umoja wa kitaifa
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran Asisitiza Umuhimu wa Umoja wa Kitaifa na Kusema Hakuna Tofauti Kuhusu Kulipiza Kisasi Dhidi ya Adui
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama ya Iran, Hojjat al-Islam Gholam-Hossein Mohseni Ejei, amesisitiza umuhimu wa kulinda na kuimarisha umoja wa kitaifa na mshikamano, akiwataka wananchi kuwa macho dhidi ya wachochezi wa fitina, wanaoeneza uvumi na wanafiki.
-
JMAT Yatoa Wito wa Maridhiano na Amani, Funga ya Siku Tatu na Maombi ya Kitaifa kwa ajili ya Umoja wa Kitaifa
Mwenyekiti wa JMAT, Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum, amesema: "Matukio ya baada ya Uchaguzi yameacha majeraha ya kisaikolojia na kuchochea hisia za kidini, hivyo kunahitajika hatua za haraka kuimarisha umoja wa kitaifa. Amehimiza maombi hayo yashirikishe waumini wa madhehebu zote na kufanyika kwa mfumo mmoja na Kwa siku moja kitaifa".
-
Jukumu la Marajii wa Kidini wa Kishia katika;
"Kulinda Umoja wa Kitaifa na Utambulisho wa Iran / Sehemu ya Saba: Kisa cha Kuokolewa kwa Lugha ya Taifa ya Iran na Ukombozi wa Azarbaijan"
Kulinda umoja wa ardhi na kuzingatia utambulisho wa kidini ni miongoni mwa masuala yaliyokuwa yakipewa umuhimu mkubwa na viongozi wa kidini katika ardhi za Kiislamu. Kiasi kwamba kila aina ya uvamizi au shambulio dhidi ya ardhi za Kiislamu ilikabiliwa na mwitikio mkali kutoka kwao. Uvamiuzi wa Azarbaijan wakati wa Vita vya Pili vya Dunia na juhudi za kuutenga mkoa huo kutoka Iran ni miongoni mwa mambo yaliyodhihirisha tena ushawishi wa uongozi wa kidini katika kulinda umoja wa ardhi ya nchi. Aidha, kulinda utambulisho wa kitaifa wa Kiairani pia lilikuwa ni mojawapo ya masuala yaliyopatiwa umuhimu maalum na viongozi (Marajii) wa kidini katika kipindi cha utawala wa Pahlavi.
-
Kiongozi wa Mapinduzi katika hotuba ya televisheni kwa taifa la Iran:
''Umoja wa Kitaifa wa Iran ni ule ule wa Tarehe 13 Juni 2009; Wote wanawajibika''
Mheshimiwa Ayatollah Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, usiku huu katika hotuba ya televisheni akiwahutubia watu, aliueleza umoja na mshikamano wa kudumu wa taifa la Iran kuwa ni ngumi ya chuma juu ya kichwa cha adui.
-
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa jukumu la UNIFIL nchini Lebanon hadi mwisho wa mwaka 2026.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeamua kuongeza muda wa jukumu la wanajeshi wa UNIFIL kusini mwa Lebanon kwa mara ya mwisho.
-
Rais wa Iran: Mashambulizi ya Israel na Marekani dhidi ya Iran Yameleta Umoja wa Kitaifa Usio na Mfano
"Leo tunashuhudia kwa macho yetu kuwa kila Muirani - awe ni mfuasi wa Serikali au mpinzani wake - amekuwa sauti moja katika kutetea hadhi, uhuru, na mamlaka ya nchi yetu".