Ayatollah Javadi Amoli
-
Ayatollah al-Udhma Javadi Amoli:
Maneno ya Ahlul-Bayt yana uzito sawa na Qur’an / “Tunapaswa kujiakisi kwa kushikamanisha nafsi zetu na viumbe walio hai na walio katika njia ya Haki
“Kile ambacho ni utambulisho wa Ahlul-Bayt (a.s), ni kilekile ambacho ni utambulisho wa Qur’an; ikiwa Qur’an inazungumza kwa ukweli, basi Ahlul-Bayt (a.s) pia wanazungumza kwa kweli, na ikiwa walisitiza kusema kitu fulani, kilikuwa kwa kweli.”
-
Ayatollah Al-Udhma Abdullah Javadi Amoli amesema kwamba “Kuunganisha Sanaa na Ushairi na Tauhidi ni ngao dhidi ya vitisho vya kigeni"
Ayatollah Al-Udhma Abdullah Javadi Amoli alisisitiza umuhimu wa kuunganisha sanaa na ushairi na Tauhidi (umoja wa kumpwekesha Mwenyezi Mungu), akisema kuwa iwapo mafundisho ya tauhidi yatahuishwa kwa sura yake halisi, basi jamii ya Kiislamu haitapotea wala kukumbwa na vitisho kutoka kwa maadui.
-
Hazrat Ayatollah Javadi Amoli:
Siku ya Quds ni sehemu ya "Siku ya Kimataifa ya Uislamu"
Ayatollah Javadi Amoli, akiwaalika watu kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alisema: Ni wajibu wetu sote kushiriki katika Maandamano haya, kwanza, Na kila mmoja wetu kwa mujibu wa elimu tuliyo nayo, awe na nia ya Tawalli na Tabarri ya Kimungu, pili, na kujaribu kufayanya kuwa maandamano mapana zaidi, tatu, yaani tuyafanye maandamano haya kwa nia ya kuwa karibu na kuwaheshimu na kuwathamini Mashahidi wa njia hii, ili hatua hizi zote zithibitishwe na Dhati Takatifu ya Mwenyezi Mungu.