Chuo Kikuu
-
Mtindo wa Maisha wa Fatima (a.s) na Kauli “Jirani Kwanza Kisha Nyumba”: Kigezo cha Kiungu Kukabiliana na Ubinafsi wa Kisasa
Katika kuelekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (a.s), kikao cha kisayansi kuhusu “Mtindo wa Maisha wa Fatima na Mafundisho ya al-jār thumma al-dār (Jirani Kwanza Kisha Nyumba)” kiliandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Habari la ABNA, ambapo watafiti walibainisha changamoto za familia katika enzi ya kisasa—hususan mgongano kati ya fikra za kisasa na mwenendo wa kimapokeo. Katika kikao hicho, mfano wa Maisha wa Bibi Zahra (a.s) uliwasilishwa kama muongozo wa kiungu na wa vitendo unaojenga maadili ya kuwajali wengine na kuleta mizani kati ya haki na wajibu ndani ya familia.
-
Profesa wa Chuo Kikuu cha Indonesia katika mahojiano na ABNA:
“Iran ni mfano wa kipekee wa maendeleo ya kisayansi na uimara dhidi ya vikwazo – ni lazima mtu aione kwa macho yake”
Amesema kuwa uongo mwingi kuhusu Iran unatolewa na taasisi zinazopingwa na msimamo wa Iran wa kusimama dhidi ya Marekani na Israel. Hata hivyo, baada ya vita vya siku kumi na mbili, wanafikra wengi duniani wamekiri wazi kwamba Iran ndilo taifa pekee lililosimama dhidi ya dhulma kwa njia ya kivitendo, si kwa maneno tu.
-
Afisa wa Kijeshi wa Iraq: Kamwe Haitatokea kusahau msaada wa Iran
Rais wa Chuo cha Ulinzi wa Iran: “Tunafurahia sana kwamba maafisa wa Iraq wanasoma katika Chuo cha Uongozi na Makao Makuu ya Jeshi la Iran. Ingawa kuna uwezekano wa kusoma katika nchi nyingine, tunapendelea maafisa wetu wapate elimu yao hapa Iran, kwa kuwa tunajua wanapata mafunzo bora chini ya wakufunzi wenye kiwango cha juu cha kielimu na kitaaluma.”
-
Meja Jenerali Musawi: Jeshi la Ukombozi litatoa jibu lililo juu ya fikra za waonevu (waovu)
Rais wa Makao Makuu ya Majeshi ya Ulinzi wa Iran amesema: Tunawapa uhakika wananchi wa Iran wenye heshima na ushujaa kuwa, vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu kwa kutegemea uwezo wao, ubunifu na mshangao wa kimkakati, viko tayari kukabiliana na vitisho vyovyote vya madhalimu na waonevu wa dunia kwa majibu ya wakati muafaka, makali, ya kujutia na yaliyo zaidi ya fikra zao.
-
Wimbi la Kukatisha Ushirikiano wa Vyuo Vikuu Duniani na Israel
Chuo Kikuu cha Amsterdam kimefuta mpango wa kubadilishana wanafunzi na Chuo Kikuu cha Kiebrania cha Yerusalemu, huku Jumuiya ya Ulaya ya Wanaanthropolojia wa Kijamii ikitangaza marufuku ya aina yoyote ya ushirikiano na Israel.
-
Chuo Kikuu cha al-Mustafa (s) Dar es Salaam - Tanzania Chaandaa Kongamano la Kielimu Kuhusu: "Dakika za Mwisho za Maisha ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)"
Mtoa Mada: Sheikh Taqi Zakariya. Tarehe: Jumamosi, 16-08-2025. Muda: Kuanzia Saa 4:00 Ask Asubuhi hadi 6:00 Mchana. Eneo: Muswalla wa Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam. Mwaliko huu ni kwa Wote.
-
Hujjat-ul-Islam Aali: Msaada kwa wengine unarudishwa (unafidiwa) mara nyingi zaidi na Mwenyezi Mungu
Mwalimu wa chuo kikuu na shule ya kidini alieleza kuwa kusaidia na kutatua matatizo ya wengine ni chanzo cha kupata malipo mengi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Alisisitiza kwamba sehemu ya kila mtu katika neema ya Mwenyezi Mungu inategemea uwezo wake wa kupokea, na ili kufaidika zaidi, ni lazima kuongeza uwezo huu.