Luiz Roberto Alves, profesa mashuhuri wa Chuo Kikuu cha São Paulo (USP), mwanazuoni wa elimu na mtetezi mahiri wa haki ya kijamii, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 78 katika mji wa São Paulo. Kifo chake kimeacha pengo kubwa katika nyanja ya elimu ya umma, usomeshaji na sera za kijamii nchini Brazili.
Rais wa Brazil Lula da Silva akizungumza katika mkutano wa kimataifa mjini New York Marekani amesisitiza juu ya ulazima wa kutatuliwa kwa amani suala la Palestina na kutekelezwa kwa mapatano ya serikali mbili.
Chuo Kikuu cha Amsterdam kimefuta mpango wa kubadilishana wanafunzi na Chuo Kikuu cha Kiebrania cha Yerusalemu, huku Jumuiya ya Ulaya ya Wanaanthropolojia wa Kijamii ikitangaza marufuku ya aina yoyote ya ushirikiano na Israel.