa majumbani mwao kutachukua miaka kadhaa.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha