Sheikh Naim Qassem
-
Kauli ya Sheikh Naim Qassem: Makubaliano ya Mfumo kati ya Lebanon na Israel ni “Fedheha na Kusaliti Mamlaka ya Taifa”
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
-
Sheikh Naim Qassem: Israel itaondoka kabisa katika ardhi ya Lebanon, hakuna maelewano ya kusalimu amri
Naibu Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amesema Israel hatimaye itaondolewa kikamilifu katika kila kipande cha ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa harakati yao haiko tayari kwa maelewano ya kusalimu amri na kwamba njama za kuangamiza Hezbollah zimefeli.
-
Sheikh Naïm Qassem: “Tumezaliwa huru kupinga dhulma, ukoloni na utegemezi; upinzani dhidi ya adui ni haki halali”
Sheikh Naim Qassem amesema kuwa wao wamezaliwa huru na wamechagua kwa makusudi kupinga dhulma, ukoloni na utegemezi wa kigeni, akisisitiza kuwa kujibu adui kwa silaha ni haki ya kujilinda, na kwamba kushikamana na kaulimbiu ya “Hussein ndiyo njia yetu” ni msingi wa kuendelea kwao katika mapambano na ushindi dhidi ya ukandamizaji.
-
Sheikh Naim Qassem: Iran ni Alama ya Heshima na Nguzo ya Muqawama Dhidi ya Israel
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amesema katika barua yake kwa Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, kwamba Iran imeonyesha kwa vitendo uungaji mkono wake kwa haki, muqawama na waliodhulumiwa. Ameeleza kuwa mchango wa Iran umeimarisha uwezo wa Lebanon kujitetea na kuitaja Iran kuwa "alama ya heshima na utukufu" katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni.
-
IRGC Yakanusha Taarifa za Kuuawa kwa Katibu Mkuu wa Hizbullah Sheikh Naim Qassem
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limezitaja kuwa za uongo taarifa zinazodai kuwa Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sheikh Naim Qassem, ameuawa katika shambulio la Israel kusini mwa Beirut, likisema ni sehemu ya vita vya kisaikolojia na upotoshaji wa habari.
-
Naim Qassem: Hezbollah Haitasalimisha Silaha na Itaendelea Kupambana Hadi Israel Iondoke Lebanon
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Naim Qassem, amesema Hezbollah haitasalimisha silaha zake wala kukubali makubaliano ya mazungumzo kati ya Lebanon na Israel, akisisitiza kuwa harakati hiyo itaendelea kupambana hadi majeshi ya Israel yaondoke kikamilifu katika ardhi ya Lebanon.
-
Sheikh Naim Qassem: Kujisalimisha si chaguo; Hezbollah ina haki ya kulipiza kisasi kwa shambulio la Dahiyeh
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, ameonya kwamba kundi la mapambano lina haki ya kulipiza kisasi kutokana na kuuawa kwa kamanda mwandamizi Haitham Al-Tabtabai, na akasisitiza kuwa kujisalimisha si chaguo kabisa.
-
Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon: “Muhammad Afif alikuwa sura yenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari vya Muqawama”
Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya kumbukumbu ya mwaka wa kuuawa shahidi kwa Muhammad Afif al-Nabulsi na wenzake, alikumbusha nafasi muhimu ya marehemu katika uwanja wa vyombo vya habari na harakati za Muqawama. Alimtaja kama mfano wa kalamu yenye kujitolea, fikra angavu na uwajibikaji katika kutetea haki na mapambano ya wananchi wa ukanda huo.
-
Sheikh Naeem Qassem: Sisi ni watoto wa Imam Hussein (a.s) na hatuoni chaguo isipokuwa kuishi kwa heshima
Katibu Mkuu wa Hizbullah alipozungumza kwa ajili ya Siku ya Shahidi alisema: hatutaachana na silaha inayoitwawezesha kujitetea. Tumeachwa kwa shambulio na tutajilinda wenyewe.
-
Marasimu adhimu ya “Siku ya Shahidi” yafanyika Beirut
Sheikh Naeem Qassem: “Siku ya Shahidi si tu kwa ajili ya kuwakumbuka mashahidi, bali pia ni heshima kwa familia zao na wote wanaounga mkono njia ya mapambano ya muqawama.”
-
Katibu Mkuu wa Hezbollah: Damu ya mashahidi wa Yemen imechanganyika na damu ya Wapalestina katika njia ya Quds (Yerusalemu)
Katibu Mkuu wa Hezbollah Lebanon katika ujumbe rasmi kwa kiongozi wa Ansarullah Yemen, pamoja na kutoa rambirambi kwa kifo cha Rais wa Baraza Kuu la Jeshi la nchi hiyo, alithamini kujitolea kwake katika njia ya Quds na kupambana na maadui wa umma wa Kiislamu, na pia alimtakia mafanikio mrithi wake.