Waziri wa Mambo ya Nje
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kishia Lebanon Beirut
Wakati wa ziara yake rasmi mjini Beirut, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyyed Abbas Araghchi, alikutana na Sheikh Ali Al-Khatib, Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Kishia nchini Lebanon. Mazungumzo yao yalijikita katika maendeleo ya kikanda, umuhimu wa umoja wa Kiislamu, na kuimarisha ushirikiano wa kidini na kisiasa kwa ajili ya uthabiti na mshikamano wa Lebanon.
-
Araqchi: Umoja wa ardhi na mamlaka ya Yemen lazima vilindwe
Katika mazingira ya kuongezeka kwa mvutano wa kisiasa na kijeshi nchini Yemen, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi, amesisitiza ulazima wa kulindwa umoja wa ardhi na mamlaka ya kujitawala ya nchi hiyo, akionya dhidi ya madhara ya mgawanyiko na kuingilia masuala ya ndani. Kauli hiyo imetolewa kupitia mazungumzo ya simu na mawaziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu, huku pia akigusia hali ya usalama nchini Yemen na kulaani uchokozi unaoendelea wa Israel dhidi ya Lebanon.
-
Ufichuzi wa mtandao wa Kizayuni:
Israel imekubali kuitambua Somaliland kwa masharti ya kukubali kuwapokea wakazi wa Gaza!
Jana, Benjamin Netanyahu, Gideon Sa’ar Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni, pamoja na Abdirahman Mohamed Abdullahi, rais wa kujitangaza wa Somaliland, walitia saini tamko la pamoja la kuitambua Somaliland kama nchi huru na inayojitegemea.
-
Araqchi: Marekani Haitaki Diplomasia ya Kweli, Bali Kulazimisha Iran Kunyimwa Haki Zake
Araqchi: "Diplomasia ya kweli haiwezi kujengwa juu ya mashinikizo na masharti ya upande mmoja. Kuitaka Iran iachane na haki zake halali si mazungumzo, bali ni jaribio la kulazimisha,”
-
Araghchi:
Balozi Mkuu wa Iran katika Van utafunguliwa / Chanzo kikubwa zaidi cha tishio kwa Syria ni kutoka kwa utawala wa Kizayuni
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alisema: Iran na Uturuki si tu nchi jirani, bali ni nchi mbili rafiki na ndugu zenye ushirikiano mkubwa sana.
-
Iran yashuku ujumbe wa Netanyahu kuhusu kutoshambulia tena
"Vikosi vya ulinzi vya Iran vipo katika hali ya tahadhari ya juu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa hila kutoka Israel, na hatuamini nia hizi".
-
Iran: Hatuna Imani na Israel Kuheshimu Usitishaji Mapigano Gaza / Mkataba wa Amani wa Abraham ni Usaliti Mkubwa – Araghchi
“Kila mara Israel inaposhindwa kijeshi au inapokabiliwa na shinikizo la kimataifa, hukubali makubaliano ya muda tu ili kupata nafasi ya kujipanga upya na kuendeleza mashambulizi mapya. Hivyo, amani ya kweli haiwezi kupatikana kwa kutegemea ahadi zake.”
-
Misri: Cairo haitaruhusu uhamishaji wa wakaazi wa Gaza
Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri alitangaza kwamba nchi yake haitaruhusu uhamishaji wa wakaazi wa Gaza kwa hali yoyote, kwa sababu hatua hiyo itakuwa sawa na kufutwa kwa suala la Palestina.