Msafara wa Kimataifa wa Ustahimilivu (al-Sumud) umetangaza kuwa Jeshi la Majini la utawala wa Kizayuni limeushambulia Msafara wa Uhuru uliokuwa ukielekea Gaza kwa lengo la kuvunja mzingiro unaoendelea dhidi ya eneo hilo.
Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza leo Jumapili kuwa, kutokana na vita na kuzidi kwa mzingiro unaoendelea wa jeshi la utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza, Wapalestina 1,500 wamepoteza uwezo wao wa kuona.