Tarehe 11 Februari 2026, maelfu ya Wairani walikusanyika kuonyesha mshikamano wao na taifa na kuthibitisha kwamba Marekani ni adui wa Umma wa Kiislamu.
Tukio hili linaonyesha wazi kwamba mbinu za adui hazina nafasi mbele ya mshikamano wa wananchi wa Iran na jitihada za kuharibu taifa hilo hazina mafanikio.
Hashd Al-Shaabi ya Iraq imefanikiwa kugundua na kuharibu handaki na maficho ya ISIS Mashariki mwa Salahuddin kwa kushirikiana na jeshi la Iraq, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuzuia kurejea kwa makundi ya kigaidi katika eneo hilo.
Mkuu wa Mahusiano ya Kigeni na Mjumbe wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesisitiza umuhimu wa kuhifadhi umoja wa Kiislamu na kufuata mafundisho ya Mtume Mtukufu Muhammad (s.a.w.w) kuhusu huruma na uongofu, akieleza juu ya juhudi endelevu za maadui katika kuharibu sura ya Uislamu.