Bendera
-
Bendera ya “Ya Hussein” Yaibuka Juu Uwanjani Los Angeles Wakati wa Mechi ya Iran na Ubelgiji
Wakati wa mechi ya Kombe la Dunia kati ya Iran na Ubelgiji iliyofanyika katika uwanja wa Los Angeles, mashabiki walishuhudia tukio la kipekee ambapo bendera kubwa iliyoandikwa “Ya Hussain” iliinuliwa juu kwenye jukwaa la watazamaji, ikionesha mchanganyiko wa imani ya kidini na burudani ya soka. Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bila kufungana (0–0).
-
Bendera ya Maombolezo ya Imam Hussain (AS) Yapandishwa katika Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh kuukaribisha Mwezi wa Muharram
Mamia ya Mazuwwari na wakazi wa mji wa Qom walishiriki hafla ya kupandisha Bendera Nyeusi ya maombolezo ya Imam Hussein (AS) juu ya Kuba la Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh (SA), kuashiria kuanza kwa Mwezi Mtukufu wa Muharram na kumbukumbu ya Mashahidi wa Karbala.
-
Ukuta wa Ujumbe Mpya Chuo Kikuu cha Tehran: “Bendera ya Iran Haichomeki"
Ukuta wenye ujumbe “Jaribu uteketezwe bure, bendera ya Iran haitachomeka” umewekwa katika eneo la Chuo Kikuu cha Tehran, hususan katika jengo la Kitivo cha Sayansi ya Jamii, ikiwa ni mwitikio wa matukio ya jana yaliyohusishwa na baadhi ya wanafunzi wanaodaiwa kufanya vitendo vya uchochezi.
-
Maadhimisho ya Kifo cha Bibi Fatima Umm ul-Banin (a.s)
Bibi Ummul-Baneen aliwapenda Ahlul-Bayt wa Mtume kuliko alivyowapenda wanawe mwenyewe. Alipopata habari za huzuni za Karbala, hakumuuliza kwanza kuhusu wanawe wanne, bali alisema: “Nijulisheni kuhusu Hussein.”
-
Picha kuhusu mradi wa fani ya ushonaji kwa ajili ya Palestina katika Msikiti wa Afrika Kusini
Baadhi ya wanaharakati na wafuasi wa Palestina nchini Afrika Kusini wanashona vipande vya kitambaa vyenye rangi za bendera ya Palestina, kuunda kazi ya ishara ya kumbukumbu kwa watoto waliopoteza maisha katika vita vya Ghaza. Kazi hii itafunguliwa rasmi mnamo tarehe 29 Novemba, Siku ya Kimataifa ya Umoja na Palestina.
-
Hamza(ra), Bendera ya Kwanza ya Uislamu
Hamza bin Abdulmuttalib (ra), ami yake Mtume wa Uislamu(saww), anajulikana kama Bendera ya kwanza ya Uislamu. Kwa ujasiri na kujitolea kwake katika kumtetea Mtume na mafundisho ya Kiislamu, alicheza nafasi muhimu katika kueneza Uislamu. Hamza hakuwa tu shujaa katika uwanja wa vita, bali pia alikuwa mfano na mlinzi wa Waislamu, daima akiwa upande wa Mtume na kwa msimamo wake, alitia nguvu na matumaini katika nyoyo za waumini.
-
Dkt. Larijani: Sayyid Hassan Nasrallah alikuwa hazina kubwa kwa ulimwengu wa Kiislamu
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, katika ziara yake kwenye eneo la Dahieh Kusini mwa Beirut na kutembelea kaburi la Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, alimueleza kuwa ni hazina kubwa kwa ulimwengu wa Kiislamu na kusisitiza juu ya kuendeleza njia ya muqawama (upinzani wa haki).