Zabihullah Mujahid, msemaji wa Taliban, leo asubuhi (Jumatatu, tarehe 27 Oktoba 2025) amesema kuwa mazungumzo kati ya ujumbe wa Afghanistan na ule wa Pakistan yanaendelea mjini Istanbul, Uturuki, kwa siku ya tatu mfululizo.
Kauli hiyo imetolewa katika ujumbe wake maalum kwa mnasaba wa Wiki ya Kuheshimu Ulinzi Usio wa Kijeshi, ambapo amesema kuwa kipindi hiki ni fursa muhimu ya kueleza umuhimu wa mikakati na mipango ya kuongeza usalama, uimara, na kinga ya miundombinu ya taifa dhidi ya kila aina ya vitisho vya maadui.