Mwezi
-
Tunajifunza nini baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?
Aliyekuwa akifanya Ibada za Usiku ndani ya Ramadhani na mwendo wake ukabadilika na tabia zake kuwa nzuri ndani ya Ramadhan, basi aendelee kuwa na tabia nzuri hivyo hivyo hata baada ya Ramadhan. Na hii ni sehemu ya wito na funzo zuri toka kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).
-
Qur'an ni Msingi wa Maisha yetu, na ni Kitabu cha kweli, chenye kudumu milele
Muislamu mwenye kuhifadhi Qur'an Tukufu na mwenye Elimu juu ya Qur'an Tukufu, huyo atakuwa ni mwenye kuangaziwa na Nuru ya Qur'an kaburini mwake, na Mtume Muhammad (s.a.w.w) atakuwa Shahidi wake kesho Siku ya Kiyama.
-
Mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi nchini Iraq katika mazungumzo na Abna:
Kuhifadhi Utukufu wa Ramadhani na kuimarisha matumaini, ni sababu ya Nguvu na Ukaribu wa Kiislamu
Ayatollah Hosseini, Mwakilishi wa Kiongozi Muadhamu wa Iraq na mjumbe wa Baraza la Wataalamu wa Uongozi ameashiria taathira za funga kiutamaduni na kijamii na kusisitiza juu ya ulazima wa kuhifadhi utukufu wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika jamii.
-
Ramadhan ni Mwezi ambao dhambi zote zinaunguzwa (zinafutwa) ndani yake
Mja asikose wala asikate tamaa katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani, bali akithirishe kwa wingi kuomba sana maghfira na msamaha kwa Mwenyezi Mungu, kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, na anasamehe dhambi za aina yoyote ile (ispokuwa dhambi ya kumshirikisha).