Shirika la Habari la Kimataifa AhlulBayt (as) -ABNA-Kundi la wananchi wa Venezuela limefanya mkusanyiko mbele ya ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mji mkuu Caracas, kuonesha mshikamano wao na watu wa Iran dhidi ya uvamizi wa utawala wa Kizayuni.
Katika maandamano hayo ya amani, raia wa Venezuela walibeba mabango na kupeperusha bendera za Iran huku wakilaani vikali mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran. Walitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kusimama dhidi ya uchokozi wa utawala huo wa Kizayuni.
Wamesema kuwa mshikamano huu unaonesha udugu wa mataifa huru ya dunia na kupinga dhulma dhidi ya raia wasio na hatia. Waandamanaji walisisitiza kuwa Venezuela inasimama pamoja na Iran katika kupigania haki, heshima ya kitaifa, na amani ya kweli duniani.
Your Comment