Katika mnasaba wa maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS), Waislamu wa Shia na Sunni walikusanyika kujadili kuhusu Mwokozi wa Ulimwengu na wajibu wa Waumini katika kipindi cha Ghaiba. Khatibu Sheikh Suleimani Abdully aliwakumbusha vijana juu ya umuhimu wa kumcha Mwenyezi Mungu, kushukuru neema Zake na kujenga tabia njema ili kuandaa jamii yenye utu, uadilifu na iliyoepukana na dhulma na ufisadi.
"Unaweza kumdhulumu mtu na ukalala usingizi mzito, lakini yule uliyemdhulumu halali kamwe. Anakumbuka dhulma yako kila siku na humlalamikia Mwenyezi Mungu dhidi yako. Na ikumbukwe kuwa macho ya Mwenyezi Mungu hayalali,” amesema Sheikh Ahmad Haji, akisisitiza hatari ya dua ya aliyedhulumiwa.