Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Msemaji wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo vinatumia kikamilifu fursa ya kipindi cha usitishaji mapigano ili kuendelea kuimarisha uwezo wake wa kijeshi, akibainisha kuwa hakuna hata dakika moja inayopotezwa katika kujiandaa kwa ajili ya kulinda usalama wa taifa.
Aidha, msemaji huyo alisisitiza kwamba iwapo adui atafanya kosa lolote au kuchukua hatua ya uchokozi, Iran itajibu kwa uthabiti na nguvu zote.
Akizungumzia mzozo kati ya Iran na Israel, alisema kuwa ni mzozo wa kimkakati unaohusu mustakabali wa pande hizo mbili, akidai kuwa kwa mtazamo wake Israel haitaendelea kuwepo katika siku zijazo.
Your Comment