Siku hii pia inakumbusha shahada ya Imam Hassan (a.s), Imam wa pili katika Ahlul-Bayt (a.s), aliyefahamika kwa msimamo wake wa amani na kujitolea kwake kwa ajili ya haki. Kifo chake ni alama ya mapambano ya kudumu kwa ajili ya uadilifu na uongofu.
Dk. Pourmarjan, mtetezi kwa bidii wa elimu, alieleza dhamira ya Ubalozi wa Iran Nchini Kenya kuwa ni kutoa ufadhili wa masomo kwa Wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu, kwa lengo la kuwapa fursa bora zaidi kwa maisha yao bora ya baadaye.