Waombolezaji
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei, Atoa Tamko Maalumu Kufuatia Mazishi ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khame
Katika tamko lake kufuatia mazishi makubwa ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei, amesisitiza kuendelezwa kwa njia ya Imam Husayn (a.s.), kulinda urithi wa Mapinduzi ya Kiislamu, na kuendelea kudai haki kwa damu za mashahidi.
-
Iraq Yaandaa Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)
Marasimu ya kihistoria ya mazishi ya mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Hussein Khamenei, pamoja na mashahidi wa familia yake, yanafanyika leo nchini Iraq kwa ushiriki wa maelfu ya waombolezaji.
-
Hilali Nyekundu: Hakuna Majeruhi Walioripotiwa Katika Hafla ya Kuaga Kiongozi Shahidi Licha ya Mamilioni ya Waombolezaji Kushiriki
Shirika la Hilali Nyekundu limetangaza kuwa hadi sasa hakuna majeruhi walioripotiwa katika hafla ya kuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, licha ya mamilioni ya waombolezaji kushiriki. Shirika hilo limeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa tukio hilo pamoja na ushirikiano wa wananchi.
-
Sala ya maiti ya Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei na familia yake kufanyika Jumapili asubuhi mjini Tehran
Kamati ya Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu imetangaza kuwa sala ya maiti ya Ayatullah al-Udhma Sayyid Ali Khamenei (r.a.) pamoja na baadhi ya wanafamilia wake na mashahidi wengine itafanyika Jumapili saa 12:00 asubuhi kwa saa za Iran katika Msala wa Tehran.
-
Wizara ya Ulinzi Iran Yatangaza Kusambaza Rasilimali Zake Kusaidia Waombolezaji wa Kiongozi Shahidi
Kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Iran, Brigedia Jenerali Tala'inik, wizara hiyo imehamasisha uwezo wake wote katika miji ya Tehran, Qom na Mashhad ili kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi wanaoshiriki shughuli za mazishi ya kiongozi shahidi, ikiwemo huduma za kitabibu, kitamaduni na msaada wa kiutendaji.
-
Mamilioni ya Wairaq Kuitikia Wito wa Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi
Takribani Wairaq milioni moja wanatarajiwa kushiriki mazishi ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi, huku zaidi ya nusu milioni wakitarajiwa kuingia Iran kupitia mpaka wa Mehran kuelekea Tehran, Qum na Mashhad kwa ajili ya maombolezo.
-
Kenya yaomboleza kifo cha Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga | Aagwa kwa Heshima Bungeni
Kifo cha Raila kimeacha pengo kubwa katika historia ya kisiasa ya Kenya, na atakumbukwa kama shujaa wa mageuzi na demokrasia nchini humo.
-
Mawakibu (1,800) za waombolezaji yalifurika katika Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) kwa Mnasaba wa kumbukumbu ya kufariki kwa Mtukufu Mtume Muhammad (s)
Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) Yapokea Makundi 1800 ya Waombolezaji Kutoka Ndani na Nje ya Iraq kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s.a.w.w).
-
Katibu Mkuu wa Baraza la Maimamu wa Kishia Pakistan:
Kukandamiza waombolezaji wa Imam Hussein (a.s) Punjab ni kitendo cha woga na kinyume na haki za kiraia
Katibu Mkuu wa Baraza la Maimamu wa Kishia nchini Pakistan, Hujjatul-Islam Shabir Hassan Meesami, amelielezea hatua ya Serikali ya Punjab ya kuwashughulikia kwa nguvu waombolezaji wa Imam Hussein (a.s) na kufungua kesi za kisheria dhidi yao kuwa ni kitendo cha woga, akitaka kusitishwa mara moja kwa kukamatwa kiholela na kuachiliwa kwa wote waliokamatwa.