17 Novemba 2025 - 20:47
Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon: “Muhammad Afif alikuwa sura yenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari vya Muqawama”

Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya kumbukumbu ya mwaka wa kuuawa shahidi kwa Muhammad Afif al-Nabulsi na wenzake, alikumbusha nafasi muhimu ya marehemu katika uwanja wa vyombo vya habari na harakati za Muqawama. Alimtaja kama mfano wa kalamu yenye kujitolea, fikra angavu na uwajibikaji katika kutetea haki na mapambano ya wananchi wa ukanda huo.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA- Sheikh Naim Qassem, Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya maadhimisho ya kumbukumbu ya Shahada ya Muhammad Afif Al-Nablsi na wenzake, alisema: “Haj Muhammad Afif alikuwa na kalamu yenye nguvu katika uandishi na hotuba, na alikuwa na hazina kubwa ya elimu, uelewa mpana, mtazamo sahihi na msimamo ulionyooka.”

Aliendelea kusema kuwa: “Afif kwa zaidi ya miaka kumi alisimamia Idara ya Mawasiliano ya Habari chini ya usimamizi wa Bwana wa Mashahidi wa Ummah, Sayyid Hassan Nasrallah (Allah amwie radhi). Baada ya kuuawa shahidi kwa kiongozi huyo, Afif ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kupendekeza kuanzishwa kwa mikutano ya mara kwa mara na waandishi wa habari.”

Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah alisisitiza kuwa: “Haj Muhammad Afif alikuwa mwanahabari mwaminifu na mwenye dhamira; katika uwanja wa Kiislamu, kisiasa, na katika njia ya muqawama (mapambano ya ukombozi).”

Mwendelezo wa hotuba
Hotuba hii inaendelea, na taarifa kamili zitatumwa baadaye.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha