Shughuli za Imam Hadi (a.s) zilikuwa na nafasi muhimu katika kuhifadhi utambulisho wa kiakili na imani wa Waislamu wafuasi wa Madhehebu ya Shi'a Ithna Ashari. Uongozi wake wa kiroho na wa fikra kwa Shi'a waliokuwa Samarra, kuimarisha mtandao wa mawasiliano kati ya wafuasi wa Ahlul Bayt(as), na kusimama imara dhidi ya shinikizo la wa Abbasi, ni miongoni mwa huduma muhimu za Imamu Hadi katika maandalizi ya Shi'a kwa zama za Ghaibat Kubwa (Kutoonekana kwa Muda Mrefu).
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) amesema kuwa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni mwangaza unaotokana na fikra na mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s), na kuongeza kuwa: Magharibi wanajitahidi kupotosha taswira ya Uislamu mbele ya dunia, hivyo ni jukumu letu kusimulia ukweli halisi wa Uislamu Sahihi na wa Haki kwa kutumia njia za kisasa za Mawasiliano na Vyombo vya Habari.