Jibu
-
Iran Yasema Iko Tayari kwa Vita Huku Mvutano wa Kikanda Ukiongezeka
Kauli hiyo inatolewa wakati mvutano ukiendelea kuongezeka katika Mashariki ya Kati, hususan kuhusiana na Israel na Marekani, kufuatia mapigano ya hivi karibuni ya kijeshi na kusimama kwa juhudi za kidiplomasia kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.
-
Zelensky: Ukraine Inatarajia Jibu la Moscow Kuhusu Rasimu ya Kumaliza Vita, Ikiikataa Sharti la NATO
Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, ameiweka wazi kuwa anatarajia kupokea jibu la Moscow leo Jumatano kuhusu rasimu mpya ya pendekezo la kumaliza vita, iliyokubaliwa awali kati ya Washington na Kyiv. Hata hivyo, Zelensky amesisitiza kuwa Ukraine haitaweza kukubali sharti lolote linalohusiana na kujiunga au kutokuwa mwanachama wa NATO, jambo ambalo Urusi ilikuwa imependekeza, akionyesha wazi kuwa suala hilo haliwezi kuwa kikwazo cha mazungumzo ya amani.
-
Jibu la Ayatollah Al-Udhma Sistani Kuhusu Kufuata Maimam wa Sala ya Jamaa Wanaopokea Malipo (Mishahara) za Kiserikali
Ayatollah Al-udhma Al-Sistani, kiongozi mkuu wa Shi’a, katika jibu lake kwa swali kuhusu kufuata maimamu wa sala ya jamaa (imam wa jamaa) wanaopokea haki (ya mishahara) kutoka serikali za Kiislamu, alishauri waumini wasisali nyuma yao, ili nafasi za kidini zilindwe dhidi ya uingiliaji wowote unaowezekana wa serikali.
-
Jibu la Kabul kwa Trump: Uwepo wa Marekani nchini Afghanistan hauna uwezekano
Serikali ya Taliban imejibu kauli za Donald Trump kuhusu kurejesha kambi ya Bagram kwa kusema kuwa uwepo wa kijeshi wa Marekani nchini Afghanistan ni jambo lisilowezekana kabisa.
-
Chama cha Kimataifa cha Utafiti wa Mauaji ya Kimbari: Israel Imetekeleza Mauaji ya Kimbari Gaza
Rais wa chama kikubwa zaidi duniani cha wataalamu wa masuala ya mauaji ya kimbari (IAGS) ametangaza kuwa taasisi hiyo imepitisha azimio linalothibitisha kuwa vitendo vya Israel katika Ukanda wa Gaza vinaendana na vigezo vya kisheria vya mauaji ya kimbari.