Majlis
-
Rais wa Majlisi ya Umoja wa Waislamu Pakistan atangaza wasiwasi juu ya ongezeko kubwa la mashambulizi ya kigaidi
Rais wa Majlis ya Umoja wa Waislamu nchini Pakistan, Seneta Raja Nasir Abbas Jafari, ameonesha wasiwasi mkubwa kufuatia ongezeko la kasi la mashambulizi ya kigaidi katika wiki za hivi karibuni, akisisitiza kuwa mashambulizi haya si ya bahati mbaya, bali ni sehemu ya kampeni mahsusi inayolenga kuisukuma Pakistan kuelekea hali ya kutokuwa na utulivu.
-
Majlis ya Kuhuisha Shahada ya Sayyidat Fatima Al-Zahra (sa) kwa Akina Mama Jijini Dar es Salaam +Picha
Katika khutba yake, Sheikh Ja'far Mwazoa alieleza kwa ufafanuzi wa kina fadhila zake nyingi, akibainisha namna ambavyo Bibi Fatima (sa) ni kigezo bora cha kuigwa na wanawake wote wa Kiislamu, na hata wanaume wa Umma wa Mtume Muhammad (saww), kutokana na uchamungu wake, hekima yake, na msimamo wake thabiti katika kutetea ukweli.
-
Mwenyekiti wa Chama cha Majlis Ittehad-ul-Muslimeen nchini India;
Ameonesha msimamo wake kufuatia mjadala uliyoibuka dhidi ya bango lenye maandishi “Nampenda Muhammad”.
Kiongozi wa chama cha Majlis Ittehad-ul-Muslimeen nchini India, akijibu mzozo ulioibuka kutokana na mabango yenye maandishi “Nampenda Muhammad” katika jimbo la Uttar Pradesh, ameishutumu serikali ya India na viongozi wa eneo hilo kwa kuweka vizuizi vya kibaguzi na vya upendeleo.
-
Baraza la Utamaduni la Ubalozi wa Iran Nairobi Latuma Salamu za Rambirambi kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s) na Shahada ya Imam Hassan a.s
Siku hii pia inakumbusha shahada ya Imam Hassan (a.s), Imam wa pili katika Ahlul-Bayt (a.s), aliyefahamika kwa msimamo wake wa amani na kujitolea kwake kwa ajili ya haki. Kifo chake ni alama ya mapambano ya kudumu kwa ajili ya uadilifu na uongofu.
-
Hawzat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni - Dar-es-salaam | Wanawake katika Kuadhimisha Shahadat ya Imam Sadiq (a.s) + Picha
Wanawake katika jamii za Kiislamu wanachukua jukumu muhimu katika kuadhimisha kifo cha Kishahidi cha Imam Sadiq (a.s), ambapo si tu wanahudhuria kimwili katika vikao kama hivi vya Maombolezo, bali pia wanashiriki kikamilifu kwa njia ya vitendo katika kueneza mafundisho ya Imam Sadiq (as) katika nyanja mbalimbali.
-
Kauli mbiu: Amani ya Palestina ni Amani ya Tanzania;
Majlis ya Siku ya Kupigwa Upanga Imam Ali (a.s), imefanyika katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Adui Ibn Muljim (laana iwe juu yake), aliyempiga Imam Ali (a.s) kwa upanga wenye sumu kali, alijua kuwa hawezi kupambana na Imam Ali (a.s) akiwa nje ya Msikiti, hivyo akaona mbinu aliyokuwa nayo ni kumuwinda akiwa katika ibada (swala), kwani awapo katika swala huwa mwili wake na hisia zake zinatoweka Duniani, na anazungumza na Mola wake Mtukufu kama vile hayupo Duniani".