Kutisha
-
Msimu wa Mizeituni Umekuwa Msimu wa Mauaji katika Ukingo wa Magharibi | Ukandamizaji na mashambulizi ya wakoloni wa Kizayuni yaongezeka kwa ukatili
Msimu wa mavuno ya mizeituni - ishara ya amani na ustawi kwa Wapalestina - umegeuzwa na utawala wa Kizayuni kuwa msimu wa hofu, damu na uharibifu. Ukandamizaji na mashambulizi ya wakoloni wa Kizayuni yaongezeka kwa mpangilio na ukatili mkubwa
-
Janga la Kibinadamu Gaza; Watoto Yatima Katika Hali ya Ndoto Mbaya
Janga la kibinadamu katika Ukanda wa Gaza limeharibu maisha ya maelfu ya watoto. Watoto hawa wamekuwa wakikabiliana na hali ya kukimbia, njaa, kifo cha wapendwa, na vurugu za kutisha kwa takriban miaka miwili. Ripoti zinaonyesha kuwa zaidi ya watu 65,000 wamefariki Gaza, huku maelfu ya watoto wakipoteza wazazi wao. Hali hii ya ukosefu wa usalama na mahitaji ya msingi inatengeneza athari kubwa za kimahusiano na kisaikolojia kwa vizazi vijavyo, na kufanya msaada wa haraka wa kimataifa kuwa jambo la dharura. Watoto hawa yatima sasa wanahitaji hifadhi, chakula, huduma za afya na msaada wa kisaikolojia ili kuweza kuendelea na maisha yao.
-
Katika taarifa ya pekee imesema:
"Wanaume majemedari wa Ansarullah wamewaacha Wazayuni katika wasi wasi / Taifa la Yemen linamfufua mataifa yaliyozama usingizini"
“Umma wa Malk Khashab,” Mwanahabari wa kike wa Ansarullah, aliandika: Katika mapambano kati ya wavamizi na Wazayuni dhidi ya Yemen, hesabu zote zimebadilika na mizani imegeuzwa. Kwa hivyo, walianza kulia na kupiga kelele kutokana na wanaume imara wa Yemen na wana-yemen kwa ujumla, na sasa Yemen imekuwa moto wa kuotea mbali na ndoto za kutisha kwao zinazowaamsha mara kwa mara.
-
Salam za Rambirambi za Baraza la Maulamaa na Wenye Mamlaka wa Madhhebu ya Shia nchini Afghanistan Kufuatia Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
Baraza la Maulamaa na Watu Wenye Mamlaka wa Madhehebu ya Shia nchini Afghanistan, kupitia taarifa rasmi, limeeleza masikitiko na mshikamano wao na familia za waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni katika mkoa wa Kunar, mashariki mwa Afghanistan, huku likisisitiza umoja wa kitaifa na hitajio la msaada wa haraka kwa waathirika.