Waziri wa Mambo ya Nje
-
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje kuhusu kuongezeka kwa mvutano kati ya Pakistan na Afghanistan
Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ikieleza wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa mvutano kati ya Pakistan na Afghanistan. Iran imezitaka pande zote mbili kuanza mazungumzo ya haraka ili kusitisha mapigano, kuheshimu mamlaka na mipaka ya kila nchi, na kuepuka hatua zinazoweza kuongeza hali ya taharuki. Pia imetangaza utayari wake kusaidia juhudi za kupunguza mvutano na kufanikisha maelewano ya amani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema makubaliano na Marekani yako “karibu kufikiwa”; Trump asema anapendelea diplomasia
Abbas Araghchi amesema makubaliano na Marekani yako karibu kufikiwa ikiwa diplomasia itapewa kipaumbele, huku Donald Trump akisisitiza kuwa anapendelea mazungumzo badala ya vita.
-
Abbas Araghchi: Makubaliano yako karibu iwapo diplomasia itapewa kipaumbele
Abbas Araghchi amesema kuwa makubaliano kati ya Iran na Marekani yako ndani ya mfukoni iwapo diplomasia itapewa kipaumbele, akisisitiza kuwa Iran haitafuti silaha za nyuklia lakini haitarudi nyuma katika haki yake ya teknolojia ya amani ya nyuklia.
-
Marco Rubio, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema kuwa kufikia makubaliano na Iran ni “jambo gumu sana”
Marco Rubio, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, siku ya Jumamosi alithibitisha kuwa Donald Trump, Rais wa nchi hiyo, anapendelea kufikia makubaliano na Iran. Hata hivyo, alikiri kuwa kufikia makubaliano hayo ni “jambo gumu sana.” Aidha, alisisitiza kuwa Marekani haitarudi nyuma katika ahadi yake ya kumaliza vita vya Ukraine.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela Aipongeza Iran kwa Miaka 47 ya Mapinduzi ya Kiislamu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela, Ivan Gil Pinto, amempongeza Iran kwa maadhimisho ya miaka 47 ya Mapinduzi ya Kiislamu, akisisitiza udugu na mshikamano wa nchi hizo mbili na kuthibitisha dhamira ya kuimarisha ushirikiano wa pamoja kwa ajili ya dunia ya pande nyingi, haki ya kijamii na amani ya mataifa.
-
Araghchi na Takht-Ravanchi Wakagua Nyaraka Muhimu Kabla ya Mazungumzo ya Nyuklia Iran–Marekani Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyyed Abbas Araghchi, pamoja na Naibu wake Majid Takht-Ravanchi, wameonekana wakipitia nyaraka muhimu kabla ya kuanza kwa mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani mjini Muscat, Oman.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi Aongoza Ujumbe wa Mazungumzo na Marekani Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameongozana na ujumbe wake wa kidiplomasia kuelekea mjini Muscat, Oman, kwa ajili ya mazungumzo na Marekani. Mazungumzo hayo yanatazamwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kujadili masuala ya nyuklia, vikwazo vya kiuchumi na usalama wa kikanda, kwa lengo la kufungua ukurasa mpya wa maelewano ya kisiasa.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kishia Lebanon Beirut
Wakati wa ziara yake rasmi mjini Beirut, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyyed Abbas Araghchi, alikutana na Sheikh Ali Al-Khatib, Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Kishia nchini Lebanon. Mazungumzo yao yalijikita katika maendeleo ya kikanda, umuhimu wa umoja wa Kiislamu, na kuimarisha ushirikiano wa kidini na kisiasa kwa ajili ya uthabiti na mshikamano wa Lebanon.
-
Araqchi: Umoja wa ardhi na mamlaka ya Yemen lazima vilindwe
Katika mazingira ya kuongezeka kwa mvutano wa kisiasa na kijeshi nchini Yemen, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi, amesisitiza ulazima wa kulindwa umoja wa ardhi na mamlaka ya kujitawala ya nchi hiyo, akionya dhidi ya madhara ya mgawanyiko na kuingilia masuala ya ndani. Kauli hiyo imetolewa kupitia mazungumzo ya simu na mawaziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu, huku pia akigusia hali ya usalama nchini Yemen na kulaani uchokozi unaoendelea wa Israel dhidi ya Lebanon.
-
Ufichuzi wa mtandao wa Kizayuni:
Israel imekubali kuitambua Somaliland kwa masharti ya kukubali kuwapokea wakazi wa Gaza!
Jana, Benjamin Netanyahu, Gideon Sa’ar Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni, pamoja na Abdirahman Mohamed Abdullahi, rais wa kujitangaza wa Somaliland, walitia saini tamko la pamoja la kuitambua Somaliland kama nchi huru na inayojitegemea.
-
Araqchi: Marekani Haitaki Diplomasia ya Kweli, Bali Kulazimisha Iran Kunyimwa Haki Zake
Araqchi: "Diplomasia ya kweli haiwezi kujengwa juu ya mashinikizo na masharti ya upande mmoja. Kuitaka Iran iachane na haki zake halali si mazungumzo, bali ni jaribio la kulazimisha,”
-
Araghchi:
Balozi Mkuu wa Iran katika Van utafunguliwa / Chanzo kikubwa zaidi cha tishio kwa Syria ni kutoka kwa utawala wa Kizayuni
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alisema: Iran na Uturuki si tu nchi jirani, bali ni nchi mbili rafiki na ndugu zenye ushirikiano mkubwa sana.
-
Iran yashuku ujumbe wa Netanyahu kuhusu kutoshambulia tena
"Vikosi vya ulinzi vya Iran vipo katika hali ya tahadhari ya juu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa hila kutoka Israel, na hatuamini nia hizi".
-
Iran: Hatuna Imani na Israel Kuheshimu Usitishaji Mapigano Gaza / Mkataba wa Amani wa Abraham ni Usaliti Mkubwa – Araghchi
“Kila mara Israel inaposhindwa kijeshi au inapokabiliwa na shinikizo la kimataifa, hukubali makubaliano ya muda tu ili kupata nafasi ya kujipanga upya na kuendeleza mashambulizi mapya. Hivyo, amani ya kweli haiwezi kupatikana kwa kutegemea ahadi zake.”
-
Misri: Cairo haitaruhusu uhamishaji wa wakaazi wa Gaza
Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri alitangaza kwamba nchi yake haitaruhusu uhamishaji wa wakaazi wa Gaza kwa hali yoyote, kwa sababu hatua hiyo itakuwa sawa na kufutwa kwa suala la Palestina.