Hizbullah
-
Mazishi ya Kamanda Mwandamizi wa Muqawama wa Lebanon yamefanyika katika eneo la Dhahiya;
"Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Uongozi wa Hizbullah: Kwa kuuawa kwa maagenti wetu, azma yetu inazidi kuwa imara kuliko hapo kabla”
Sheikh Ali Damuush amesema: “Kulegeza msimamo au kukubali mashinikizo na maagizo ya Marekani na Israel hakutaleta matokeo yoyote. Sisi hatutasalimu amri; hata ikiwa maadui wataweka juhudi zao zote kutuangamiza, kamwe hatutaacha njia ya muqawama (mapambano) wala kujitoa katika kuilinda nchi yetu.”
-
Hizbullah: Ulegevu wa serikali ya Lebanon unaongeza ukatili wa Wazayuni
Hizbullah imesisitiza katika taarifa yake kwamba serikali ya Lebanon inapaswa kufahamu kuwa kila aina ya ulegevu, udhaifu au kujisalimisha mbele ya utawala wa Kizayuni kutawafanya waongeze ukatili na tamaa zao za kupindukia.
-
Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon: “Muhammad Afif alikuwa sura yenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari vya Muqawama”
Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya kumbukumbu ya mwaka wa kuuawa shahidi kwa Muhammad Afif al-Nabulsi na wenzake, alikumbusha nafasi muhimu ya marehemu katika uwanja wa vyombo vya habari na harakati za Muqawama. Alimtaja kama mfano wa kalamu yenye kujitolea, fikra angavu na uwajibikaji katika kutetea haki na mapambano ya wananchi wa ukanda huo.
-
Utawala wa Kizayuni: “Kabla ya kushambulia Iran, lazima kwanza kudhoofisha Hizbullah / Kaskazini lazima itulie ndipo iwezekane kuivamia Iran!”
Utawala wa Israel umekaza vitisho vyake kuhusu kuanzisha awamu mpya ya mapigano ya kijeshi dhidi ya Lebanon. Lengo lililotangazwa la operesheni hii ni kuzuia kujengwa upya kwa uwezo wa kijeshi wa Hizbullah na kulazimisha serikali ya Lebanon kutekeleza mpango wa kulivua silaha kundi hilo.
-
Lebanon Yakatishwa Tamaa na Msaada wa Kimataifa Dhidi ya Uvamizi wa Israel / Shinikizo Linaloongezeka la Kuilazimisha Hizbullah Kuweka Silaha Chini
Aoun: “Tumeziomba nchi rafiki za Lebanon zisaidie kuishinikiza Israel kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano, lakini hadi sasa hakuna matokeo chanya yaliyopatikana.”
-
Marasimu adhimu ya “Siku ya Shahidi” yafanyika Beirut
Sheikh Naeem Qassem: “Siku ya Shahidi si tu kwa ajili ya kuwakumbuka mashahidi, bali pia ni heshima kwa familia zao na wote wanaounga mkono njia ya mapambano ya muqawama.”
-
Sheikh Naeim Qassem: „Kwa mapigano ya aina ya Karbala, tutakabiliana na kuondolewa kwa silaha za harakati ya upinzani.“
Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, katika hotuba ya kumbukumbu ya mashahidi Sayyid Hassan Nasrallah na Sayyid Hashim Safiuddin, amesisitiza kuwa Hizbullah imesalia thabiti katika ahadi yake na itapinga vikali jaribio lolote la kuondoa silaha zake.
-
Mtazamo juu ya Septemba ya Umwagaji Damu Lebanon;Kuanzia Jinai za Pagers hadi Subira ya Kistratejia ya Hizbullah baada ya Shahidi “Sayyid wa Muqawama"
Siku hizi ni kumbukumbu ya jinai za kipekee za utawala wa Kizayuni nchini Lebanon – kuanzia milipuko ya pageri hadi mauaji ya makamanda waandamizi wa Hizbullah. Hivyo basi, Septemba ya mwaka uliopita kwa Wana-Lebanon imekuwa mwezi usiosahaulika
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa Lebanon katika mahojiano na ABNA:
"Baada ya kuondolewa kwa silaha za Hizbullah, hakuna dhamana ya kulinda Lebanon dhidi ya adui msaliti"
Adnan Mansour: Je, viongozi rasmi wa Lebanon wanaweza kusimama dhidi ya Marekani na kulinda maslahi ya Lebanon na hatari za kuondolewa kwa silaha? Nani atakayebaki Lebanon kupambana na uvamizi wa Israel? Je, jeshi la Lebanon linaweza kukabiliana na uvamizi peke yake? Kamwe.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah: Kama siyo Muqawama, Israel ingeingia Beirut / Kamwe hatutaweka silaha chini
Sheikh Qasim alieleza kuwa ramani ya njia ya baadaye ni: kufukuza adui kutoka ardhi ya Lebanon, kusimamisha uvamizi, kuwaachia huru wafungwa, kuanza upya ujenzi wa taifa na kisha kushughulika na mkakati wa ulinzi wa kitaifa.
-
Taarifa ya Hizbullah na Harakati ya Amal zinatoa wito wa mkusanyiko wa kuonyesha upinzani dhidi ya maamuzi ya serikali
Katika taarifa ya Hizbullah na Harakati ya Amal ilisemwa: 'Enyi wafanyakazi na wazalishaji wa Lebanon, tumekuwa wavumilivu kwa muda mrefu juu ya changamoto zinazolikumba taifa letu, na sasa umefika wakati wa kuonyesha msimamo wetu wa kitaifa kwa pamoja.' Wakaongeza: 'Tuna miadi ya kusimama kwa pamoja kama taifa, kuonyesha kupinga kwetu njia ya kujisalimisha na kutii bila masharti, na kulinda nguvu na uhuru wa Lebanon'.
-
Beirut - Wananchi wa Lebanon Wamiminika Mitaani Kuiunga Mkono Hizbullah na Mapambano ya Muqawama
Wakisambaza ujumbe wao kwa sauti na maandamano, wananchi hao wamesisitiza kuwa Hizbullah si tu harakati ya kijeshi, bali pia ni nguzo muhimu ya taifa katika ulinzi wa mipaka na heshima ya Lebanon. Kwao, wazo la kuondoa silaha za harakati hiyo ni sawa na kuiweka Lebanon mikononi mwa maadui wake.