Baraza
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (as) Akutana na Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq mjini Baghdad
Mkutano huo uliangazia masuala ya Ulimwengu wa Kiislamu, huku viongozi hao wakitoa salamu za rambirambi na kuzungumzia nafasi ya uongozi wa Kiislamu pamoja na umuhimu wa mshikamano wa Waislamu.
-
Marasimu ya Kumuenzi Ayatollah al-Fayyadh Yafanyika Virginia, Marekani
Kundi la Wanazuoni wa Kiislamu, maimamu wa vituo vya Kiislamu na wajumbe wa Baraza la Wanazuoni wa Kishia wa eneo la Metropolitan Washington walikusanyika Virginia kumuenzi Ayatollah al-Fayyadh na kuenzi mchango wake wa kielimu na kidini.
-
Rais Pezeshkian: Umoja wa Kitaifa Ndiyo Mtaji Mkubwa Zaidi wa Iran Katika Kipindi Hiki
Rais Masoud Pezeshkian amesema mshikamano wa kitaifa ndio msingi wa maendeleo ya Iran, akisisitiza matumizi ya uwezo wa wataalamu na kujibu mahitaji ya wananchi ili kutatua changamoto zinazoikabili nchi.
-
Chanzo Chafichua Rasimu ya Vipengele 14 vya Makubaliano Yanayodaiwa Kupendekezwa kati ya Iran na Marekani
Chanzo kilicho karibu na timu ya mazungumzo ya Iran kimefichua rasimu ya makubaliano yenye vipengele 14 vinavyohusisha usitishaji wa uhasama, kuondolewa kwa vikwazo, kufunguliwa kwa Mlango wa Hormuz, pamoja na kuachiliwa kwa mabilioni ya dola za mali za Iran zilizogandishwa.
-
Iran Yaukosoa Mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Yasema Azimio 2231 Lilikoma Mwaka Jana
Ujumbe wa Iran katika Umoja wa Mataifa umeelezea kikao cha Baraza la Usalama kuhusu Iran kuwa ni “onyesho jingine la unafiki na viwango viwili,” ukisisitiza kuwa Azimio Na. 2231 la Baraza la Usalama lilimalizika rasmi Oktoba 18, 2025 na kwamba hakuna tena msingi wa kisheria wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran.
-
Mkwamo katika Bunge la Iraq; mizani ya kisiasa yameelemea kwa Waislamu wa Kishia na Wakurdi
Wakati ambapo Waislamu wa Kisunni wameshindwa kufikia mwafaka juu ya mgombea mmoja, hatima ya urais wa Bunge la Iraq imefungamana zaidi kuliko wakati mwingine wowote na maamuzi pamoja na hesabu za kisiasa za Waislamu wa Kishia na vyama vya Kikurdi.
-
Makamu wa Rais wa Baraza Kuu la Waishe Shia wa Lebanon: Msitoe hata nafasi wala marupurupu kwa adui Mzayuni
Sheikh Ali Al-Khatib, Rais wa Baraza Kuu la Kiislamu la Mashia wa Lebanon, ameitaka serikali isitoe marupurupu ya kihalisi au kisiasa bila malipo kwa adui wa Kizayuni.
-
Iran: Kukabiliana na ugaidi kunahitaji ushirikiano wa kikanda, hasa na Afghanistan
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran alitangaza kuwa makundi ya kigaidi hayapo tu nchini Afghanistan, bali yameenea katika nchi mbalimbali za eneo hilo. Alisisitiza kuwa kukabiliana na tishio hili kunahitaji ushirikiano wa pamoja wa nchi jirani, hasa Afghanistan.
-
Kongamano la Waombolezaji wa Kike wa Fatimiyyah Kufanyika Mjini Qom - Iran
Wanawake waumini jijini Qom watafanya matembezi ya maombolezo hadi kwenye kaburi la Shahidi Asiyejulikana katika chuo cha Jami‘atu-z-Zahra (a), wakiomboleza kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a), Mama wa Maimamu wa Ahlul-Bayt (as).
-
Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Iraq:
Hatukuruhusu wala hatutaruhusu anga ya Baghdad itumike dhidi ya Iran
Ali Larijani: “Hatukuruhusu, wala hatutaruhusu anga ya Baghdad au mipaka ya Iraq itumike dhidi ya Iran. Hatupaswi kuruhusu upande wowote kuvuruga usalama wa eneo hili.”
-
Katika mazungumzo ya simu kati ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Pakistan:
Araghchi alisema: “Azimio namba 2231 la Baraza la Usalama linapaswa kuchukuliwa kuwa limekamilika na kuhitimishwa kwa wakati uliopangwa.”
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, huku akishukuru msimamo wa uwajibikaji wa Pakistan katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kupinga matumizi mabaya ya nchi tatu za Ulaya, alisisitiza kwamba Azimio namba 2231 lazima, kwa mujibu wa masharti yake na maandiko ya makubaliano ya nyuklia (JCPOA), lichukuliwe kuwa limekamilika katika muda uliopangwa, yaani tarehe 26 Mehr 1404 (18 Oktoba 2025).
-
Ismail Baghaei – Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran:
Amesema kuwa taarifa ya Kundi la G7 kuhusu kurejesha vikwazo vya Baraza la Usalama dhidi ya Iran ni ya kinafiki na yenye upotoshaji.
Ismail Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amelaani na kulikemea tamko la Kundi la G7 kuhusu suala la nyuklia la Iran, akilitaja kuwa ni la kinafiki na kupotosha ukweli.
-
Jenerali Shakarchi: Uzalishaji wa Makombora ya Iran Hautasimama Kamwe / Uzoefu wa Libya Umeonyesha Kuondoa Silaha Kunaleta Uharibifu Tu
Shakarchi aliongeza: Adui walidhani kuwa kuendelea kwa vita zaidi ya wiki moja kutasababisha uchovu na kuchoshwa kwa watu, lakini ushiriki mkubwa wa umma na msaada usiokatizwa kwa Mapinduzi na mfumo viligonga mipango yao yote na mfululizo wa kushindwa kwao ukaendelea.
-
Upigaji kura wa leo katika Baraza la Usalama kuhusu kurejesha vikwazo dhidi ya Iran
Uanzishaji wa ‘mfumo wa kichocheo’ (Snapback mechanism / Triger Machanism) na Ulaya umeiweka Baraza la Usalama katika hali nyeti; ambapo kupinga azimio jipya kunamaanisha kurejea kwa vikwazo vyote dhidi ya Iran.
-
Kuongezwa kwa muda wa uteuzi wa Majukumu ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu
Kiongozi wa Mapinduzi ameidhinisha kuongezwa kwa muda wa jukumu la Hujjatul-Islam Shahriari kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu
-
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini:
"Swala ya Ijumaa ni nguzo ya Umoja wa Kitaifa - Lazima iwafikie watu wa makundi yote"
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini: "Swala ya Ijumaa inapaswa kuwa ya watu wote na kuakisi umoja wa kitaifa."Akiangazia umuhimu wa nafasi ya wananchi na ushirikishi mpana katika Swala ya Ijumaa, mwenyekiti huyo alisema: “Makamati ya Swala ya Ijumaa yanapaswa kwa ubunifu na upangaji madhubuti, kuweka mazingira yanayowezesha ushiriki wa watu wa makundi yote ya jamii — kuanzia wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu na wasomi, hadi wafanyakazi wa viwandani na wakulima.” Aliongeza kuwa kwa njia hii, ibada hii ya kiroho na kisiasa itakuwa ni taswira kamili ya mshikamano na umoja wa kitaifa.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Akhtari kwa Sayyid Abdul Malik al-Houthi: Shambulio la Israel Nchini Yemen ni Jinai Mpya ya Kivita
"Ninatoa rambirambi zangu za dhati kwa watu wa Yemen mashujaa na kwa uongozi wake jasiri – ukiwemo wewe ndugu yetu mpendwa, Sayyid Abdul Malik – kwa msiba huu mkubwa wa kifo cha Shahidi Ahmad Ghalib al-Rahwi na wenzake waliouawa kwa udhalimu na usaliti wa utawala haramu wa Kizayuni.”
-
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa jukumu la UNIFIL nchini Lebanon hadi mwisho wa mwaka 2026.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeamua kuongeza muda wa jukumu la wanajeshi wa UNIFIL kusini mwa Lebanon kwa mara ya mwisho.
-
Baraza la Utamaduni la Ubalozi wa Iran Nairobi Latuma Salamu za Rambirambi kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s) na Shahada ya Imam Hassan a.s
Siku hii pia inakumbusha shahada ya Imam Hassan (a.s), Imam wa pili katika Ahlul-Bayt (a.s), aliyefahamika kwa msimamo wake wa amani na kujitolea kwake kwa ajili ya haki. Kifo chake ni alama ya mapambano ya kudumu kwa ajili ya uadilifu na uongofu.
-
Mkutano wa Haji Muhammad Muhaqiq na Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Iraq
Mchana wa Jumamosi tarehe 25 Mordad 1404 (sawa na Agosti 16, 2025), Haji Muhammad Muhaqiq, kiongozi wa Chama cha Umoja wa Kiislamu wa Watu wa Afghanistan, alikutana na Dk. Humam al-Hammoudi, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Iraq, na kufanya mazungumzo naye.
-
Ahadi Mpya za Taliban / Ufunguzi wa Shule za Wasichana Wategemea "Kibali cha Kisharia"
Zabihullah Mujahid, msemaji wa serikali ya Taliban, ametangaza kuwa mchakato wa kupata “kibali sahihi cha kisharia” kwa ajili ya kufunguliwa tena shule na vyuo vikuu vya wasichana bado unaendelea. Hii ni baada ya zaidi ya miaka minne ya kunyimwa wanawake na wasichana haki ya msingi ya elimu.
-
Katibu wa Usalama wa Taifa Iran: “Muqawama ni Hazina Kuu kwa Eneo na Umma wa Kiislamu"
Larijani alitembelea Iraq na Lebanon kwa mazungumzo na viongozi wakuu, akiwemo Rais Joseph Aoun na Spika Nabih Berri.
-
Ayatollah Makarim Shirazi: Baraza la Uratibu wa Matangazo Lina Nafasi Muhimu Katika Kulinda Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu
Ayatollah Makarim Shirazi amethibitisha kwamba Baraza la Uratibu wa Matangazo ya Kiislamu lina mchango mkubwa usio na mfano katika kuhifadhi mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Ayatollah Jannati:
Hamasa ya Arubaini ni Taa ya Waombao Haki Duniani / Kudhibiti Gaza Kikamilifu na Kuliweka Chini ya Silaha Hizbullah ni Ndoto ya Ovyo
madai ya kuteka Gaza kikamilifu na kulivua silaha jeshi la Hizbullah ni “ndoto ya ovyo,” na kwamba harakati ya kudai haki ya upinzani, kwa kutegemea mafundisho ya Uislamu na kuiga Mapinduzi ya Kiislamu, hatimaye itafikia ushindi.
-
Marekani Yapongeza Uamuzi wa Baraza la Mawaziri wa Lebanon wa Kulazimisha Udhibiti wa Silaha Mikononi mwa Serikali
Mjumbe wa Marekani afurahishwa na hatua ya baraza la mawaziri la Lebanon dhidi ya silaha za Muqawama.
-
Likizo ya Wiki Moja katika Mkoa wa Najaf Al-Ashraf kwa Ajili ya Kuwakaribisha Mazuwwari wa Arubaini
Baraza la Mkoa wa Najaf Al-Ashraf limetangaza likizo ya wiki moja kwa ofisi zote za serikali katika mkoa huo, ili kuwezesha ushiriki wa wananchi katika maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s) na kutoa huduma bora kwa maelfu ya mahujaji wanaoelekea Najaf Ashraf.