Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Baraza la Mkoa wa Najaf Al_Ashraf limetoa taarifa rasmi leo hii Jumanne, likisema kuwa likizo ya Wiki Moja kwa ajili ya kuwakaribisha Mazuwwari itaanza siku ya Alhamisi, tarehe 16 Mfunguo Nne (Agosti), hadi tarehe 27 mwezi huo.
Hata hivyo, taasisi za usalama na huduma za msingi hazitahusishwa na likizo hiyo.
Hussein Al-Isawi, Mwenyekiti wa Baraza la Mkoa wa Najaf Ashraf, amesema kuwa:
"Uamuzi huu umechukuliwa ili kutoa nafasi kwa wakaazi wa Najaf kushiriki kikamilifu katika ibada za Arubaini na pia kuwezesha utoaji huduma kwa maelfu ya wageni wanaokuja kushiriki maombolezo ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s)."
Maadhimisho ya Arubaini hujumuisha mamilioni ya mahujaji kutoka Iraq na sehemu mbalimbali duniani, na Najaf Ashraf ni moja ya vituo vikuu vya maandalizi ya matembezi ya kuelekea Karbala.
Your Comment