Mwezi
-
Majlisi ya Maombolezo ya Muharram Yafanyika Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam
Majlisi ya maombolezo ya mwezi wa Muharram imefanyika katika Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam, Tanzania, ambapo mhadhiri alikuwa Sheikh Taqee Zacharia Athumani, akizungumzia sababu za kuhuishwa kwa kumbukumbu ya Karbala kila mwaka.
-
"Mtu kama mimi hawezi kumpa baia mtu kama yeye" – Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei alipofafanua somo Kubwa la Muharram
Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei alisema kuwa somo kubwa zaidi la Mwezi wa Muharram ni kujitolea kwa Imam Hussein (AS) kwa ajili ya kuilinda dini ya Uislamu, akisisitiza kuwa kila Muumini anapaswa kuwa tayari kujitoa kwa kila alicho nacho pale utetezi wa Uislamu unapohitajika.
-
Bendera ya Maombolezo ya Imam Hussain (AS) Yapandishwa katika Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh kuukaribisha Mwezi wa Muharram
Mamia ya Mazuwwari na wakazi wa mji wa Qom walishiriki hafla ya kupandisha Bendera Nyeusi ya maombolezo ya Imam Hussein (AS) juu ya Kuba la Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh (SA), kuashiria kuanza kwa Mwezi Mtukufu wa Muharram na kumbukumbu ya Mashahidi wa Karbala.
-
Serikali ya Iran Yatangaza Mali Zilizoachwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (r.a)
Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema uchunguzi wa mali za Ayatullah Sayyid Ali Khamenei (r.a.) umebaini kuwa aliacha mali chache sana, jambo linalotajwa kuakisi maisha yake ya ucha-Mungu na kujiepusha na anasa.
-
Mazungumzo yaendelea kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kunyang’anya silaha Gaza / Kikosi cha Indonesia chatarajiwa kuwasili mwezi Machi
Katika muktadha wa kunyang’anya silaha huko Gaza, mapendekezo mengi yamewasilishwa. Inabakia kuonekana iwapo Hamas na makundi ya muqawama watakubali kikamilifu suala hili. Hapo awali, mazungumzo yalihusu tu silaha nzito, lakini sasa yanajumuisha pia silaha za mtu binafsi.
-
Sehemu ya Tatu:
Khutba ya Mtume Mtukufu (s.a.w.w) katika kukaribia Mwezi wa Ramadhani - Sehemu ya Khutba ya Sha‘baniyyah
Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, dua za waumini hupokelewa haraka. Ni wakati wa kuomba kwa moyo safi na nia thabiti, hasa kuomba Mwenyezi Mungu atupatie neema ya kufunga Ramadhani na kusoma Qur’ani. Huu ni mwaliko wa kiroho wa kujijenga, kujisafisha na kuimarisha uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu.
-
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Woldan:
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kurekebisha mtindo wa maisha
Mkurugenzi Mkuu wa Tablighi za Kiislamu mkoa wa Fars ameeleza kuwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kujenga upya roho na kurekebisha mtindo wa maisha. Amesema kuwa Mwenyezi Mungu ameumba mfumo wa uwepo wa mwanadamu kwa namna ambayo katika kipindi fulani cha mwaka huhitaji mabadiliko katika namna ya kuishi na kula; mabadiliko ambayo hupelekea kuinuka kwa roho na kuimarika kwa irada. Ramadhani ni uwanja wa mazoezi ya ibada na kujijenga nafsi, na kwa tafsiri nyingine ni hundi nyeupe yenye saini ya Kimungu kwa ajili ya msamaha na kuangazwa kwa nyoyo.
-
Kikao cha Qur’an katika Husseiniyyah ya Imam Khomeini kikihudhuriwa na Kiongozi Mkuu wa Iran Siku ya Kwanza ya Ramadhan
Kikao cha Qur’an katika Husseiniyyah ya Imam Khomeini (M.A) Siku ya kwanza ya Ramadhan kilisisitiza umuhimu wa Qur’an katika maisha ya kiroho ya Waislamu na thawabu za usomaji wake.
-
Ayatollah Sistani ametangaza kesho (Alhamisi) kuwa ni Siku ya Kwanza ya Ramadhani
Ali al-Sistani ametangaza kuwa kesho Alhamisi ni siku ya Kwanza ya Ramadhani 1447H.
-
Siku za Kufunga Mwezi wa Rajab: Hazina Iliyo fichika kwa Wapendao Imani
Kufunga mwezi wa Rajab ni ufunguo wa kufungua milango ya ufalme wa mbinguni na kuhifadhi thawabu zisizo na kikomo. Riwaya zinaeleza thawabu za kufunga huu kwa namna ambayo inaonekana kama tone moja tu kutoka katika bahari ya radhi ya Mwenyezi Mungu.
-
Kashfa Yazuka Kuhusu Kujiingiza kwa Sara Netanyahu Katika Uteuzi wa Mkuu wa Mossad
Ingawa muungano wa utawala umepongeza uteuzi huo, ndani ya taasisi ya Mossad mwenyewe kuna mshangao mkubwa pamoja na maswali mengi mazito kuhusu uhalali na mchakato wa uteuzi huo.
-
Kuongezeka kwa Mapokezi ya Ziara za Ahlul-Bayt (a.s) Katika Dunia ya Shia Mwisho mwa Mwezi Safar
mwisho wa mwezi Safar ni kipindi cha kipekee cha ziara, kinachotoa fursa ya kiroho, maarifa na kijamii kwa waumini wa Shia, huku akinafunzi na wafuasi wakipata fursa ya kujifunza, kutenda na kuimarisha imani yao kwa Ahlul-Bayt (a.s).
-
Ushiriki wa Vikundi vya Jihadi na Wananchi katika Mahema ya RASHT hadi Mwisho wa Mwezi wa Safar
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (SEPAH) wa Eneo Kuu la RASHT, Kanali Hassan Amini, ametangaza kuhusu kuanzishwa kwa mahema ya wananchi katika barabara ya watembea kwa miguu ya kiutamaduni ya Manispaa ya Rasht kwa mwaka wa nne mfululizo, na kusema kuwa mahema haya, yenye programu za kitamaduni, huduma na kidini, yatapokea wageni na wapenzi wa Sayyid al-Shuhadaa (a.s.) hadi mwisho wa mwezi wa Safar.
-
Likizo ya Wiki Moja katika Mkoa wa Najaf Al-Ashraf kwa Ajili ya Kuwakaribisha Mazuwwari wa Arubaini
Baraza la Mkoa wa Najaf Al-Ashraf limetangaza likizo ya wiki moja kwa ofisi zote za serikali katika mkoa huo, ili kuwezesha ushiriki wa wananchi katika maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s) na kutoa huduma bora kwa maelfu ya mahujaji wanaoelekea Najaf Ashraf.