mrengo
-
Salvador Nasrallah; mgombea wa Liberal wa Honduras akikabiliana na Moncada / Ushirikisho wa Trump ukisaidia Asfura, mgombea wa mrengo wa kulia
Zaidi ya raia milioni 6.5 wa Honduras watapiga kura Jumapili hii kuamua kama mradi wa kisiasa wa mrengo wa kushoto wa Rais Xiomara Castro na mgombea wake, Rexy Moncada, utaendelea au la, au kama shinikizo la Donald Trump litaweza kumsaidia Nasry Asfura, mgombea wa mrengo wa kulia, kufanikisha ushindi.
-
Mwanasiasa wa mrengo wa kulia nchini Marekani afungua kesi kwa sababu polisi hawakumuunga mkono katika kitendo cha kuchoma Qur’ani!
Jake Lang, mgombea wa chama cha Republican katika uchaguzi wa Seneti ya Florida na mmoja wa wafuasi wakubwa wa Trump, baada ya kushindwa kutekeleza kitendo cha kuchoma Qur’ani huko Dearborn, jimbo la Michigan, na kuingia katika makabiliano na waandamanaji, amewasilisha kesi ya dola milioni 200 akimshutumu Meya Mwislamu wa jiji hilo na polisi wa eneo hilo kwa “kutompa ulinzi.” Hapo awali, picha zilizochukuliwa na waandishi wa habari huru na vyombo kama Reuters na Anadolu zilionyesha kwamba Lang alijaribu kuchoma nakala ya Qur’ani kwa kutumia kimiminika cha kuwasha moto, lakini alikabiliwa mara moja na mpinga-maandamano aliyemtibua kabla ya kufanya kitendo hicho.
-
Mwanazuoni wa Kireno atoa ukosoaji mkali kuhusu sheria ya kupiga marufuku burqa
Kupitishwa kwa sheria ya kupiga marufuku burqa nchini Ureno - iliyotetewa kwa kisingizio cha “kulinda usalama na haki za wanawake” - kumezua upinzani kutoka kwa wanaharakati kadhaa. Miongoni mwa wakosoaji hao ni Paulo Mendes Pinto, mtafiti wa masuala ya dini nchini humo, ambaye katika mahojiano na chombo cha habari cha ndani ametoa maoni ya kuvutia kuhusu suala hilo.
-
Televisheni yenye kufuata mrengo wa Kizayuni "Iran International" imeanguka, na sasa BBC imechukua nafasi yake
Katika dunia ya sasa, ni vigumu kujua ukweli kamili kwa urahisi, hivyo ni muhimu kuwa na vyombo vya habari vya kuaminika vinavyotumia vyanzo vya haki na kuthibitisha taarifa kabla ya kuzisambaza. Hivyo ndio Vyombo vya kufuatilia na kusikiliza. Na sio kufuata kila chombo cha Habari bila kujua kuwa hiki chombo kinatumiwa na waovu wa uistikbari wa Dunia au la.