22 Machi 2025 - 17:08
Watu 2 wameuawa Shahidi na wengine 10 kujeruhiwa kutokana na Mashambulizi ya utawala wa Kizayuni huko Kusini mwa Lebanon

Watu 2 wameuawa Shahidi na watu 10 wamejeruhiwa kutokana na mvutano uliozuka tena Kusini mwa Lebanon na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni katika eneo la Tolin.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahl al-Bayt (a.s) - Abna -; Watu wawili wameuawa Shahidi na watu 10 wamejeruhiwa kufuatia mashambulizi ya utawala wa Kizayuni katika eneo la Tolin Kusini mwa Lebanon.

Kwa mujibu wa ripoti ya al-Hadath, na kwa upande mwingine, gazeti la Yediot Ahronot liliripoti kwamba milipuko mikali ilisikika katikati mwa Israel.

Redio ya Jeshi la Kizayuni pia imeripoti kuwa, mashambulizi ya Israel katika eneo la Kusini mwa Lebanon bado yanaendelea.

Chanzo cha kijeshi cha Lebanon pia kimesema kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa roketi zilizorushwa kuelekea maeneo yanayokaliwa kwa mabavu zilikuwa za aina ya zamani.

Aidha, alitangaza uratibu kamili wa Jeshi la Lebanon na vikosi vya UNIFIL kufuatilia maendeleo katika uwanja huo.

Wakati huo huo vyombo vya habari vya Lebanon vilitangaza kuwa, Hezbollah ya Lebanon ilimuarifu Rais na Waziri Mkuu wa Lebanon kwamba wanatafuta na kufuatilia usitishaji vita.

Jeshi la Kizayuni pia limetangaza shambulio hilo dhidi ya majukwaa ya kurusha makombora na makao makuu ya amri ya operesheni ya Hezbollah ya Kusini mwa Lebanon.

Jeshi hilo limeongeza kuwa vikosi vya Hezbollah vya Lebanon vilikuwepo katika maeneo yaliyolengwa.

Ikumbukwe kuwa kutokana na mashambulizi ya makombora kutoka Lebanon katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na jibu la haraka la utawala wa Kizayuni dhidi ya shambulio hilo, linaifanya hali ya mipaka ya Kusini mwa Lebanon kuwa ya wasiwasi kwa mara nyingine tena.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha