Wanawake
-
Utafiti Mpya: Wanawake Waislamu Wakabiliwa na Kiwango Kikubwa cha Kutokuwa Salama Katika Usafiri wa Umma Uingereza
Kwa mujibu wa matokeo ya uchunguzi mpya, wanawake Waislamu nchini Uingereza wanakabiliana na hisia kubwa ya kutokuwa salama na viwango vya juu vya unyanyasaji katika mitandao ya usafiri wa umma. Ripoti inaonyesha kuwa wengi wao hulazimika kubadili mwenendo wao wa safari kutokana na hofu ya usalama wa kibinafsi—ikiwemo kuepuka kusafiri nyakati fulani, kubadilisha mavazi yao, au kutumia teksi kwa gharama zao wenyewe.
-
Majlis ya Kuhuisha Shahada ya Sayyidat Fatima Al-Zahra (sa) kwa Akina Mama Jijini Dar es Salaam +Picha
Katika khutba yake, Sheikh Ja'far Mwazoa alieleza kwa ufafanuzi wa kina fadhila zake nyingi, akibainisha namna ambavyo Bibi Fatima (sa) ni kigezo bora cha kuigwa na wanawake wote wa Kiislamu, na hata wanaume wa Umma wa Mtume Muhammad (saww), kutokana na uchamungu wake, hekima yake, na msimamo wake thabiti katika kutetea ukweli.
-
Kongamano la Waombolezaji wa Kike wa Fatimiyyah Kufanyika Mjini Qom - Iran
Wanawake waumini jijini Qom watafanya matembezi ya maombolezo hadi kwenye kaburi la Shahidi Asiyejulikana katika chuo cha Jami‘atu-z-Zahra (a), wakiomboleza kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a), Mama wa Maimamu wa Ahlul-Bayt (as).
-
Kuendelea kwa Mjadala Mkali Kuhusu Mbio ya Hisani ya Msikiti wa East London; Wito Watolewa kwa Mapitio ya Sera ya Utenganisho wa Jinsia
Baada ya mashambulizi makubwa ya vyombo vya habari vya Uingereza dhidi ya mbio ya hisani iliyoandaliwa na Msikiti wa East London kwa sababu ya utenganishaji wa kijinsia, Tume ya Usawa na Haki za Kibinadamu ya Uingereza imeitangaza kwamba waandaaji wa tukio hilo wamekubali kupitia upya sera zake kabla ya awamu ijayo ya mashindano. Hata hivyo, msikiti huo umeeleza kwamba matukio kama hayo yapo kwa wingi katika maeneo mbalimbali ya Uingereza-ikiwemo mashindano maalumu ya wanawake na vipindi vya kuogelea vinavyoandaliwa katika vituo vya jamii ya Kiyahudi-lakini hakuna hata moja kati ya matukio hayo yaliyowahi kusababisha mjadala au msukosuko kama huu.
-
Bibi Zahra (a.s): Kielelezo cha Juu cha Maadili ya Kibinadamu na Kiislamu Kuhusu Mwanamke
Bibi Zahra (a.s) ni kielelezo cha Mwanamke kamili katika Uislamu - mfano wa ucha Mungu, hekima, upendo wa kifamilia, ushujaa wa kijamii na mapambano ya kiroho. Maisha yake ni dira ya kudumu kwa wanawake na wanaume wote wanaotaka kufikia ukamilifu wa kibinadamu katika njia ya Mwenyezi Mungu.
-
Mwanazuoni wa Kireno atoa ukosoaji mkali kuhusu sheria ya kupiga marufuku burqa
Kupitishwa kwa sheria ya kupiga marufuku burqa nchini Ureno - iliyotetewa kwa kisingizio cha “kulinda usalama na haki za wanawake” - kumezua upinzani kutoka kwa wanaharakati kadhaa. Miongoni mwa wakosoaji hao ni Paulo Mendes Pinto, mtafiti wa masuala ya dini nchini humo, ambaye katika mahojiano na chombo cha habari cha ndani ametoa maoni ya kuvutia kuhusu suala hilo.
-
Rais wa Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu: Vita vya Siku 12 Vilikuwa Vita vya Kwanza vya Akili Bandia (AI)
Rais wa Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Muhammad Mahdi Imanipour, amesema kwamba dunia sasa imeingia katika zama za Akili Bandia (AI) na kwamba uwanja wa mapambano ya kimataifa umebadilika kikamilifu. Amesema pia kuwa vita vya siku 12 vilivyohusisha Iran na utawala wa Kizayuni (Israeli) vilikuwa “vita vya kwanza vya akili bandia”.
-
Magaidi 10, Wakiwemo Wanawake Wawili, Watekwa na Shirika la Taarifa za Kijajusi la Kijeshi la Iraq
Shirika la Taarifa za Kijeshi la Iraq leo limetangaza kuwa katika operesheni mbalimbali za kiusalama, limefanikiwa kuchukua watu 10 wa kigaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi, wakiwemo wanawake 2.
-
Bi Mujtahida Saffati: Vyuo vya kidini vya wanawake vinapaswa kuchukua uongozi wa kielimu wa wanawake katika ulimwengu wa Kiislamu
Profesa mashuhuri wa vyuo vya kidini vya wanawake, katika hafla ya uzinduzi wa mwaka mpya wa masomo, alivitaja “ikhlasi na uchamungu (taqwa)”, “kuungana na uongozi wa Kiislamu (wilaya)”, na “kuzingatia haki za wengine” kuwa ni nguzo tatu muhimu za mafanikio kwa wanafunzi wa fani za dini. Akaeleza kwa msisitizo kuwa: Taasisi za kielimu za wanawake zinapaswa kuchukua uongozi wa kielimu kwa wanawake wa ulimwengu wa Kiislamu, na kutumia uwezo huo kwa ajili ya kusambaza maarifa ya Kiislamu katika ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
Zaidi ya Wanawake na Wasichana 1,000 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
UN: Wanawake na Wasichana 1,025 Wamefariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan. Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) nchini Afghanistan imetangaza kuwa: Jumla ya wanawake na wasichana 1,025 wamepoteza maisha kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea katika maeneo ya mashariki mwa Afghanistan. Taarifa hiyo inasisitiza ukubwa wa athari za kibinadamu, hasa kwa wanawake na watoto, katika tukio hili la maafa ya asili.
-
Washindi wa mwito wa kazi za sanaa na vyombo vya habari kuhusu mashujaa wanawake wametuzwa
Kwa wakati mmoja na kufanyika kwa mkutano wa kumbukizi ya mashujaa wa kike katika mkoa wa Gilan — ambao uliandaliwa kwa lengo la kuthamini hadhi ya juu ya mashujaa wanawake — washindi wa shindano la kitaifa la kazi za sanaa na vyombo vya habari lililokuwa na mada kuu ya mashujaa wa kike walitambulishwa rasmi na kutuzwa kwa mchango wao wa ubunifu.
-
Umoja wa Mataifa:Katika kuelekea miaka 4 ya utawala wa Taliban, wanawake wa Afghanistan wanakabiliwa na mgogoro mkubwa wa haki za wanawake Duniani
Kitengo cha wanawake cha Umoja wa Mataifa, katika kuelekea kumbukumbu ya miaka minne tangu Taliban ichukue madaraka nchini Afghanistan, kimetoa taarifa ikikosoa vikali mwenendo wa kundi hilo kuhusu wanawake wa Afghanistan.
-
Wataalamu wa Kieneo katika Mahojiano na ABNA: Njaa ya kimfumo dhidi ya watu wa Gaza ni uhalifu usio na kifani na doa la aibu juu ya uso wa Binadamu
Jinai za uharibifu kamili wa ardhi, watu na kila dalili za maisha katika ardhi za Palestina inayokaliwa kwa mabavu (na Utawala wa Kizayuni) zinaakisi matamanio ya jeshi la Netanyahu kuwa tawi la uhalifu wa kimataifa katika ardhi za Kiislamu.
-
Baraza Kuu la Fat'wa la Syria: Kusaliti na kuomba msaada kwa adui wa Kizayuni ni haramu
"Adui wa Kizayuni ni adui wa wazi na ambaye uadui wake umethibitika, na kuomba msaada kwake ni miongoni mwa mambo yaliyo haramu kwa yakini."
-
Wananchi wa Yemen wanalenga (wanashambulia) maeneo mbalimbali ya Wazayuni kujibu jinai zinazoendelea kufanywa na Israel
Vikosi vya jeshi la Yemen vimeanzisha operesheni mpya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya utawala wa Israel, hatua ambayo kwa mujibu wa duru za Yemen, ilifanyika kujibu mauaji ya raia huko Gaza.
-
Mashambulio ya kinyama ya utawala wa Kizayuni katika baadhi ya Makazi ya raia Jijini Tehran
Katika siku ya tatu ya uvamizi wake dhidi ya nchi yetu, utawala haramu wa Kizayuni ulilenga baadhi ya maeneo ya Tehran katika mfululizo wa mashambulizi makali.