udhaifu

  • Majibu kwa Shubuhati Zinazohusu Wilayat na Uimamu, na Siri Iliyofichika katika Tukio la Ghadir

    Majibu kwa Shubuhati Zinazohusu Wilayat na Uimamu, na Siri Iliyofichika katika Tukio la Ghadir

    «وَلَوْ شِئْتُ أَنْ أُسَمِّیَ الْقَائِلِينَ بِذَلِكَ بِأَسْمَائِهِمْ لَسَمَّيْتُ ... وَلَكِنِّي وَاللَّهِ فِي أُمُورِهِمْ قَدْ تَكَرَّمْتُ» "Na kama ningetaka kuwataja wale waliotoa maneno hayo kwa majina yao, basi ningewataja. Lakini kwa hakika, kwa jina la Mwenyezi Mungu, nimewatendea kwa ukarimu na staha katika mambo yao." Kauli hii inaonyesha kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliwajua wanafiki mmoja baada ya mwingine na alikuwa na uwezo wa kuwataja waziwazi. Hata hivyo, kutokana na hekima, ukarimu na maslahi ya Umma wa Kiislamu, hakufanya hivyo. Je, jambo hili lina maana kwamba Mtume (s.a.w.w.) alipuuza wajibu wake? Hapana. Kusudi la utume halikuwa tu kufichua watu, bali lilikuwa kuongoza jamii, kuwapa nafasi ya kutubia na kurejea katika haki, pamoja na kulinda umoja wa Waislamu dhidi ya fitina kubwa zaidi. Kama Mtume (s.a.w.w.) angewataja wanafiki wote hadharani, huenda baadhi yao wangetangaza uasi wao dhidi ya Uislamu, jambo ambalo lingeweza kusababisha migawanyiko mikubwa na hata vita vya ndani katika jamii changa ya Kiislamu. Kwa hiyo, kunyamaza kwake kuhusu majina yao hakukuwa udhaifu wala kuacha wajibu, bali ilikuwa ni sehemu ya hekima ya uongozi wa Mtume katika kuhifadhi maslahi makubwa ya dini na jamii.

  • Ongezeko lisilo la kawaida la kesi za ujasusi kwa manufaa ya Iran ndani ya Israel

    Ongezeko lisilo la kawaida la kesi za ujasusi kwa manufaa ya Iran ndani ya Israel

    Gazeti la The Jerusalem Post limeripoti kuongezeka kwa wasiwasi wa vyombo vya usalama vya Israel kufuatia ongezeko lisilo la kawaida la kesi za ujasusi zinazodaiwa kuwa kwa manufaa ya Iran. Kwa mujibu wa ripoti ya Shin Bet, zaidi ya kesi 150 zimefunguliwa ndani ya miaka miwili iliyopita, hali inayoelezwa kuwa ni kipindi chenye msongamano mkubwa zaidi wa shughuli za kijasusi za Iran ndani ya Israel, na inayoibua maswali kuhusu udhaifu wa kiusalama na changamoto za kukabiliana na upenyezaji.

  • Wazayuni Wajibu Kauli za Trump: “Sisi Hatuko Chini ya Utawala wa Marekani!”

    Wazayuni Wajibu Kauli za Trump: “Sisi Hatuko Chini ya Utawala wa Marekani!”

    Hali ya sasa ya utawala wa Kizayuni (Israel) kutokana na utegemezi wake mkubwa kwa siasa za Marekani pamoja na changamoto za ndani, imegeuka kuwa moja ya hatua muhimu za kihistoria katika uhusiano wa kimataifa wa utawala huo. Mabadiliko haya yanaweza kusababisha mabadiliko ya kimkakati katika siasa za Israel na namna inavyoshirikiana na jamii ya kimataifa na Wapalestina.

  • Kurudi kwa Tishio la ISIS nchini Syria / Mashambulizi ya Kigaidi Yasambaa Raqa na Hasaka

    Kurudi kwa Tishio la ISIS nchini Syria / Mashambulizi ya Kigaidi Yasambaa Raqa na Hasaka

    Licha ya kupoteza udhibiti wa ardhi, kundi la ISIS bado lina uwezo wa kufanya mashambulizi ya milipuko, uvamizi wa ghafla na mauaji ya kulenga watu binafsi katika maeneo ya Raqa na Hasaka.

  • Shamkhani: Sisi sote tuko kwenye meli moja / Inasikitisha ikiwa meli itapata doa au udhaifu

    Shamkhani: Sisi sote tuko kwenye meli moja / Inasikitisha ikiwa meli itapata doa au udhaifu

    Mwakilishi wa Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi katika Baraza Kuu la Ulinzi, akisisitiza umuhimu wa kudumisha umoja na mshikamano wa ndani, alisema: "Sisi sote tuko kwenye meli moja ambayo mashahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu waliizindua, na inasikitisha ikiwa, kwa bahati mbaya, tofauti zetu zitasababisha doa au pengo katika meli hii."

  • Pezeshkian: Shambulio kwenye taasisi za nyuklia ni kielelezo tosha kuwa Marekani ni msababishaji mkuu wa hatua za uhasama za Kizayuni dhidi ya Iran

    Pezeshkian: Shambulio kwenye taasisi za nyuklia ni kielelezo tosha kuwa Marekani ni msababishaji mkuu wa hatua za uhasama za Kizayuni dhidi ya Iran

    Jibu kali la Iran lilikuwa ujumbe wa wazi kwa wahalifu wa Kizayuni. Marekani, baada ya majibu makali na ya kuadabisha kutoka kwa vikosi vya ulinzi vya nchi yetu, na kuona udhaifu na ulegeaji wa wazi wa utawala wa Kizayuni, hawakuweza kuvumilia ispokuwa kutojitokeza na kuamua kujitumbukiza rasmi kwenye dimbwi la uhasama."