Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema: Tutajibu ongezeko la mvutano kwa ongezeko la mvutano. Kuanzia sasa, sambamba na kupiga marufuku kupita kwa meli za Israeli katika Bahari Nyekundu, kupita kwa meli za Marekani pia ni marufuku.
Mjumbe Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Ansarullah amesisitiza kuwa, Yemen haitaacha kuiunga mkono Palestina kwa gharama yoyote ile na akasema: Kila mtu anajua kuwa Yemen ni Mwaminifu katika kujibu hujuma ya adui, na Marekani inapaswa kusubiri jibu la Yemen.