Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA-: Bunge la Ureno, kwa pendekezo la chama cha mrengo wa kulia cha “Chega”, limepitisha sheria inayokataza kuvaa burqa katika maeneo ya umma. Sheria hiyo imeelezwa kuwa inalenga “kulinda haki za wanawake na usalama wa taifa,” lakini Mendes Pinto anasema lengo halisi ni kueneza chuki na unyanyapaa dhidi ya Waislamu.
Katika mahojiano na shirika la habari Lusa, Mendes Pinto alisisitiza kwamba sheria hiyo itachochea zaidi Uislamuophobia na kuunda picha hasi kuhusu wahamiaji nchini Ureno, akibainisha kuwa idadi ya wanawake wanaovaa burqa ni ndogo sana. Amesema kuwa kuvaa burqa si wajibu wa kidini katika Uislamu, bali ni tamaduni za kijamii katika baadhi ya maeneo duniani, na hivyo haiwezi kuhusishwa na Waislamu wote.
Mtafiti huyo amependekeza badala ya kutunga sheria za vizuizi, serikali iwaamishe viongozi wa dini na maimamu kushiriki katika elimu ya kijamii na kuhimiza heshima, utu na ushiriki wa wanawake katika jamii. Kwa maoni yake, njia hii ni yenye manufaa zaidi kuliko marufuku ya kisheria, na inaweza kuimarisha umoja, amani, na kuheshimiana kati ya wananchi.
Your Comment