Siku
-
Mazungumzo ya ngazi ya pili yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani imeendelea Siku ya Jumanne huko Geneva, Uswisi
Raundi ya pili ya mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani imefanyika Siku ya Jumanne katika Ubalozi wa Oman uliopo mjini Geneva, Uswisi. Mazungumzo haya yanafanyika katika hali ambayo bado kuna ukosefu wa imani, unaotokana na kile kinachoelezwa kuwa ni misimamo na tabia zinazokinzana kutoka upande wa Washington—hali ambayo inaendelea kuwa moja ya changamoto kuu katika mchakato huu wa mazungumzo.
-
Maandamano Yatikisa Marekani, Minneapolis Kituo Kikuu cha Upinzani Dhidi ya ICE
Wimbi la maandamano linaendelea kuitikisa Marekani, huku jiji la Minneapolis likiwa miongoni mwa vituo vikuu vya upinzani dhidi ya operesheni za polisi wa uhamiaji (ICE). Maelfu ya raia wameingia mitaani wakipinga matumizi ya nguvu kupita kiasi, na maandamano yamesambaa hadi miji mingine kama Portland, Maine, San Francisco na Washington DC. Serikali iko chini ya shinikizo kubwa la ndani, huku wananchi wakidai haki, uwazi na kuheshimiwa kwa utu wa raia.
-
Sayyid Khamenei: Kiongozi Aliyesimama Kidete Dhidi ya Ubeberu wa Kimataifa
Baada ya hatua thabiti na za kishujaa za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran dhidi ya kambi za kijeshi za Israel na Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, dunia iliamka asubuhi ikiwa inazungumzia wasifu mpya wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei—kiongozi wa kiroho aliyeonesha ujasiri, busara na msimamo usiotetereka mbele ya madola ya kibeberu.
-
Mazungumzo kati ya Taliban na Pakistan mjini Istanbul yaingia siku ya tatu
Zabihullah Mujahid, msemaji wa Taliban, leo asubuhi (Jumatatu, tarehe 27 Oktoba 2025) amesema kuwa mazungumzo kati ya ujumbe wa Afghanistan na ule wa Pakistan yanaendelea mjini Istanbul, Uturuki, kwa siku ya tatu mfululizo.