Muqawama
-
Shinikizo la Marekani kwa Baghdad; Makundi ya Muqawama: Hatufutiki kisiasa
Chanzo cha karibu na makundi ya Muqawama kilisema: “Muqawama na al-Hashd al-Shaabi pamoja na washirika wao wana angalau viti 97 bungeni, na wao ni sehemu isiyotenganishwa na mlinganyo wa kisiasa wa Iraq. Washington ilishindwa hapo awali kuyadhibiti makundi ya muqawama, na leo pia haitafanikiwa kwa vitisho vya kidiplomasia.” Chanzo hicho kiliongeza: “Sharti letu ni wazi; Waziri Mkuu awe huru, asiye tegemezi kwa Marekani, na anayewakilisha vipengele vyote vya nyumba ya taifa ya Iraq.”
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Tasnia ya Madahi inapaswa kuwa kitovu cha fasihi ya Muqawama na ufafanuzi wa mafundisho ya dini na mapinduzi
Katika hotuba yake iliyochukua takriban saa tatu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliwapongeza Wairani kwa kuadhimisha kuzaliwa kwa Bibi Fatimah (a.s) na kusema kuwa “mwananchi wa Iran, kwa kupitia msimamo wa kitaifa wa kimapinduzi, ameshindwa kabisa njama za adui kutaka kubadilisha utambulisho wa kidini, kihistoria na kiutamaduni wa taifa hili.”
-
Ushindi wa Jukwaa la Upinzani (Muqawama) ni Kudhihirika kwa Utabiri wa Qur’an
Kushindwa kwa Israel na Marekani katika mapambano ya hivi karibuni kunatokana na uongozi wa busara wa Ayatullah Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Mchambuzi wa Kisiasa wa Lebanon:
Mkutano wa Kiuchumi na Wawakilishi wa Israel ni Uongo Mtupu na Vita vya Kisaikolojia / Muqawama Haitaruhusu Aina Yoyote ya Uhalalishaji wa Mahusiano
Katika mazungumzo yake na ABNA, Fadi Boudieh alisema kuwa bila shaka Israel inajaribu kuwapotosha baadhi ya Walebanoni, Waisraeli na hata baadhi ya nchi za Kiarabu, kwa kuwashawishi kuwa imefanikiwa kulazimisha hali mpya ya kiuchumi kwa Lebanon kwa kutumia nguvu, na kwamba chaguo la upinzani (Muqawama) limekwisha.
-
Aida Surour:
"Kielelezo cha Ushujaa na Subira ya Mama za Mashahidi/Riwaya ya Mama wa Mashahidi Wawili wa Lebanon, Kuanzia Malezi ya Kiashura hadi Subira ya Zaynab"
Mama wa mashahidi wawili wa Lebanon, katika mahojiano na ABNA, alisimulia uzoefu wake kama mama katika njia ya muqawama na uvumilivu aliokuwa nao baada ya kuwapoteza watoto wake. Pia aliwasihi mama na wake za mashahidi waendelee kufuata njia ya wapendwa wao na kushikamana na imani.
-
Jeshi la Lebanon liliwaruhusu waandishi wa habari kuingia katika vituo vya Hizbullah;
JKituo cha kihistoria cha Muqawama ambacho ukweli wake umejulikana baada ya kusitishwa kwa mapigano
Bonde la Zabqin, kutokana na muundo wake maalum wa kijiografia na umbali wa takribani kilomita 10 kutoka mpaka wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu, linachukuliwa kuwa mojawapo ya ngome kuu za Muqawama (Upinzani). Ni ngome ambayo vizazi mbalimbali vya wapiganaji wa Kipalestina na Wenyeji wa Lebanon wamekuwa wakikuwapo humo kwa miaka mingi.
-
Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon: “Muhammad Afif alikuwa sura yenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari vya Muqawama”
Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya kumbukumbu ya mwaka wa kuuawa shahidi kwa Muhammad Afif al-Nabulsi na wenzake, alikumbusha nafasi muhimu ya marehemu katika uwanja wa vyombo vya habari na harakati za Muqawama. Alimtaja kama mfano wa kalamu yenye kujitolea, fikra angavu na uwajibikaji katika kutetea haki na mapambano ya wananchi wa ukanda huo.
-
Majibu Makali ya Muqawama wa Iraq kwa Mjumbe wa Trump / Silaha za Muqawama Zimeleta Kujitolea Kukubwa Zaidi Ikiwemo Kufukuza Wavamizi
"Makundi ya Muqawama ni sehemu ya roho ya wananchi wa Iraq, na roho hiyo haiwezi kutenganishwa nao kwa uamuzi au matakwa ya wageni".
-
Katibu Mkuu wa Mtandao wa Uhuru wa Palestina nchini Indonesia (FPN) katika mahojiano na Shirika la Habari la AhlulBayt (ABNA):
"Msaada kwa Palestina unapaswa kuongozwa kwa ufanisi, kuandaliwa kwa umoja na kuongezwa mara kadhaa"
"Ni kweli kwamba usitishaji wa vita umewapa Wapalestina muda wa kupumua, lakini tunapaswa kuwa waangalifu dhidi ya mpango wa kibepari wa Trump. Haiwezekani Marekani - ambayo ni mshirika mkuu katika mauaji ya Wapalestina - kuwa msuluhishi wa haki. Katika mpango wa vipengele 20 wa Trump, hakuna popote palipotajwa uhuru wa Palestina.”
-
Maadhimisho ya Mwaka wa kwanza wa Shahada ya Sayyid Hassan Nasrallah yatafanyika Siku ya Alhamisi
Baraza la Kuratibu Tablighi la Kiislamu limetangaza katika taarifa yake kwamba maadhimisho ya mwaka wa kwanza wa kifo cha shahidi Sayyid Hassan Nasrallah yatafanyika Alhamisi, tarehe 02 Oktoba, 2025, katika nchi nzima, chini ya kauli mbiu kuu “Innā ‘ala al-‘Ahd”. Hafla kuu itafanyika saa 4:00 usiku katika Uwanja wa Ibada wa Imam Hussein (a.s) mjini Teheran.
-
Profesa kutoka Lebanon katika mahojiano na ABNA:
Jina la Nasrallah limehusishwa na usalama na uaminifu / Silaha za Hezbollah zitaendelea kuwa sehemu ya mlingano wa Lebanon na eneo la kikanda
Yeye (Sayyid Hassan Nasrallah) alihesabiwa kuwa alama ya heshima na mapambano kwa wote, na alikuwa mfano wa malengo ya sehemu kubwa ya wapiganaji wa muqawama wa Kishia ambao kwa vitendo walitaka kufikia mamlaka, uhuru, na kujitegemea kwa Lebanon.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain:
Kujiondoa kwenye njia ya Muqawama (Mapambano ya kupinga dhulma) ni sawa na fedheha na udhalili
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain alisisitiza kuwa kuacha njia ya Muqawama (mapambano dhidi ya wavamizi na dhulma) hakuzai chochote isipokuwa fedheha, udhalilishaji na utumwa.
-
Mtazamo juu ya Septemba ya Umwagaji Damu Lebanon;Kuanzia Jinai za Pagers hadi Subira ya Kistratejia ya Hizbullah baada ya Shahidi “Sayyid wa Muqawama"
Siku hizi ni kumbukumbu ya jinai za kipekee za utawala wa Kizayuni nchini Lebanon – kuanzia milipuko ya pageri hadi mauaji ya makamanda waandamizi wa Hizbullah. Hivyo basi, Septemba ya mwaka uliopita kwa Wana-Lebanon imekuwa mwezi usiosahaulika
-
Atlantic: Iran Yajenga Njia Mpya na Kuwapita Maadui Zake
Tabia ya ustahimilivu ya Iran na mhimili wa muqawama (mapambano ya upinzani) katika miongo iliyopita imeonyesha kuwa, licha ya mashinikizo na mashambulizi kutoka Marekani na utawala wa Kizayuni, Iran daima imeweza kujirekebisha kimkakati na kupata njia mpya za kukabiliana na changamoto.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah: Kama siyo Muqawama, Israel ingeingia Beirut / Kamwe hatutaweka silaha chini
Sheikh Qasim alieleza kuwa ramani ya njia ya baadaye ni: kufukuza adui kutoka ardhi ya Lebanon, kusimamisha uvamizi, kuwaachia huru wafungwa, kuanza upya ujenzi wa taifa na kisha kushughulika na mkakati wa ulinzi wa kitaifa.
-
Maandamano Makubwa ya Wenyeji Lebanon Kupinga Uamuzi wa Serikali wa Kuvunja Silaha za Muqawama
Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Lebanon wamefanya maandamano na mikutano ya hadhara kupinga uamuzi wa serikali wa kuhodhi na kuvunja silaha za vikosi vya Muqawama.