hezbollah
-
Hezbollah, Ansarullah na Iran Wampongeza Khalil Al-Hayya kwa Kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas
Hezbollah ya Lebanon, Ansarullah ya Yemen, Kata’ib Hezbollah ya Iraq pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran wametoa pongezi kwa Dkt. Khalil Al-Hayya kufuatia kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti mpya wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Hamas, wakisisitiza kuendelea kwa Mshikamano na Harakati ya Upinzani wa Palestina licha ya kuuawa kwa viongozi wake wakuu.
-
Macron: Hezbollah Ikabidhi Silaha Zake, Israel Iondoe Vikosi Vyake Lebanon
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesisitiza kuwa Hezbollah inapaswa kukabidhi silaha zake kwa mamlaka ya Lebanon, huku akitaka pia Israel iondoe vikosi vyake kutoka maeneo ya kusini mwa Lebanon ili kuimarisha amani na utulivu wa kudumu katika eneo hilo.
-
“Diplomasia ya Aya”: Aya za Qur'ani zilizosomwa katika marasimu ya mazishi ya Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Khamenei zavutia hisia za wengi
Katika marasimu ya kuuaga mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei (Quds Sirruh), uteuzi wa Aya za Qur'ani Tukufu zilizosomwa kwa kila ujumbe wa wageni waliotoa salamu za rambirambi ulivutia hisia za wengi, huku kila Aya ikionekana kubeba ujumbe maalumu wa kisiasa, kiitikadi na kiroho.
-
Kauli ya Sheikh Naim Qassem: Makubaliano ya Mfumo kati ya Lebanon na Israel ni “Fedheha na Kusaliti Mamlaka ya Taifa”
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
-
Kamanda Matokeo Qaani: Gaza “ina tufani”, atoa onyo kali kuhusu matokeo ya kisiasa na kijeshi
Kamanda wa Kikosi cha Quds, Esmail Qaani, ametoa onyo akisema “Gaza ina tufani” na kwamba kupuuza hali halisi ya uwanja wa mapambano na kuendeshwa na maamuzi ya kisiasa kunaweza kusababisha matokeo makubwa, akirejea pia uzoefu wa Hezbollah kama mfano wa tahadhari.
-
Iran Yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz; Yaanza Hatua za Kujibu Ukiukaji wa Makubaliano na Marekani na Israel
Khalil Nasrallah: Iran yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz kama hatua ya kwanza ya kujibu ukiukaji wa makubaliano unaodaiwa kufanywa na Marekani na Israel; sasa mpira uko kwa Donald Trump.
-
Sheikh Naïm Qassem: “Tumezaliwa huru kupinga dhulma, ukoloni na utegemezi; upinzani dhidi ya adui ni haki halali”
Sheikh Naim Qassem amesema kuwa wao wamezaliwa huru na wamechagua kwa makusudi kupinga dhulma, ukoloni na utegemezi wa kigeni, akisisitiza kuwa kujibu adui kwa silaha ni haki ya kujilinda, na kwamba kushikamana na kaulimbiu ya “Hussein ndiyo njia yetu” ni msingi wa kuendelea kwao katika mapambano na ushindi dhidi ya ukandamizaji.
-
Makubaliano ya Iran na Marekani Yazua Mabadiliko Mapya ya Kisiasa Mashariki ya Kati
Makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yameibua mabadiliko makubwa ya kisiasa Mashariki ya Kati, huku yakionekana kuwa ushindi wa diplomasia lakini yakizua mvutano mpya kuhusu Lebanon, Israel na mustakabali wa uhusiano wa Washington na Tel Aviv.
-
Hezbollah Yatangaza Mashambulizi 22 Dhidi ya Vikosi vya Israel Kusini mwa Lebanon
Hezbollah imesema imefanya operesheni 22 za kijeshi kwa kutumia makombora, ndege zisizo na rubani na mizinga dhidi ya vikosi vya Israel kusini mwa Lebanon, ikidai kuharibu magari ya kijeshi, kulenga vituo vya kijeshi na kulazimisha ndege ya Israel ya aina ya Hermes 450 kuondoka katika anga la Lebanon.
-
Netanyahu Awataka Raia wa Lebanon Kuungana na Israel Dhidi ya Hezbollah
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametoa wito kwa raia wa Lebanon kujitenga na Hezbollah, akidai kuwa kundi hilo limeishikilia nchi hiyo “mateka” na kusisitiza kuwa Israel haina uhasama na wananchi wa Lebanon.
-
Naim Qassem: Hezbollah Haitasalimisha Silaha na Itaendelea Kupambana Hadi Israel Iondoke Lebanon
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Naim Qassem, amesema Hezbollah haitasalimisha silaha zake wala kukubali makubaliano ya mazungumzo kati ya Lebanon na Israel, akisisitiza kuwa harakati hiyo itaendelea kupambana hadi majeshi ya Israel yaondoke kikamilifu katika ardhi ya Lebanon.
-
Robert Pape: Ujumbe wa Trump Unaonyesha Kuongezeka kwa Nguvu za Iran Kanda ya Mashariki ya Kati
Profesa Robert Pape amesema msimamo wa Iran wa kutokushiriki mazungumzo wakati mashambulizi dhidi ya Hezbollah yanaendelea umeonyesha uzito wa ushawishi wake wa kikanda, huku akionya kuhusu uwezekano wa kipindi kirefu cha ukosefu wa utulivu katika eneo hilo.
-
Iran Yatoa Onyo Kali kwa Walowezi wa Kaskazini mwa Israel Endapo Beirut Itashambuliwa
Iran imeonya kuwa kushambuliwa kwa vitongoji vya kusini mwa Beirut kutakabiliwa na majibu makali, huku ikiwataka walowezi wa Kaskazini mwa Israel kuondoka katika maeneo hayo kwa ajili ya usalama wao iwapo mashambulizi hayo yatatekelezwa.
-
Hezbollah Yaongeza Mashambulizi ya Droni, Makamanda wa Israel Walengwa Kusini mwa Lebanon
Hezbollah imeripotiwa kuanzisha kampeni ya kulenga makamanda waandamizi wa Israel kusini mwa Lebanon kwa kutumia droni za upelelezi na mashambulizi, huku ving’ora vya tahadhari vikisikika zaidi ya mara 25 kaskazini mwa Israel kutokana na makombora na droni zilizorushwa kutoka Lebanon.
-
Ripoti ya Channel 13: Israel Yaendelea Kupata Hasara Lebanon Bila Lengo la Wazi la Kijeshi
Televisheni ya Channel 13 ya Israel imeripoti kuwa jeshi la Israel linaendelea kupata hasara dhidi ya Hezbollah nchini Lebanon, huku changamoto za kijiografia na mgogoro wa kisiasa vikizidisha hali ngumu ya operesheni hiyo.
-
Israel Yakiri Kushindwa Kukabiliana na Droni za Muqawama wa Lebanon
Jeshi la Israel limekiri kuwepo kwa hitilafu katika mifumo yake ya onyo dhidi ya droni za FPV zinazotumiwa na Muqawama wa Hezbollah, huku ripoti zikieleza kuwa teknolojia mpya ya droni hizo zinazoongozwa kwa “fiber-optic” imeongeza hofu na changamoto kubwa kwa vikosi vya utawala huo katika medani za mapambano.
-
Onyo la Kataib Hezbollah Iraq kwa Marekani kuhusu Kuanzisha Vita katika Eneo
Kataib Hezbollah imeonya kuwa iwapo Marekani itaanzisha vita katika eneo hilo, itakabiliwa na hasara kubwa na vita vya muda mrefu, huku pia ikiutahadharisha utawala wa Kurdistan kuepuka kushirikiana na majeshi ya kigeni.
-
Israel Leo Iko Dhaifu, Iran Imebaki Imara – Sheikh Naeem Qasim
Sheikh Naeem Qasim na Katibu Mkuu wa Hezbollah wanasema kuwa Israel leo iko dhaifu kuliko hapo awali, huku Iran chini ya uongozi wa Imam Khamenei ikibaki imara, huru na thabiti. Mapinduzi ya Iran yameendeleza upinzani katika eneo kwa miaka 47 bila kutegemea Mashariki au Magharibi, na Jamhuri ya Kiislamu imefanikiwa katika mapambano yake, hasa dhidi ya uvamizi wa Israel.
-
Kituo cha 12 cha Israel: "Hezbollah ina wapiganaji 70,000 na mamia ya makombora, iko tayari kwa makabiliano na Israel"
Usiku uliopita, katika mwendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Lebanon, utawala huo ulianzisha mashambulizi ya anga katika maeneo mbalimbali ya Lebanon.
-
Uchambuzi wa New York Times;
Je, , Beirut inaweza kuipokonya silaha Hezbollah ifikapo mwishoni mwa mwaka 2025?
Wachambuzi wanaonya kuwa ikiwa Beirut itaharakisha zoezi la kuipokonya silaha bila kupata mafanikio sambamba kutoka kwa Israel - kama vile kusitishwa kwa mashambulizi ya anga- hatua hiyo inaweza kuimarisha nafasi ya kisiasa na kijamii ya Hezbollah. Hii ni kwa sababu Hezbollah si kundi la kijeshi pekee, bali pia ni chama cha kisiasa chenye ushawishi mpana.
-
Utawala wa Kizayuni: Hezbollah imerejesha uwezo wake wa kijeshi katika sehemu kubwa ya majimbo ya mapigano (Mapambano)
Maafisa wa Israel wametoa tahadhari kwamba Hezbollah, kwa msaada wa kifedha kutoka Iran, imefanikiwa kurejesha uwezo wake wa kijeshi na sasa inachukuliwa kuwa tishio la kimkakati kwa Tel Aviv.
-
Sheikh Naim Qassem:
Lebanon inapaswa kukabiliana kikamilifu na uvamizi wa kibeberu wa utawala wa Kizayuni | Mashahidi walijitolea kwa roho, mali na kila walichokuwa nacho
Lebanon inakabiliwa na uvamizi hatari wa Kizayuni: Akirejea mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel kusini mwa Lebanon, alisema: “Lebanon inakabiliwa na uvamizi wa hatari na wa kupanua mipaka wa utawala wa Kizayuni. Lazima tukabiliane nao kwa kila njia na mbinu. Adui huyu haheshimu makubaliano yoyote.”
-
Marekani na Israel wanaandaa / Wanatengeneza simulizi (riwaya) mpya ili kuongeza shinikizo dhidi ya Hezbollah na Lebanon
Israel, kwa msaada wa Marekani, inajaribu kutengeneza mazingira ya kuanzisha vita na kuongeza mashinikizo dhidi ya Lebanon, kwa kutishia kulazimisha Hezbollah ivuliwe silaha kufikia mwisho wa mwaka.
-
Sheikh Naim Qassem: Kujisalimisha si chaguo; Hezbollah ina haki ya kulipiza kisasi kwa shambulio la Dahiyeh
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, ameonya kwamba kundi la mapambano lina haki ya kulipiza kisasi kutokana na kuuawa kwa kamanda mwandamizi Haitham Al-Tabtabai, na akasisitiza kuwa kujisalimisha si chaguo kabisa.
-
Vyombo vya Habari vya Israel: Kuongezeka kwa Nguvu ya Iran na Muungano wa Muqawama “Kunatia Wasiwasi”
Maafisa wa Idara ya ujasusi ya Israel walisema kuwa endapo mzozo mpya baina ya Iran na Israel utazuka, basi kisasi cha Iran kitaifanya Israel ikabiliwe na hatari kubwa zaidi kuliko ile iliyoshuhudiwa katika tukio lililopita.
-
Hizbullah Yatangaza Kuuawa Shahidi kwa Kamanda Wake Mwandamizi, Abu Ali Tabatabai
Hizbullah ya Lebanon imetangaza kwamba mmoja wa makamanda wake mashuhuri, Haitham Tabatabai (Abu Ali), ameuliwa shahidi katika shambulio la anga lililofanywa leo na Israel.
-
Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon: “Muhammad Afif alikuwa sura yenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari vya Muqawama”
Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hezbollah nchini Lebanon, katika hotuba yake ya kumbukumbu ya mwaka wa kuuawa shahidi kwa Muhammad Afif al-Nabulsi na wenzake, alikumbusha nafasi muhimu ya marehemu katika uwanja wa vyombo vya habari na harakati za Muqawama. Alimtaja kama mfano wa kalamu yenye kujitolea, fikra angavu na uwajibikaji katika kutetea haki na mapambano ya wananchi wa ukanda huo.
-
Sheikh Naeem Qassem: Sisi ni watoto wa Imam Hussein (a.s) na hatuoni chaguo isipokuwa kuishi kwa heshima
Katibu Mkuu wa Hizbullah alipozungumza kwa ajili ya Siku ya Shahidi alisema: hatutaachana na silaha inayoitwawezesha kujitetea. Tumeachwa kwa shambulio na tutajilinda wenyewe.
-
Lebanon Yakatishwa Tamaa na Msaada wa Kimataifa Dhidi ya Uvamizi wa Israel / Shinikizo Linaloongezeka la Kuilazimisha Hizbullah Kuweka Silaha Chini
Aoun: “Tumeziomba nchi rafiki za Lebanon zisaidie kuishinikiza Israel kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano, lakini hadi sasa hakuna matokeo chanya yaliyopatikana.”
-
Onyo la jarida la The National Interest kuhusu kuibuka kwa “Hezbollah Mpya” Katika Eneo
Jarida la Marekani “The National Interest” katika makala yake ya uchambuzi limeonesha shaka kuhusu mafanikio ya mpango wa Donald Trump wa kuleta uthabiti wa kudumu katika Ukanda wa Gaza, na limeonya kuwa mpango huo unaweza kuchangia kuibuka kwa taasisi au kundi jipya linalofanana na Hezbollah katika eneo hilo.