Baraza
-
Mtaalamu wa Kisiasa: Kulipiza Kisasi cha Kiongozi Shahidi Lazima Kugeuke Kuwa Mkakati wa Kisiasa
Profesa Fouad Izadi amesema suala la kulipiza kisasi cha kiongozi shahidi halipaswi kubaki katika kiwango cha kauli na misemo, bali linapaswa kufuatiliwa kwa njia za kisheria na kisiasa. Ameonya pia kwamba Marekani inaweza kuwa inarudia mbinu ya kutumia mazungumzo na ahadi za makubaliano kama njia ya kudhibiti mwenendo wa Iran na kuandaa mazingira ya hatua nyingine.
-
Rais Pezeshkian Amteua Mohsen Rezaei kuwa Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemteua Mohsen Rezaei kuwa Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, akimtaka kuimarisha uratibu wa taasisi za usalama, kukabiliana na vitisho vipya na vya kiteknolojia, na kulinda umoja wa kitaifa, mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Iran.
-
Ejei kwa Katibu mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa: Kulitumikia taifa la Kiislamu ni wajibu wa lazima
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama ya Iran, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Gholam-Hossein Mohseni Ejei, amempongeza Mohsen Rezaei kwa kuteuliwa kuwa Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, akisisitiza kuwa kulitumikia taifa la Kiislamu ni wajibu wa lazima, hasa katika kukabiliana na njama zinazolenga kuidhoofisha Iran na mfumo wake.
-
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa Iran: Mlango wa Hormuz Hautafunguliwa Marekani Isiporekebisha Mwenendo Wake
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Baqir Zolqadr, amesema kuwa Mlango wa Hormuz hautafunguliwa hadi Marekani itakaporekebisha mwenendo wake, akitaja masharti kadhaa ikiwemo kusitisha vitisho na mashambulizi dhidi ya Iran, kuondoa vikwazo na kulipa fidia ya uharibifu uliosababishwa na vita.
-
Kiongozi wa Yemen: Kulengwa kwa Meli ya Saudi Kumeimarisha Mlingano wa "Mzingiro kwa Mzingiro"
Mjumbe wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Abdulaziz bin Habtour, amesema operesheni ya vikosi vya Yemen dhidi ya meli ya Saudi Arabia imethibitisha kuwa njia mbadala za kukwepa hatua zilizotangazwa na Yemen hazina usalama tena.
-
Qalibaf afichua jinsi taarifa ya kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ilivyoandaliwa kutangazwa
Spika wa Bunge la Ushauri la Kiislamu la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema baada ya kuthibitishwa kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, viongozi wa nchi waliratibu namna ya kutangaza taarifa hiyo na kuwahamasisha wananchi kudumisha umoja.
-
Iraq yakemea mashambulizi ya anga ya Marekani na Saudi Arabia
Serikali ya Iraq imelaani mashambulizi ya Marekani na Saudi Arabia, ikisisitiza kuwa yanakiuka mamlaka yake. Baraza la Usalama wa Taifa limeagiza kuandaliwa kwa mpango wa kukabiliana na ukiukaji huo, huku Wizara ya Mambo ya Nje ikitakiwa kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Iraq pia imeahidi kurekodi matukio hayo na kulinda haki na mamlaka yake ya kitaifa.
-
Dhu al-Qadr: Mashambulizi Endelevu Yataendelea Hadi Adui Asalimu Amri Kikamilifu
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran: “Mashambulizi endelevu na yaliyoelekezwa ya wapiganaji wetu yataendelea hadi adui asalimu amri kikamilifu na kulipiza kisasi kwa damu za watoto wasio na hatia wa Minab na Lamerd.”
-
Afisa wa Lebanon: Makubaliano Mapya na Israel Hayana Uhalali wa Kisheria
Afisa wa Lebanon, Bassam Al-Hashem, amesema kuwa makubaliano ya mfumo yaliyopendekezwa na Israel hayana thamani ya kisheria bila kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri na Bunge la Lebanon, akionya kuwa baadhi ya vipengele vyake vinakiuka mamlaka ya taifa.
-
Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kiislamu la Washia Lebanon: Iran Inaingia Katika Kipindi Kipya cha Nguvu
Sheikh Ali Al-Khatib amesema kuwa baada ya kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, Iran imeingia katika hatua mpya ya nguvu, akisisitiza kuwa misingi ya fikra, dini na maadili ya uongozi wake imejikita kwa kina miongoni mwa Wairani, Waislamu na watu huru duniani.
-
Baraza la Ulamaa BAKWATA Lamsimamisha Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Lateua Kaimu Katika Nafasi Hiyo
Baraza la Ulamaa la BAKWATA, katika kikao chake cha dharura kilichoongozwa na Kaimu Mufti wa Tanzania, Sheikh Ali Khamis Ngeruko, limeazimia kumsimamisha Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam na kumteua Sheikh Abbas Ramadhani kukaimu nafasi hiyo.
-
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa Iran: Shambulio la Miundombinu Litajibiwa kwa Hatua Kama Hiyo
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Baqer Zolqadr, amesema kuwa shambulio lolote dhidi ya miundombinu ya Iran litajibiwa kwa hatua kama hiyo, akisisitiza kuwa Israel haitakwepa majibu ya wapinzani wake.
-
Iran Yalaani Katika Baraza la IMO Mashambulizi ya Marekani Dhidi ya Miundombinu ya Bahari ya Nchi Hiyo
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani katika mkutano wa Baraza la Shirika la Kimataifa la Bahari (IMO) mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya bandari, maeneo ya pwani na miundombinu ya bahari ya Iran, ikiyataja kuwa ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na tishio kwa usalama wa raia na usafiri wa baharini.
-
Lariijani: Ushiriki Katika Mazishi ya Shahidi Ni Ishara ya Imani, Utii na Azma ya Taifa
Mwenyekiti wa Baraza la Uamuzi wa Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu ameueleza kuwa kushiriki katika hafla ya kuaga kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni ishara ya imani, utii na azma ya umma uliosimama katika njia ya uhuru, heshima na muqawama.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (as) Akutana na Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq mjini Baghdad
Mkutano huo uliangazia masuala ya Ulimwengu wa Kiislamu, huku viongozi hao wakitoa salamu za rambirambi na kuzungumzia nafasi ya uongozi wa Kiislamu pamoja na umuhimu wa mshikamano wa Waislamu.
-
Marasimu ya Kumuenzi Ayatollah al-Fayyadh Yafanyika Virginia, Marekani
Kundi la Wanazuoni wa Kiislamu, maimamu wa vituo vya Kiislamu na wajumbe wa Baraza la Wanazuoni wa Kishia wa eneo la Metropolitan Washington walikusanyika Virginia kumuenzi Ayatollah al-Fayyadh na kuenzi mchango wake wa kielimu na kidini.
-
Rais Pezeshkian: Umoja wa Kitaifa Ndiyo Mtaji Mkubwa Zaidi wa Iran Katika Kipindi Hiki
Rais Masoud Pezeshkian amesema mshikamano wa kitaifa ndio msingi wa maendeleo ya Iran, akisisitiza matumizi ya uwezo wa wataalamu na kujibu mahitaji ya wananchi ili kutatua changamoto zinazoikabili nchi.
-
Chanzo Chafichua Rasimu ya Vipengele 14 vya Makubaliano Yanayodaiwa Kupendekezwa kati ya Iran na Marekani
Chanzo kilicho karibu na timu ya mazungumzo ya Iran kimefichua rasimu ya makubaliano yenye vipengele 14 vinavyohusisha usitishaji wa uhasama, kuondolewa kwa vikwazo, kufunguliwa kwa Mlango wa Hormuz, pamoja na kuachiliwa kwa mabilioni ya dola za mali za Iran zilizogandishwa.
-
Iran Yaukosoa Mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Yasema Azimio 2231 Lilikoma Mwaka Jana
Ujumbe wa Iran katika Umoja wa Mataifa umeelezea kikao cha Baraza la Usalama kuhusu Iran kuwa ni “onyesho jingine la unafiki na viwango viwili,” ukisisitiza kuwa Azimio Na. 2231 la Baraza la Usalama lilimalizika rasmi Oktoba 18, 2025 na kwamba hakuna tena msingi wa kisheria wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran.
-
Mkwamo katika Bunge la Iraq; mizani ya kisiasa yameelemea kwa Waislamu wa Kishia na Wakurdi
Wakati ambapo Waislamu wa Kisunni wameshindwa kufikia mwafaka juu ya mgombea mmoja, hatima ya urais wa Bunge la Iraq imefungamana zaidi kuliko wakati mwingine wowote na maamuzi pamoja na hesabu za kisiasa za Waislamu wa Kishia na vyama vya Kikurdi.
-
Makamu wa Rais wa Baraza Kuu la Waishe Shia wa Lebanon: Msitoe hata nafasi wala marupurupu kwa adui Mzayuni
Sheikh Ali Al-Khatib, Rais wa Baraza Kuu la Kiislamu la Mashia wa Lebanon, ameitaka serikali isitoe marupurupu ya kihalisi au kisiasa bila malipo kwa adui wa Kizayuni.
-
Iran: Kukabiliana na ugaidi kunahitaji ushirikiano wa kikanda, hasa na Afghanistan
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran alitangaza kuwa makundi ya kigaidi hayapo tu nchini Afghanistan, bali yameenea katika nchi mbalimbali za eneo hilo. Alisisitiza kuwa kukabiliana na tishio hili kunahitaji ushirikiano wa pamoja wa nchi jirani, hasa Afghanistan.
-
Kongamano la Waombolezaji wa Kike wa Fatimiyyah Kufanyika Mjini Qom - Iran
Wanawake waumini jijini Qom watafanya matembezi ya maombolezo hadi kwenye kaburi la Shahidi Asiyejulikana katika chuo cha Jami‘atu-z-Zahra (a), wakiomboleza kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a), Mama wa Maimamu wa Ahlul-Bayt (as).
-
Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Iraq:
Hatukuruhusu wala hatutaruhusu anga ya Baghdad itumike dhidi ya Iran
Ali Larijani: “Hatukuruhusu, wala hatutaruhusu anga ya Baghdad au mipaka ya Iraq itumike dhidi ya Iran. Hatupaswi kuruhusu upande wowote kuvuruga usalama wa eneo hili.”
-
Katika mazungumzo ya simu kati ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Pakistan:
Araghchi alisema: “Azimio namba 2231 la Baraza la Usalama linapaswa kuchukuliwa kuwa limekamilika na kuhitimishwa kwa wakati uliopangwa.”
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, huku akishukuru msimamo wa uwajibikaji wa Pakistan katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kupinga matumizi mabaya ya nchi tatu za Ulaya, alisisitiza kwamba Azimio namba 2231 lazima, kwa mujibu wa masharti yake na maandiko ya makubaliano ya nyuklia (JCPOA), lichukuliwe kuwa limekamilika katika muda uliopangwa, yaani tarehe 26 Mehr 1404 (18 Oktoba 2025).
-
Ismail Baghaei – Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran:
Amesema kuwa taarifa ya Kundi la G7 kuhusu kurejesha vikwazo vya Baraza la Usalama dhidi ya Iran ni ya kinafiki na yenye upotoshaji.
Ismail Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amelaani na kulikemea tamko la Kundi la G7 kuhusu suala la nyuklia la Iran, akilitaja kuwa ni la kinafiki na kupotosha ukweli.
-
Jenerali Shakarchi: Uzalishaji wa Makombora ya Iran Hautasimama Kamwe / Uzoefu wa Libya Umeonyesha Kuondoa Silaha Kunaleta Uharibifu Tu
Shakarchi aliongeza: Adui walidhani kuwa kuendelea kwa vita zaidi ya wiki moja kutasababisha uchovu na kuchoshwa kwa watu, lakini ushiriki mkubwa wa umma na msaada usiokatizwa kwa Mapinduzi na mfumo viligonga mipango yao yote na mfululizo wa kushindwa kwao ukaendelea.
-
Upigaji kura wa leo katika Baraza la Usalama kuhusu kurejesha vikwazo dhidi ya Iran
Uanzishaji wa ‘mfumo wa kichocheo’ (Snapback mechanism / Triger Machanism) na Ulaya umeiweka Baraza la Usalama katika hali nyeti; ambapo kupinga azimio jipya kunamaanisha kurejea kwa vikwazo vyote dhidi ya Iran.
-
Kuongezwa kwa muda wa uteuzi wa Majukumu ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu
Kiongozi wa Mapinduzi ameidhinisha kuongezwa kwa muda wa jukumu la Hujjatul-Islam Shahriari kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu
-
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini:
"Swala ya Ijumaa ni nguzo ya Umoja wa Kitaifa - Lazima iwafikie watu wa makundi yote"
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini: "Swala ya Ijumaa inapaswa kuwa ya watu wote na kuakisi umoja wa kitaifa."Akiangazia umuhimu wa nafasi ya wananchi na ushirikishi mpana katika Swala ya Ijumaa, mwenyekiti huyo alisema: “Makamati ya Swala ya Ijumaa yanapaswa kwa ubunifu na upangaji madhubuti, kuweka mazingira yanayowezesha ushiriki wa watu wa makundi yote ya jamii — kuanzia wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu na wasomi, hadi wafanyakazi wa viwandani na wakulima.” Aliongeza kuwa kwa njia hii, ibada hii ya kiroho na kisiasa itakuwa ni taswira kamili ya mshikamano na umoja wa kitaifa.