Muqawama
-
Muqawama wa Kiislamu Iraq: Jibu kwa Marekani Halitakwepeka Baada ya Arbaeen, Yatoa Onyo kwa Serikali ya Iraq
Muqawama wa Kiislamu nchini Iraq umetangaza kuwa utatoa jibu dhidi ya kile ulichokiita mashambulizi ya Marekani baada ya kumalizika kwa ibada za Arbaeen ya Imam Hussein (as), huku ukitoa muda kwa serikali ya Iraq hadi tarehe 23 Safar kuchukua msimamo kuhusu usalama na suala la silaha za makundi ya Muqawama.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah na Mashahidi Wenzake Waliugeuza Mche wa Muqawama Kuwa Mti Imara
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, amesema Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah na mashahidi wenzake waliugeuza mche wa Muqawama wa Kiislamu kuwa mti mkubwa na imara ulioipa Lebanon heshima na utukufu katika Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Hezbollah Yatuma Ujumbe wa Utii na Uungaji Mkono kwa Kiongozi Mkuu wa Iran
Hezbollah - Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon — imemtumia ujumbe Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ikimpongeza kwa kuuawa shahidi kwa baba yake, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na kutangaza kumpa kiapo cha utii pamoja na kuahidi kuendelea na njia ya muqawama, jihadi na kujitolea chini ya uongozi wake.
-
Upinzani wa Iraq Waunga Mkono Mkakati wa Yemen wa Kufunga Mlango wa Bab al-Mandab
Abu Alaa al-Wala’i: “Yemen ina haki ya kufunga Mlango wa Bab al-Mandab ili dunia isikie kwamba wananchi wa Yemen hawatakufa kimya.”
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mazishi ya Mamilioni ya “Mbeba Bendera wa Muqawama” Nchini Iraq Yamebadilisha Mizani ya Madola ya Kiburi
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, amewapongeza wananchi wa Iraq kwa kuandaa mazishi makubwa na ya kihistoria ya kiongozi shahidi wa Muqawama, akisisitiza kuwa ushiriki wa mamilioni ya wananchi wa Iran na Iraq umeonesha mshikamano wa kina na undugu wa mataifa hayo mawili na kuvuruga njama za maadui za kuleta mgawanyiko.
-
Vyombo vya Habari vya Kiarabu Vyaupa Uzito Ujumbe wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu; Vasisitiza Ulipizaji wa Damu na Kuendelea kwa Muqawama
Vyombo vya habari mashuhuri vya eneo hilo kutoka Lebanon, Iraq, Yemen, Palestina, Qatar na Saudi Arabia, vimeripoti kwa upana ujumbe wa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, uliotolewa baada ya kumalizika kwa ibada kubwa ya mazishi ya Kiongozi huyo aliyefariki akiwa shahidi. Vyombo hivyo vimeutaja ujumbe huo kuwa ni ishara ya kuanza kwa hatua mpya katika uongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu. Miongoni mwa mambo makuu yaliyoangaziwa katika taarifa hizo ni pamoja na kusifiwa kwa ushiriki wa kihistoria wa wananchi, uhusiano kati ya Mapinduzi ya Kiislamu na harakati ya Ashura, kuendelea kwa mbele ya Muqawama (upinzani dhidi ya dhuluma), pamoja na kusisitizwa kwa ulipizaji wa damu za mashahidi wa vita vya hivi karibuni.
-
Mamia ya Watunisia Waandaa Mazishi ya Mfano kwa Heshima ya Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Husseini Khamenei
Mamia ya wananchi wa Tunisia walifanya mazishi ya mfano kwa heshima ya Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Husseini Khamenei, wakithibitisha mshikamano wao na mhimili wa muqawama na kupinga kuhalalishwa kwa uhusiano na utawala wa Kizayuni.
-
Qalibaf: Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi nchini Iraq Yalikuwa Tamko la Kulipiza Damu Yake
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema mazishi ya kihistoria ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi nchini Iraq hayakuwa tukio la maombolezo pekee, bali yalikuwa tamko la kuendeleza njia yake na kulipiza damu yake.
-
Qalibaf: Amani ya kweli nchini Lebanon haiwezi kupatikana bila mchango wa Iran
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa amani ya kudumu nchini Lebanon inaweza kupatikana kupitia nafasi ya Iran, huku akisisitiza kuendelea kuunga mkono washirika wa Jamhuri ya Kiislamu katika Muqawama.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Vita vya Siku 40 Vilidhihirisha Umoja wa Kambi ya Muqawama na Nguvu ya Kitaifa ya Iran
Msemaji wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Mohammad Akrami-Nia, amesema kuwa vita vya siku 40 vilivyoitwa "Vita vya Ramadhani" vilionyesha mshikamano wa Kambi ya Muqawama, kuimarisha uwezo wa kijeshi wa Iran na kuthibitisha nafasi ya nchi hiyo katika mlinganyo wa usalama wa kikanda.
-
Sheikh Naim Qassem: Mpango wa Kuangamiza Iran na Muqawama Umeshindwa / Amani Itategemea Kusitishwa kwa Uvamizi na Kujiondoa kwa Adui
Katibu Mkuu wa Hezbollah amesema kuwa mpango wa kuangamiza Iran na muqawama umefeli, akisisitiza kuwa kusitishwa kwa mapigano lazima kuwe kwa masharti ya kusitishwa kabisa kwa uvamizi na kujiondoa kwa adui katika maeneo wanayoyakalia.
-
Mchambuzi: “Heiba ya Marekani Yaporomoka Mbele ya Muqawama; Ushindi Wake Ni kwa Serikali Tegemezi Pekee”
Dkt. Hassan al-Rassabi: “Marekani haijashinda dhidi ya mataifa ya Muqawama, bali imefanikiwa tu kwa serikali tegemezi; heba ya Washington imeporomoka kimkakati.”
-
Jenerali Ismail Qa'ani: Gaza pia ina “Tufani” yake; msidharau uwezo wa Muqawama
Kamanda wa Kikosi cha Quds katika Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Jenerali Ismail Qa'ani, ameonya kuwa Gaza pia ina uwezo mkubwa wa kujibu mashambulizi, akisema kuwa kupuuza maonyo ya Muqawama kunaweza kusababisha hasara kubwa zaidi.
-
Qalibaf: Muqawama wa Lebanon na Diplomasia ya Iran Vinahakikisha Uhuru na Uadilifu wa Ardhi ya Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema jihadi ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon pamoja na diplomasia madhubuti ya Iran vinahakikisha mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa maadui hawataweza kamwe kuitenga au kuisambaratisha nguzo yoyote ya Muqawama.
-
Iran Yatangaza Rasmi Kufikiwa kwa Rasimu ya Mwisho ya Makubaliano na Marekani; Ijumaa Kutia Saini
Iran imetangaza rasmi kwa mara ya kwanza kufikiwa kwa rasimu ya mwisho ya makubaliano na Marekani, huku Ijumaa ikitajwa kuwa siku ya kutiwa saini; wakati huo huo, wachambuzi wanaeleza kuwa usitishaji wa mapigano nchini Lebanon, endapo Israel itautekeleza, ni matokeo ya msimamo wa Iran wa kujumuisha suala la Lebanon katika makubaliano hayo na ustahimilivu wa Muqawama katika medani ya mapambano.
-
Makundi ya Muqawama Iraq Yalionya Serikali ya Mpito ya Syria Dhidi ya Ushirikiano na Marekani na Israel
Makundi ya Muqawama nchini Iraq yametoa onyo kali kwa serikali ya mpito ya Syria, yakisema kuwa ushirikiano wowote wa kijeshi au kiusalama na Marekani na Israel dhidi ya Hizbullah ya Lebanon utakabiliwa na jibu la kijeshi.
-
Qaani: Kuanzia Hormuz hadi Bab al-Mandab kutaundwa “ukanda mpya wa kiusalama wa Muqawama”
Kamanda wa Kikosi cha Quds katika Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ismail Qaani, amesema kuwa hatua za wakati muafaka na za “busara” zinazochukuliwa na Yemen zinaonyesha uimara na mshikamano wa mhimili wa Muqawama. Amesema pia kuwa, endapo kutahitajika, pande nyingine zinaweza kujiunga katika hatua hizo.
-
Mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi: Iran Ipo Mstari wa Mbele wa Mhimili wa Muqawama
Hujjatul-Islam Mohammad Taqi Vakilpour amesema Iran ipo mstari wa mbele wa mhimili wa muqawama pamoja na Lebanon, Palestina na Yemen, huku akisisitiza umuhimu wa umoja wa kitaifa, kuimarisha mfumo wa Kiislamu na kukabiliana na juhudi za maadui za kueneza migawanyiko ndani ya jamii.
-
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq: Wavamizi wa Marekani Lazima Waondoke
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq imesisitiza katika taarifa yake kwamba uwepo wa majeshi ya Marekani nchini Iraq ni aina ya uvamizi unaokiuka mamlaka ya taifa hilo, na imetaka kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani kutoka ardhi ya Iraq. “Wavamizi wanaendelea kukiuka anga la Iraq; iwe kupitia ndege zisizo na rubani (drones) au kwa kutumia ndege zao za kivita. Hatua hizi zinachukuliwa kuwa tishio kubwa kwa usalama, uthabiti na umoja wa ardhi ya nchi, na ni uvamizi wa wazi dhidi ya mamlaka na heshima ya dola ya Iraq.”
-
Upendo na Uaminifu Usio na Kikomo kwa Muqawama na Wilayat; Kumbukumbu ya Mashahidi Nasrallah na Safiyyu al-Din
Katika kumbukumbu ya mwaka wa kwanza wa mazishi ya mashahidi wa Hezbollah, Hassan Nasrallah na Hashim Safiyyu al-Din, Naim Qassem alisisitiza kuendelea kwa njia ya Muqawama na uaminifu (Wilayat) kwa Kiongozi Sayyid Ali Khamenei, akieleza kuwa Muqawama hauwezi kushindwa iwe kwa ushindi au kwa shahada.
-
Shinikizo la Marekani kwa Baghdad; Makundi ya Muqawama: Hatufutiki kisiasa
Chanzo cha karibu na makundi ya Muqawama kilisema: “Muqawama na al-Hashd al-Shaabi pamoja na washirika wao wana angalau viti 97 bungeni, na wao ni sehemu isiyotenganishwa na mlinganyo wa kisiasa wa Iraq. Washington ilishindwa hapo awali kuyadhibiti makundi ya muqawama, na leo pia haitafanikiwa kwa vitisho vya kidiplomasia.” Chanzo hicho kiliongeza: “Sharti letu ni wazi; Waziri Mkuu awe huru, asiye tegemezi kwa Marekani, na anayewakilisha vipengele vyote vya nyumba ya taifa ya Iraq.”
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Tasnia ya Madahi inapaswa kuwa kitovu cha fasihi ya Muqawama na ufafanuzi wa mafundisho ya dini na mapinduzi
Katika hotuba yake iliyochukua takriban saa tatu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliwapongeza Wairani kwa kuadhimisha kuzaliwa kwa Bibi Fatimah (a.s) na kusema kuwa “mwananchi wa Iran, kwa kupitia msimamo wa kitaifa wa kimapinduzi, ameshindwa kabisa njama za adui kutaka kubadilisha utambulisho wa kidini, kihistoria na kiutamaduni wa taifa hili.”
-
Ushindi wa Jukwaa la Upinzani (Muqawama) ni Kudhihirika kwa Utabiri wa Qur’an
Kushindwa kwa Israel na Marekani katika mapambano ya hivi karibuni kunatokana na uongozi wa busara wa Ayatullah Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Mchambuzi wa Kisiasa wa Lebanon:
Mkutano wa Kiuchumi na Wawakilishi wa Israel ni Uongo Mtupu na Vita vya Kisaikolojia / Muqawama Haitaruhusu Aina Yoyote ya Uhalalishaji wa Mahusiano
Katika mazungumzo yake na ABNA, Fadi Boudieh alisema kuwa bila shaka Israel inajaribu kuwapotosha baadhi ya Walebanoni, Waisraeli na hata baadhi ya nchi za Kiarabu, kwa kuwashawishi kuwa imefanikiwa kulazimisha hali mpya ya kiuchumi kwa Lebanon kwa kutumia nguvu, na kwamba chaguo la upinzani (Muqawama) limekwisha.
-
Aida Surour:
"Kielelezo cha Ushujaa na Subira ya Mama za Mashahidi/Riwaya ya Mama wa Mashahidi Wawili wa Lebanon, Kuanzia Malezi ya Kiashura hadi Subira ya Zaynab"
Mama wa mashahidi wawili wa Lebanon, katika mahojiano na ABNA, alisimulia uzoefu wake kama mama katika njia ya muqawama na uvumilivu aliokuwa nao baada ya kuwapoteza watoto wake. Pia aliwasihi mama na wake za mashahidi waendelee kufuata njia ya wapendwa wao na kushikamana na imani.
-
Jeshi la Lebanon liliwaruhusu waandishi wa habari kuingia katika vituo vya Hizbullah;
JKituo cha kihistoria cha Muqawama ambacho ukweli wake umejulikana baada ya kusitishwa kwa mapigano
Bonde la Zabqin, kutokana na muundo wake maalum wa kijiografia na umbali wa takribani kilomita 10 kutoka mpaka wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu, linachukuliwa kuwa mojawapo ya ngome kuu za Muqawama (Upinzani). Ni ngome ambayo vizazi mbalimbali vya wapiganaji wa Kipalestina na Wenyeji wa Lebanon wamekuwa wakikuwapo humo kwa miaka mingi.
-
Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon: “Muhammad Afif alikuwa sura yenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari vya Muqawama”
Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya kumbukumbu ya mwaka wa kuuawa shahidi kwa Muhammad Afif al-Nabulsi na wenzake, alikumbusha nafasi muhimu ya marehemu katika uwanja wa vyombo vya habari na harakati za Muqawama. Alimtaja kama mfano wa kalamu yenye kujitolea, fikra angavu na uwajibikaji katika kutetea haki na mapambano ya wananchi wa ukanda huo.
-
Majibu Makali ya Muqawama wa Iraq kwa Mjumbe wa Trump / Silaha za Muqawama Zimeleta Kujitolea Kukubwa Zaidi Ikiwemo Kufukuza Wavamizi
"Makundi ya Muqawama ni sehemu ya roho ya wananchi wa Iraq, na roho hiyo haiwezi kutenganishwa nao kwa uamuzi au matakwa ya wageni".
-
Katibu Mkuu wa Mtandao wa Uhuru wa Palestina nchini Indonesia (FPN) katika mahojiano na Shirika la Habari la AhlulBayt (ABNA):
"Msaada kwa Palestina unapaswa kuongozwa kwa ufanisi, kuandaliwa kwa umoja na kuongezwa mara kadhaa"
"Ni kweli kwamba usitishaji wa vita umewapa Wapalestina muda wa kupumua, lakini tunapaswa kuwa waangalifu dhidi ya mpango wa kibepari wa Trump. Haiwezekani Marekani - ambayo ni mshirika mkuu katika mauaji ya Wapalestina - kuwa msuluhishi wa haki. Katika mpango wa vipengele 20 wa Trump, hakuna popote palipotajwa uhuru wa Palestina.”